Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Wadau naomba nijuzwe sukari F1 ipi ni bora kati ya ile ya Africasia na East African Seeds
 
ubora sijaweza kutofautisha ila mwaka jana nitumia east African seeds il a mwaka nataka nijaribu kutoka balton Tanzania
 
Kuna yeyote anayelima kibaha mana nmepata shamba huko msaada plz
 
SAALAMU
HAYA MATIKITI YANAOITWA YA KISASA (F1) HYBRID, HAYA YANAKUWA YAMETENGEZWA YAKIWA NA SIFA ZA ZIADA KULIKO HAYA YA KAWAIDA (lOCAL/OPV). HAYA YA KISASA YAPO AMBAYO YAMEKINGWA KUWEZA KUTOSHAMBULIWA NA MAGONJWA MBAIMBALI KAMA VILE MAGONJWA YA UMBWILI PODA (POWDERY MILDEW), AU KUJIKUNJA KWA MAJANI (LEAF CURLING ). LAKINI PIA YA KISASA YAMETENGENZWA KUWAHI KUKOMAA, MENGI SANA KAMA SUKARI F1 AU JULINA F1 et al... YANAANZA KUKOMAA BADADA YA SIKU 70-75. FAIDA NYINGINE YA KUPANDA HAYA YA KISASA NI KUWA KATIKA SHIMO UNAWEKA MBEGU 1 MAXIMUM SANA NI MBILI, NA ASILIMIA ZA UOTAJI WAKE NI MKUBWA SANA
95%+
KWA MFANO HAYA YA KISASA UNAHITAJI KWA EKA 1 UNAHITAJI MBEGU GRAM 200-250 COZ UNAPANDA MOJA MOJA, LAKINI HAYA YA KIENYEJI (LOCAL/OPV) UNAPANDA MBEGU HADI 3 KWA SHIMO MOJA, HIVYO KWA EKA 1 UNAHITAJI HADI MBEGU GRAM 500-700 NA SI ZOTE ZITAOTA. PIA HAYA YA KISASA NDANI YANASUKARI SANA, NA YANAVUTIA KIUMBO RANGI NA HATA UZITO MENGI UNAKUTA YANAKILO 5 HADI 12. FAIDA NYINGINE YA MUHIMU ZAIDI NI KUWA HIZI ZA KISASA ZINAKUPA MAVUNO MENGI KWA KAMBA MOJA, HIVYO UKILIMA VIZURI NA UKAWEZA KUPAMBANA NA HIZO CHANGAMOTO ZA LISHE, NA WADUDU, NA MADALALI BASI UHAKIKA WA KURUDISHA GHARAMA ZAKO NI MKUBWA SANA.


Hivi haya ya kisasa yana nini zaidi? Maana naona kama wakulima wanaachana na matikiti ya asili
 
SALAAMU
UNAPOZUNGUMZIA UBORA, KUNA MAMBO MENGI HAPO MKUU, JE UNAAMISHA UBORA KWA MAANA YA UTAMU (SUKARI/MAJI), JE UNAANGILIA UBORA KATIKA KUTOSHAMBULIWA NA WADUDU, JE UNAANGALIA UBORA KATIKA KUTOSHAMBULIWA NA MAGONJWA ETC, AU JE UNAANGALIA UBORA KATIKA SHAPE/UMBO KUVUTIA ETC. HAYO MAMBO MARA NYINGI YANAKUWA YAMEANDIKWA KATIKA VILE VIKARATASI/VIFUNGASHO HADI GERMINATION PERCENT WAWEZA IONA, AU ZAIDI KABLA YA KUNUNUA UNAWEZA ULIZA HII MBEGU INAUTOFAUTI GANI NA HII..UTAAMBIWA TU. SUKARI F1 YA EAST WEST INASIFIKA KWA KUWA INAUWEZO WA KUKOMAA HARAKA, INASUKARI SANA, NA INAKUWA KUBWA MNO MAXIMUM NI KILO 12, LAKINI PIA KUNA TAARIFA ZINAONYESHA ZIKO IMPROVED DHIDI YA MAGONJWA MENGI YA FANGASI (KUTU YA MAJANI, NA UBWIRI UNGA/PODA).

KABLA YA KUNUNUA ULIZA KWANZA UPATE ELIMU TOKA KWA MUUZAJI, KAMA NI MWAMINIFU ATAKWAMBIA UTOFAUTI WA MBEGU ALIZONAZO.

Wadau naomba nijuzwe sukari F1 ipi ni bora kati ya ile ya Africasia na East African Seeds
 
Kwanza hongera kwa kuamua kuingia shambani, mimi nalima matikiti na nimeshajilipua kulima ktk kipindi hiki cha masika, kubwa zaidi tafuta mbegu bora kwenye maduka ya kilimo mfano pitia kariakoo, mimi nalima Hybrid F1 sugar queen, na kiwango cha ekari moja utatakiwa kuwa na gram 300 na kila shimo panda mbegu 2 japo wapo wanaopanda mpaka 3, na hapa utatakiwa kuwa na mshimo kama 2000.
Andaa shamba vizuri japo wiki tatu kabla ya kupanda na hakikisha eneo lako lina maji ya kutosha kwani tikiti linahitaji maji mengi katika uhai wake, Panda kwa mbolea, ni vema zaidi kama utapata samadi na kama utatumia ya viwandani zipo kama vile winner(hapa kuna kiambato chake, utamuuliza muuzaji), kwa kukuzia utatumia CAN, andaa dawa za wadudu wanaokata majani pindi matikiti yanapoanza kuota tu na pindi unapoona dalili za matikiti kushambuliwa majani (karate itakufaa).
Unahitaji uangalizi wa karibu sana kuanzia mwanzo mpaka mwisho na hakikisha unakuwa na dawa za kutosha kwa ajili ya kuzuia wadudu waharibifu, ukungu hasa kipindi hiki na magonjwa yanayoshambulia majani, maua na matunda.
Gharama kubwa utakayoingia kwenye kilimo hiki ni kwenye mbegu( ekari moja ni gram 300= 250,000 kwa Dar), dawa( hapa inategemea na hali ya eneo na jinsi magonjwa na wadudu wanavyoshambulia), nguvu zako mwenyewe kwenye kumwagilia( hapa kama unatumia ndoo, ila kama unatumia mashine ya kuvutia maji basi utahitaji wastani wa lita 5 kwa ekari moja kila unapomwagilia) na kutunza shamba, kama unatumia kijana basi hapo ni makubaliano yenu, bomba la kupigia dawa ni muhimu sana.
Mavuno ni kuanzia siku 65 mpaka 75 inategemea na eneo lenyewe na aina ya mbegu, na kiasi cha mavuno kwa ekari moja ni kiasi cha matikiti kama 7000( kila mche mmoja utoe matikiti 2 tu yenye afya nzuri) na soko likiwa nuri basi utauza kwa wastani wa Tsh 1500 au zaidi shambani, na ukiMU kwenda mwenyewe sokoni mfano Buguruni unaweza kuuza bei nzuri kama ni kipindi mmea huo haupatikani.
Ushauri: usiende shambani na matarajio makubwa zaidi ya kupata hela nyingi ukasahau changamoto zake( mavuno kidogo, hasara na muda), shambani kunahitaji uangalizi wa karibu sana na usijaribu kulima kwa simu hasa kama una watu wasio waaminifu watakuua kwa ugonjwa wa moyo. Pia hizo faida zinazopatiakana ni pale tu utakapo fata ushauri wa kitaalamu na ukaamua kwa dhati kufanya kilimo. Nimejaribu kueleza kile ninachofahamu japo sio kwa utaalamu zaid, mengine wajuzi watakuja kujazia.
Karibu sana shambani
Umeeleza vyema sana mkuu. Ubarikiwe.
 
KAKA HII HABARI UMETOA HAIKO SAHIHI husasan unaposema unapanda kwa umbali wa 2 by 3 metres halafu unapata mashimo 1000. hicho kitu hakipo since one acre ina 70 by 70 metres na surface area ya 4900 meter squared. kama unapanda kwa 2 by 3m, utakua na mashimo 575 tu katika acre moja. this means kama unapataga matunda matano kwenye shimo moja basi utapata 575*5*5= 14375 manke utakua na mashimo 575. iyo inamaanisha utapata matunda 14375 kwa acre tano, kulingana na bei yako ya kuuzia shamba sh mia tano ambayo utakua ulipunjwa sana, manake tikiti moja bei shamba ni buku dsm, hata mikoani. revenue yako itakua 14375*500= 7187500 tsh only, or lets say 7200000. kitu kingine u realy have to explain inakuaje unatumia million 25 kulima na kumwagilia kwa mwaka mmoja. wakati sisi tunatumia just 2. mil kulima acre tano izo izo kwa msimu, kwa mwaka roughly 10 million. hebu tuelezee kuhusu garama zako, manake naanza kuhisi untaka kukatisha watu tamaa ya kulima hayo matunda

WANAOJUA, 1 by 1m space kutoka kwenye mmea mmoja mpaka mwingine. that means kunakua na mashimo 4900 kwa acre. kama target ni kupata matunda matatu makubwa kila shimo then tunfanya simple calculations 4900*3= 14700 fruits per one acre. fanya iyo times the market price ya shamba ambayo ni buku revenues inakua 14700000 ( forteen million tsh). iyo forteen milion toa garama ya 250,000 tsh ya kuhudumia iyo acre moja kuanzia unapopanda, palizi, DAWA, ulinzi, mbegu, trekta, harrow, kila kitu mpaka kuvuna.

Post yako ina makosa katika vipimo. Acre moja ina surface area of 4046.86 meter squire. Kama unabisha fanya utafiti zaidi, unaweza hata ku google. eg acre to squire meters.
 
Naomba kuuliza, ni mbegu ipi nzuri zinazotoa tikitiki zenye ubora? Msaada
 
Ndiyo zipo zinakua na uwezo Wa kuhimili mikikimikiki ya masika.hizi nyingine zinaoza.mi mwenyewe ninampango Wa kulima tikiti la masika kwsbb linalipa.kuna jamaa ni mzoefu zaidi Wa mambo haya ndiye aliyeniwekea oda kiwandani.km utapenda nitakutumia no.yake
Nammimi naomba namba nkuu
 
Hii mada ingenoga kwa kuweka na picha ili iwe rahisi kutambua na kutofautisha hizo aina
 
Habar wana JF!

Nahtaji kuanza kufanya kilimo cha matikiti maji kule Mikese Morogoro mwezi huu wa sita!

Kipi cha kufanya ndugu zangu ili swala hili liende vzuri!
 
Kanunue mbegu inaitwa Juliana F1 inazalishwa na kibo seeds... Ukikosa Hiyo kanunue mbegu inaitwa sugar baby king inazalishwa na African seeds
 
Back
Top Bottom