LGE2024 Kilimanjaro: Wasiojulikana waiba madaftari ya kujiandikishia, wengine wachoma moto Ofisi ya Mtendaji

LGE2024 Kilimanjaro: Wasiojulikana waiba madaftari ya kujiandikishia, wengine wachoma moto Ofisi ya Mtendaji

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeongeza muda wa kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa wakazi wa Kijiji cha Kikelelwa Kata ya Tarakea Motamburu wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro hadi Oktoba 28,2024.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu baada ya kutembelea kituo cha kujiandikisha cha Josho, ambapo watu wasiojulikana wameiba vitabu viwili vya kujiandikishia vikiwa tayari na majina ya watu waliojiandikisha.

Babu amesema tukio hilo limetokea usiku wa Oktoba 18,2024 ambapo ameagiza kutafutwa kwa wahusika ili hatua kali zichukuliwe dhidi yao.

Tayari vitabu hivyo viliishaandikisha wakazi 1,105 wa Kijiji cha Kikelelwa, hivyo kuongezwa kwa muda huo kutawapa nafasi ya kujiandikisha tena.

Mbali na tukio hilo, Babu pia ametembelea kituo cha Lokoro kilichopo katika Kijiji cha Kikelelwa ambapo watu wasiojulikana wamechoma moto ofisi ya Mtendaji wa kijiji ambapo daftari la waliojiandikisha lilikuwemo ndani, hivyo kuunguza nyaraka hizo na nyingine za Serikali.

Chanzo: TBC
 
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imeongeza muda wa kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa wakazi wa Kijiji cha Kikelelwa Kata ya Tarakea Motamburu wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro hadi Oktoba 28,2024.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu baada ya kutembelea kituo cha kujiandikisha cha Josho, ambapo watu wasiojulikana wameiba vitabu viwili vya kujiandikishia vikiwa tayari na majina ya watu waliojiandikisha.

Babu amesema tukio hilo limetokea usiku wa Oktoba 18,2024 ambapo ameagiza kutafutwa kwa wahusika ili hatua kali zichukuliwe dhidi yao.

Tayari vitabu hivyo viliishaandikisha wakazi 1,105 wa Kijiji cha Kikelelwa, hivyo kuongezwa kwa muda huo kutawapa nafasi ya kujiandikisha tena.

Mbali na tukio hilo, Babu pia ametembelea kituo cha Lokoro kilichopo katika Kijiji cha Kikelelwa ambapo watu wasiojulikana wamechoma moto ofisi ya Mtendaji wa kijiji ambapo daftari la waliojiandikisha lilikuwemo ndani, hivyo kuunguza nyaraka hizo na nyingine za Serikali.

Chanzo: TBC
Watapatikana tu soon, na hatua kali za kisheria dhidi yao zitachukuliwa ili iwe fundisho kwa wengine wenye nia, mipango na tabia kama hiyo 🐒
 
watapatikana tu soon, na hatua kali za kisheria dhidi yao zitachukuliwa ili iwe fundisho kwa wengine wenye nia, mipango na tabia kama hiyo 🐒
Hawo ni ccm ndio wanaofanya hayo ili ionekane yameibiwa ila ni mbinu mbovu y na ujinga wa kufanya hivyo. Kwanini ccm mamjiamini na kila siku mnakuja na nyimbo za kuwa mtashinda kwa halali?

Kuandikisha watu kwenye kambi za jkt, kuandikisha watu kwenye nyumba za makarani, kuandikisha huku mnaacha nafasi kusudi ili mpate kujaza watu wengine hewa, yaani hamna mnaloweza kiushindana.
 
Kujiandikisha tu ilikuwa taabu, kupiga kura ndio itakuwa vichekesho.

Nakwambia watasubiri wanafunzi warejee madarasani ndio wakapige kura, la sivyo watarudia utaratibu wao wa kuteua watawala nchi nzima kama 2019.
 
Sijui lini ulishatoa kauli kama hiyo kw wa2 walioteka na kupoteza wengine ...!
 
Washindwe kuwakamata watekaji waweze kuwakama waiba daftari, upo serious kweli?
are you sure wezi wa madaftari ya wapiga kura ndiyo wanahusika kuwachukua misukule na kuhusika na kafara kwa hicho kisingizio chako?

Serikali haimini katika ushirikina, ramli na uchawi gentleman 🐒
 
Hawo ni ccm ndio wanaofanya hayo ili ionekane yameibiwa ila ni mbinu mbovu y na ujinga wa kufanya hivyo. Kwanini ccm mamjiamini na kila siku mnakuja na nyimbo za kuwa mtashinda kwa halali?

Kuandikisha watu kwenye kambi za jkt, kuandikisha watu kwenye nyumba za makarani, kuandikisha huku mnaacha nafasi kusudi ili mpate kujaza watu wengine hewa, yaani hamna mnaloweza kiushindana.
unataka kusema ni kama wale wa kila chama kinachofanya uchaguzi wao wa ndani wanapotezana kwa ushirikina, ramli chonganishi, kutoana kafara na kuchukuana misukule kwaajili ya kupata uongozi, huku wakisingizia wengine wasiohusika, sijui nini huko right?🐒
 
Back
Top Bottom