Habari za saa wakuu wangu?
Bila kupoteza muda niende katika jambo husika kwenu wahenga na wasamaria mnisaidie maarifa...
Wakuu kama mhitimu bila kupoteza muda ktk kutafuta na kusubiri kupata ajira mwaka huu nilifanya maamuzi ya kuwekeza fedha yangu ya akiba ktk kilimo cha maharage huko Gairo Morogoro, namshukuru Mungu pamoja na changamoto za ukosefu wa mvua nimefanikiwa kupata mavuno yakuridhisha kiasi chake, nililima maharage ya njano na soya... Ktk hali ya ugeni ktk sekta hii na changamoto katika kumuuguza mama ambae kwa mapenzi ya Mungu aliona mama apumzike sikufanikiwa kufanya tafiti za kutosha juu ya soko la maharage
Sasa nimevuna na ninao mzigo kubwa wastani wa tani 5 na bado sijamaliza kuvuna ni maharage ya soya na njano, kwa yeyote mwenye kujua soko lake kwa wafanyabiashara ama taasisi yoyote tafadhali niunganishe nao, natanguliza shukrani za dhati
1 kg ni 1400 bei yaweza kupungua kulingana na ukubwa wa mzigo pia tutaweza fanya kazi endelevu hata baada ya msimu kupita, gharama za usafiri kwa asilimia kubwa zitakuwa kwangu, karibu pm mkuu