Kilimanjaro: TAKUKURU yazuia milioni 329 ya kununua jenereta zisizo na ubora

Kilimanjaro: TAKUKURU yazuia milioni 329 ya kununua jenereta zisizo na ubora

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Kilimanjaro, imezuia Sh329 milioni zilizopangwa kutumika kununua jenereta mbili kwa ajili ya iliyokuwa Mamlaka ya Uendeshaji na Uendelezaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KADCO), baada ya kugundua kuwa hazina ubora unaotakiwa.

Akizungumza kuhusu ripoti ya robo ya kwanza ya mwaka leo Jumatatu, Novemba 11, 2024 Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kilimanjaro, Sabas Salehe, amesema jenereta hizo zilikuwa na matatizo, ikiwemo injini zenye kutu na sehemu nyingine kupakwa rangi tu, ili kuficha hali yake.

Soma Pia: TAKUKURU Dodoma yakamata Tani 120 za Nondo zisizo na ubora zilizopangwa kujenga Barabraba ya Ihumwa-Bandari Kavu

"Tulipofanya ufuatiliaji, tulibaini kuwa Kadco ilikuwa inakusudia kununua jenereta mbili kutoka Kampuni ya African Power Machinery (APM) kwa gharama ya Sh328.4 milioni," amesema Salehe.

Amefafanua kuwa jenereta hizo zilizowasilishwa zilikuwa na kasoro kama vile nyaya tofauti na injini zilizochakaa.
 
Kwa Maafisa Elimu Kata zote, Wakuu wa Shule za Serikali za Msingi na Sekondari, Moshi Manispaa, Kilimanjaro

Mkurugenzi wa Manispaa, Mwajuma Nasombe, kwa mamlaka aliyonayo, anawataka watumishi wote kuchangia fedha kwa ajili ya "Get Together" ya Watumishi Wote wa Moshi Manispaa, ikiwa ni sherehe ya kuukaribisha Mwaka 2025. Sherehe hii itafanyika tarehe 01.02.2025.

Kiwango cha Kuchangia

Wakuu wa Idara na Vitengo, Waratibu Elimu Kata, Wakuu wa Shule za Sekondari, na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi: Tsh 50,000/-
Walimu Wote: Tsh 30,000/-
watumishi wengine: Tsh 20,000/-

Mwisho wa kuchangia ni siku ya 26.01.2025 bila kukosa.

Angalizo

Hata hivyo, ni muhimu kuwajulisha watumishi kuhusu baadhi ya masuala yanayohusiana na zoezi hili la kuchangia fedha:

1. Ushirikishwaji: Watumishi wengi hawajashirikishwa kabla ya tangazo hili. Ushirikishwaji wa awali ni muhimu ili kuhakikisha kuwa kila mmoja anafahamu lengo la michango hii.

2. Kamati ya Kuratibu: Hakuna kamati iliyoundwa kwa ajili ya kuratibu zoezi hili. Kukosekana kwa kamati kunaleta hofu miongoni mwa watumishi kuhusu matumizi ya fedha zao.

3. Muda wa Tangazo: Tangazo hili limetolewa muda mfupi sana, kuanzia tarehe 23.01.2025 na mwisho wa kuchangia ni tarehe 25.01.2025. Hii inapunguza nafasi ya watumishi kupanga na kujiandaa kwa michango yao.

4. Mshahara na Madeni: Watumishi wengi wamepokea mshahara wao na tayari wameshatumia kwa kulipa madeni wanayodaiwa. Hali hii inawafanya wengi kuwa na wasiwasi kuhusu kutoa michango zaidi.

5. Kujulishwa kwa Mkuu wa Wilaya: Mkuu wa Wilaya hajajulishwa kuhusu ukusanyaji huu wa fedha za michango, jambo ambalo ni muhimu ili kuweza kufuatilia matumizi ya fedha hizo.

6. *Kuchoshwa na Mkurugenzi:*Watumishi wengi wanasema wanachoshwa na mkurugenzi huyu, kwani mara kwa mara anaitisha michango. Wengi wanahisi kuwa huenda hii ni sehemu ya fedha za kampeni yake kuelekea kwenye uchaguzi wa ubunge.

Ombi

Kwa kuzingatia masuala haya, tunaomba zoezi hili lisitishwe hadi pale ambapo itakapofanyika mabadiliko yanayohitajika ili kuhakikisha kuwa watumishi wanashirikishwa ipasavyo na michango inakusanywa kwa njia ya uwazi na uaminifu.
Hii itasaidia kujenga uhusiano mzuri kati ya watumishi na uongozi wa manispaa.

Tunatumai kuwa maelezo haya yatasaidia katika kueleweka kwa sababu za kutokubali michango hii na kutafutwa kwa suluhisho la kudumu litakalowafaidi watumishi wote wa Moshi Manispaa.

Ahsanteni.
 
Back
Top Bottom