Yoyo Zhou
Senior Member
- Jun 16, 2020
- 126
- 215
Katika miaka ya hivi karibuni serikali za nchi za Afrika Mashariki zimepata mafanikio makubwa katika vita dhidi ya mihadarati na kupongezwa na jumuiya ya kimataifa. Kwa sasa upatikanaji wa dawa za kulevya kama vile Cocaine, Heroinna dawa nyingine kama hizo umepungua sana.
Mwaka 2017 Lesotho ilikuwa ni nchi ya kwanza barani Afrika kuhalalisha matumizi ya bangi kwa sababu za kimatibabu, mwaka 2019 Zambia ilihalalisha uzalishaji wa bangi kwa ajili ya kusafirisha nje ya nchi, mwaka 2018 mahakama ya katiba ya Afrika Kusini ilitangaza kuwa matumizi ya bangi sio kosa tena kisheria, na kuhakakisha sekta ya bangi ambayo inatarajiwathamani yake kwa mwaka 2023 itafikia dola za kimarekani bilioni 1.7.
Kuonekana faida ya kiuchumi kwenye biashara ya bangi, na tafiti za kisayansi kuthibitisha kuwa zao hilo linaweza kuwa malighafi kwenye viwanda vya dawa, kumefanya baadhi ya nchi zianze kufikiria njia za kunufaika na zao hilo. Lakini bado jamii ina wasiwasi na uamuzi kama huo. Mwaka 2017 kamati ya afya ya baraza la seneti ya Kenya ilitaka serikali iangalieuwezekano wa kuhalalisha bangi kwa ajili ya matumizi ya kimatibabu lakini mwito huo haukuitikiwa na serikali. Kumekuwa na habari kuwa nchini Tanzania wamejitokea wawekezaji wanaotaka kulima zao la bangi, nchini Uganda serikali ilijadili uwezekano wa kutoa ruhusa ya kulima zao hilo kwa sababu za kibiashara, na Zimbabwe ilikwenda hatua zaidi na kubadilisha sheria zake kuhusiana na bangi, na kuruhusu kilimo cha bangi kwenye eneo la gereza kuu la Harare, lakini bangi hiyo si kwa ajili ya matumizi ya gereza bali ni malighafi ya kiwanda cha dawa.
Licha ya kuwa ni serikali ya Afrika Kusini ambayo imesema matumizi ya bangi si kosa kisheria katika nchi hiyo, kwenye nchi nyingi za Afrika kilimo, biashara na hata matumizi ya bangi hasa uvutaji, ni kosa ambalo limefanya watu wengi wafungwa. Licha ya kuwa kwa sasa kuna sauti ya kutaka kilimo cha zao hilo kiruhusiwe, kuna upinzani mkubwa kutoka wahafidhina na makasisi wanaona kuwa bado hakuna njia za kudhibiti na kuhakikisha kilimo cha bangi kinasimiwa bila kuleta madhara katika jamii.
Wakati wa maadhimisho ya siku ya kupambana na dawa za kulevya, Tanzania ilitangazwa kuwa imepata mafanikio makubwa kwenye kupambana na mihadarati. Lakini siku chache baadaye imeonekana kuwa mafanikio ya serikali ya Tanzania kwenye kupambana na dawa hizo, kumefanya uzalishaji haramu wa bangi uongezeke na kuleta changamoto kubwa. Kwa sasa suala la kuhalalisha kilimo cha bangi hata kama ni kwa matumizi ya kimatibabu, ni changamoto kubwa kwa nchi za Afrika kwa kuwa bado hakuna njia za kuhakikisha zao hilo hakitatumika kwa matumizi yasiyopangwa
Mwaka 2017 Lesotho ilikuwa ni nchi ya kwanza barani Afrika kuhalalisha matumizi ya bangi kwa sababu za kimatibabu, mwaka 2019 Zambia ilihalalisha uzalishaji wa bangi kwa ajili ya kusafirisha nje ya nchi, mwaka 2018 mahakama ya katiba ya Afrika Kusini ilitangaza kuwa matumizi ya bangi sio kosa tena kisheria, na kuhakakisha sekta ya bangi ambayo inatarajiwathamani yake kwa mwaka 2023 itafikia dola za kimarekani bilioni 1.7.
Kuonekana faida ya kiuchumi kwenye biashara ya bangi, na tafiti za kisayansi kuthibitisha kuwa zao hilo linaweza kuwa malighafi kwenye viwanda vya dawa, kumefanya baadhi ya nchi zianze kufikiria njia za kunufaika na zao hilo. Lakini bado jamii ina wasiwasi na uamuzi kama huo. Mwaka 2017 kamati ya afya ya baraza la seneti ya Kenya ilitaka serikali iangalieuwezekano wa kuhalalisha bangi kwa ajili ya matumizi ya kimatibabu lakini mwito huo haukuitikiwa na serikali. Kumekuwa na habari kuwa nchini Tanzania wamejitokea wawekezaji wanaotaka kulima zao la bangi, nchini Uganda serikali ilijadili uwezekano wa kutoa ruhusa ya kulima zao hilo kwa sababu za kibiashara, na Zimbabwe ilikwenda hatua zaidi na kubadilisha sheria zake kuhusiana na bangi, na kuruhusu kilimo cha bangi kwenye eneo la gereza kuu la Harare, lakini bangi hiyo si kwa ajili ya matumizi ya gereza bali ni malighafi ya kiwanda cha dawa.
Licha ya kuwa ni serikali ya Afrika Kusini ambayo imesema matumizi ya bangi si kosa kisheria katika nchi hiyo, kwenye nchi nyingi za Afrika kilimo, biashara na hata matumizi ya bangi hasa uvutaji, ni kosa ambalo limefanya watu wengi wafungwa. Licha ya kuwa kwa sasa kuna sauti ya kutaka kilimo cha zao hilo kiruhusiwe, kuna upinzani mkubwa kutoka wahafidhina na makasisi wanaona kuwa bado hakuna njia za kudhibiti na kuhakikisha kilimo cha bangi kinasimiwa bila kuleta madhara katika jamii.
Wakati wa maadhimisho ya siku ya kupambana na dawa za kulevya, Tanzania ilitangazwa kuwa imepata mafanikio makubwa kwenye kupambana na mihadarati. Lakini siku chache baadaye imeonekana kuwa mafanikio ya serikali ya Tanzania kwenye kupambana na dawa hizo, kumefanya uzalishaji haramu wa bangi uongezeke na kuleta changamoto kubwa. Kwa sasa suala la kuhalalisha kilimo cha bangi hata kama ni kwa matumizi ya kimatibabu, ni changamoto kubwa kwa nchi za Afrika kwa kuwa bado hakuna njia za kuhakikisha zao hilo hakitatumika kwa matumizi yasiyopangwa