Kilimo cha Maharage: Mbinu za kulima, Ushauri na Masoko yake

Unaweza kulima kwa greenhouse na makisio ya gharama ya greenhouse ya hekari 2 ni tshs ngapi na unaweza kupata ngunia ngapi kipindi cha mavuno?
Ni heka siyo hekari.......Ekari moja ni kilo 600 mpk 1200 mavuno......heka moja ni sawa na Ekari 2.5 sasa hapo jipigie mahesabu mwenyewe.
 
Yana deal maana kilo 1200x1800(bei ya jumla) ni sh 2,160,000

Afu naona hayana changamoto sana kama mahindi cos yenyewe unatumia mwezi mmoja tu kuyapalilia tangu umeyapanda na baada ya hapo unavuna miezi miwili baadae na uzuri wake soko lake ni constant sana.
 
Kilimo cha magazetini kitamu sana ila utamu wa ngoma anajua mchezaji
 
Habari za saa wakuu wangu?

Bila kupoteza muda niende katika jambo husika kwenu wahenga na wasamaria mnisaidie maarifa...

Wakuu kama mhitimu bila kupoteza muda ktk kutafuta na kusubiri kupata ajira mwaka huu nilifanya maamuzi ya kuwekeza fedha yangu ya akiba ktk kilimo cha maharage huko Gairo Morogoro, namshukuru Mungu pamoja na changamoto za ukosefu wa mvua nimefanikiwa kupata mavuno yakuridhisha kiasi chake, nililima maharage ya njano na soya... Ktk hali ya ugeni ktk sekta hii na changamoto katika kumuuguza mama ambae kwa mapenzi ya Mungu aliona mama apumzike sikufanikiwa kufanya tafiti za kutosha juu ya soko la maharage

Sasa nimevuna na ninao mzigo kubwa wastani wa tani 5 na bado sijamaliza kuvuna ni maharage ya soya na njano, kwa yeyote mwenye kujua soko lake kwa wafanyabiashara ama taasisi yoyote tafadhali niunganishe nao, natanguliza shukrani za dhati

1 kg ni 1400 bei yaweza kupungua kulingana na ukubwa wa mzigo pia tutaweza fanya kazi endelevu hata baada ya msimu kupita, gharama za usafiri kwa asilimia kubwa zitakuwa kwangu, karibu pm mkuu
 
Nenda sokoni kwa uhakika zaidi
 
Duhh Tani 5 halafu unasema kuwa hapo ndio ulilima kwa changamoto!

Mkuu si mihela hiyo?

Uko mkoa gani mkuu? Jaribu kwenda katika masoko makuu ya mkoa ambao upo kisha watafute madalali Bila Shaka wataweza kutatua Tija yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…