Nashukuru sana kwa hiyo topic naomba hata mie nichangie, Kilimo cha Alizeti sina uzoefu nacho ila ninachoweza kukusaidia tu ni uzoefu nilionao wa mwaka mmoja nikiendesha kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti hapa Dar es salaam.
Uzalishaji wa mbegu za alizeti kwa maeneo ya Iringa, Singida, Dodoma, n.k bado upo chini ukilinganisha ni demand ya mafuta yatokanayo na mimea ambayo yanakiwango kidogo cha LEHEMU (low level of cholestrol), ukiangalia mfano importation ya edible oil from indonesia, and other Asian country is almost 80% ya demand ya edible oil kwa nchi nzima, wakati mafuta haya yanakiwango kikubwa cha LEHEMU, na ukisoma machapisho (articles za PWC,World Bank na RLDC - ambazo zinaelezea Alizeti, utaona hiyo shortfall na kuwa inchi yetu inatumia fedha nyingi sana za kigeni kwenye ununuzi wa mafuta ghafi kutoka Asian country).
Ukitoa mafuta ya disel, petrol na mafuta ya taa, mafuta ghafi ya kula yanachukua nafasi ya pili kwa kutumia fedha za kigeni kwenye uagizaji wake nje ya nchi.
Hivyo basi demand ya mbegu kwa viwanda vidogo vidogo na vikubwa vya kukamua mafuta hayo ni kubwa na inasababisha kuwepo na shortage ya hizo mbengu. Mfano mwaka huu ngunia moja la kg 65-70 kwa sasa linauzwa kati ya Tsh36,000/= hadi 45,000/=(the current price is 45,000 - 60,000 per kg January 2011)) kutegemea na eneo wakati huo huo kwa mwaka jana ngunia hilo hilo liliweza kuuzwa kwa Tsh 22,000/= hadi 35,000/= kwa kipindi hicho hicho.
Point nayotaka ku-raise hapa ni kuwa ongezeko kubwa la viwanda vidogo vidogo limeongeza demand ya mbegu, na awareness ya watu kuhusu mafuta yenye kiwango kidogo cha LEHEMU imesababisha kuwepo na demand ya mafuta hayo.
Kwa mantiki hiyo basi kama unataka kulima kilimo cha KIBEPARI na cha KISASA kwa kuangalia ile opened window kwa ajili ya KILIMO KWANZA, that is a great opportunity, go for it!!!
My take: Ila kama tu unataka kwa ajili ya ku access ile mikopo ya TIB then upeleke pesa kwingine then i don't have any comment.
Mimi ni mdau naomba tushirikiane.