zambezi_21
Member
- Jul 18, 2021
- 7
- 14
Ni kweli kwamba Dunia kwa Sasa ipo katika mapinduzi ya nne ya viwanda na sekta inayoongoza mapinduzi haya ni sekta ya teknologia na habari. Matajiri wakubwa wa Dunia kwa kiasi kikubwa ni Vijana na wazee ambao wamewekeza katika sekta hii kwa kiasi kikubwa,hapa nawazungumzia watu Kama Jeff Bezos,elon musk,mark zuckerberg,bill gates na wengine ambao ndio kwa sehemu kubwa wanamiliki utajiri wa Dunia.
Nchi nyingi za Africa Zina mchango mdogo Sana katika mapinduzi ya viwanda yanayotokea kwasasa tofauti na hapo wajasiria mali wengi waafrika imekua ni vigumu kwao kwa kupitia sekta ya teknologia na habari kutengeneza uchumi unao endana na Hawa matajiri wanao endesha uchumi wa Dunia kutokana na mifumo mibovu ya kiuchumi katika nchi za Africa lakini pia ugumu wa bidhaa zetu kuheshimika na kukubalika katika soko la Dunia.
Kwa namna moja au nyingine waafrika na watanzania hususani, inabidi kabla ya kushiriki kikamilifu katika sekta hii kiongozi ya teknologia na uchumi,tuanzie katika sekta ya kilimo Kama nchi tajiri zilipo anzia, kwa wakati huo huo tuchanganye kilimo na technologia na habari hapa ndipo tutajenga uchumi wa kweli.
Kilimo kinachoendelea hapa tanzania kwa asilimia kubwa sicho ambacho kinauwezo wa kuinua uchumi wetu na kujilinganisha na walioendelea. Tanzania tuna aridhi ambayo inafaa kilimo hekta million 13.5, zipo nchi ambazo ukubwa tuu wa nchi haufiki hecta million 13 lakini wanazalisha mazao ya kilimo Mara 2 zaidi yetu.
Uwekezaji mkubwa katika kilimo unaleta tija katika uchumi wa nchi kwani kilimo ni sekta ambayo inashabihiana mojakwamoja na ukuaji wa viwanda pamoja na mambo mengine. Katika nchi zilizoendela wakulima wanauwezo wa kuzalisha mazao pamoja na kuyaongezea thamani hapo hapo shambani mpaka kuwa bidhaa ambayo inaweza ikapelekwa moja kwa moja kwa mlaji.
Shambani la hekta 10000 linaweza kuzalisha chakula mpaka tani 110,000 Za nafaka kwa mwaka. Hili ndilo shamba la mkulima na mtanzania wakawaida anapashwa kudhamiria kuliendesha. Shamba hili pia kwa kutumia teknologia mbali mbali lina weza kuzalisha umeme wa mega watt 15 Kwa kutumia mtambo wa umeme ambao unatumia makuti ya mazao Kama mahindi,alizeti na mengine (biogas power plant au straw power plant). Kwa maana nyingine baada ya kulima mkulima atavuna kwa kutumia combine havester,ambapo kwa ukubwa huu wa hekta 10,000 combine havester aina ya (Claas Lexion 770 TT)Inaweza kuvuna shamba lote,mashine hii inavuna inapukuchua nakumwaga kwenye gari la nafaka. Baada ya hapo mkulima atatumia ( Claas Quadrant 3200 RC T) Kukusanya makuti yaliyoachwa chini. Makuti hayo baadhi yataenda kuingia kwenye mtambo wa kuzalisha umeme straw power plant au biogas power plant. Baada ya makuti haya kutumika kuzalisha umeme ule uji utakao bakia Kama taka za mwisho ni bidhaa adhimu Sana ambapo mkulima atatumia tena shambani Kama liquid fertilizer. Baadhi ya makuti yanataingizwa kwenye machine kuyakandamiza na kukausha maji halafu kutumika kutengenezea bidhaa mbali mbali Kama mbao (chip wood) au matofali (straw block)
Shambani pia mkulima ataweza kuweka viwanda mbali mbali kama kiwanda cha mafuta ya alizeti (vegetable oil distillation factory) Kiwanda cha gas (katika kutengeneza umeme wa biogas patazalishwa kwa wingi gesi ya methane ambayo utaweza kuzalisha umeme ama kuiandaa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani) pia kiwanda cha unga (wheat and corn flour milling factory)
Shamba hili litahitaji matrekta makubwa ambayo ndiyo yanaongoza kwa ufanisi duniani. Hapa nazungumzia trakta Kama Case IH Quadtrac 620 walau moja,Case IH Quadtrac STX 375 pia moja,Case IH Maxxum 130 CVR moja na mengine pia machine za kuandalia na kupandia shamba Kama Gregoire Besson Semi Mounted Plough, Farmet Kompaktomat K1570, Bourgault 3420-100 Paralink Hoe Drill, Horsch Maestro 36 row na nyingine hizi zote ni za kuandaa shamba pamoja na kupanda
Pia shamba la ukubwa huu linahitaji Agricultural Drone Korec eeBe SQ,hii ni drone ya teknologia ya Hali ya juu Sana,kazi yake kwa kutumia kamera zake maalumu inaonesha uwiano wa maji baada ya kumwagilia,rutuba katika udongo,adhari za magonjwa na wadudu,kiwango cha mbolea kinachohitajika sehemu maalumu. Kwa kutumia GPS system technology taarifa hizi itazituma katika mashine zingine zote ili kujua sehemu fulani kipindi kingine panahitaji maji zaidi au mbolea zaidi au dawa zaidi. Na mwisho wa siku kwa kutumia data kutoka kila mashine Kama vile combine havester ambayo pia wakati inavuna inapima pia na wingi wa mavuno pamoja na ukubwa wa puche iliyovunwa kwenye GPS location flani kwahiyo unajua sehemu fulani ulipata mavuno machache au mengi kwa sababu gani. Hapa pia panahitajika Agricultural Drone DJI MG 1 walau ziwe kumi, hizi hutumika kwa ajili ya kupulizia dawa na kumwagilia liquid fertilizer, zinaruka umbali wa mita 3 kutoka kwenye mmea na moja inamwagilia upana wa mita 5, pilot mmoja anaweza kuziendesha 5 kwa pamoja. Hizi zinawasiliana na mashine zingine zote kujua wapi pakuwekwa kiasi gani cha mbolea au dawa japo pia mbolea hii unaweza pia kiimwagilia kwa kutumia irrigation system inayofungwa mwanzoni.
Shamba hili linahitaji miundo mbinu madhubuti shambani kwa maana ya barabara, silos za kuhifadhia nafaka ( grain silo plant) walau 3 za tani 5000, na 3 za tani 3000. Magari ya usafirishaji,magari ya moto (fire truck ya kuzima moto)mizani ya kupia nafaka,kituo cha kujazia mafuta,Majengo ya viwanda,Majengo kwa ajili ya kuhifadhia makuti( jengo la chuma lisilo na umeme ili kuepuka hatari ya moto) na jengo la karakana kwa ajili ya kutengeneza mbao,matofali na bidhaa zitokanazo na mbao. Pia Majengo ya makazi kwa ajili ya wafanya kazi,ofisi pia kanteen ya chakula.
Mradi wa shamba hili unahitaji walau mtaji wa billion 11 za kuanzia (initial investment)na kwa kipindi cha miaka walau mitano na kuendelea faida yake kubwa inapaswa irudi shambani ambapo kwa ukamilifu wake billion 25 zitatosha kuwa mtaji wa kuendesha shamba hili kwa uwezo wake kamilifu. Mtaji huu kwa kiasi kikubwa utategemea msamaha wa kodi katika kuingiza machine zote za kilimo nchini. Shamba hili linauwezo wa kuzalisha tani 110,000 za chakula kwa mwaka kwa ajili ya masoko ya ndani Kama azam,azania na milling factory zingine pia baadhi ya mazao kwa ajili ya masoko ya nje,hapa patalimwa mahindi,ngano,shairi,maharage,alizeti pamoja na viazi. Shamba hili linauwezo wakuzalisha tani 350,000 mpaka 400,000 za makuti ambazo zingiweza kupotea aridhi lakini hapa zitatengeneza umeme mpaka mega watt 15 au 45,000,000 Nm³ Methane gas. Kwa bajeti hiyo niliyoiweka ya kuanzia (initial investment) ya billion 11,hapa unaweza kuweka mtambo wa umeme wakuzalisha mega watt 1.5 kwa maana nyingine unaweza ukahudumia umeme kwa mkoa mzima kupitia shamba hili
Pamoja na faida zingine katika shamba hili, kwa kutumia mashine na matrekta makubwa yaliyopo shambani hapa itawasaidia wakulima wote wa pembembezoni mwa shamba wenye mashamba yenye ukubwa wa ekari 1000 na kuendelea kutumia mashine hizi wakati hazina kazi shambani,ambapo kwa muda mrefu wa kuendelea kufanya hivo wakalima Hawa watajijengea uwezo wa kuweza kuagiza mashine zao wenyewe kutoka nje za ukubwa huo. Pia umeme utakao zalishwa hapa unaweza kuelekezwa katika vijiji vya Jirani na mwingine kuwekwa katika grid ya taifa kwa makubaliano na tanesco. Pia kwa kutumia machine Kama seed dressing machine na zingine patazalishwa mbegu bora kabisa kwa ajili ya wakulima wa pembeni na kwa ajili ya biashara,pia mbolea inayotoka katika mtambo wa umeme na gesi unaweza kulitosha shamba Hili pamoja na wakulima wa pembembezoni na kwa ajili ya biashara pia.
Kiuhalisia unahitaji muda mrefu wa ujuzi katika kilimo kuweza kuendesha shamba la ukubwa huu. Hakuna linaloshindikana,kwa kupitia mashamba madogo ya hekari chini ya elfu moja watanzania wanaweza kudhamiria kujijenga kiujuzi na pia kwa kuwatembelea wenzetu na kutumia wataalamu wa ndani ikawezekana watanzania wakawaida kabisa kumiliki na kuendesha mashamba ya namna hii. Mtaji wa pesa nyingi namna hii unapatikana huko huko shambani. Wapo watanzania wengi waliowekeza katika mazao ya muda mrefu hapa nazungumzia machungwa,maembe,maparachichi mkonge na mengine tena wakiwa wameanza kwa kipato kidogo lakini leo hii wanatengeneza mabilioni ya shilingi. Bila kubadilisha mitazamo yetu katika kuiendea sekta hii ya kilimo na kuamua kudhamiria kufanya kilimo chenje kujenga uchumi wetu mkubwa wa taifa zima,wazungu wataendelea kutucheka na kutushangaa kwamba kwanini tumejifunga akili zetu na kushindwa kudhubutu kutumia aridhi yetu kujiendeleza na kuweza kushindana na mataifa makubwa kiuchumi. Binafsi nathubutu kusema kwamba aridhi tuliyonayo kwa ajili ya kilimo ni mali kubwa tuliyopewa na Mwenyezi Mungu kuliko madini,mafuta au gesi ambazo kila siku tunakimbizana nazo.
Nchi nyingi za Africa Zina mchango mdogo Sana katika mapinduzi ya viwanda yanayotokea kwasasa tofauti na hapo wajasiria mali wengi waafrika imekua ni vigumu kwao kwa kupitia sekta ya teknologia na habari kutengeneza uchumi unao endana na Hawa matajiri wanao endesha uchumi wa Dunia kutokana na mifumo mibovu ya kiuchumi katika nchi za Africa lakini pia ugumu wa bidhaa zetu kuheshimika na kukubalika katika soko la Dunia.
Kwa namna moja au nyingine waafrika na watanzania hususani, inabidi kabla ya kushiriki kikamilifu katika sekta hii kiongozi ya teknologia na uchumi,tuanzie katika sekta ya kilimo Kama nchi tajiri zilipo anzia, kwa wakati huo huo tuchanganye kilimo na technologia na habari hapa ndipo tutajenga uchumi wa kweli.
Kilimo kinachoendelea hapa tanzania kwa asilimia kubwa sicho ambacho kinauwezo wa kuinua uchumi wetu na kujilinganisha na walioendelea. Tanzania tuna aridhi ambayo inafaa kilimo hekta million 13.5, zipo nchi ambazo ukubwa tuu wa nchi haufiki hecta million 13 lakini wanazalisha mazao ya kilimo Mara 2 zaidi yetu.
Uwekezaji mkubwa katika kilimo unaleta tija katika uchumi wa nchi kwani kilimo ni sekta ambayo inashabihiana mojakwamoja na ukuaji wa viwanda pamoja na mambo mengine. Katika nchi zilizoendela wakulima wanauwezo wa kuzalisha mazao pamoja na kuyaongezea thamani hapo hapo shambani mpaka kuwa bidhaa ambayo inaweza ikapelekwa moja kwa moja kwa mlaji.
Shambani la hekta 10000 linaweza kuzalisha chakula mpaka tani 110,000 Za nafaka kwa mwaka. Hili ndilo shamba la mkulima na mtanzania wakawaida anapashwa kudhamiria kuliendesha. Shamba hili pia kwa kutumia teknologia mbali mbali lina weza kuzalisha umeme wa mega watt 15 Kwa kutumia mtambo wa umeme ambao unatumia makuti ya mazao Kama mahindi,alizeti na mengine (biogas power plant au straw power plant). Kwa maana nyingine baada ya kulima mkulima atavuna kwa kutumia combine havester,ambapo kwa ukubwa huu wa hekta 10,000 combine havester aina ya (Claas Lexion 770 TT)Inaweza kuvuna shamba lote,mashine hii inavuna inapukuchua nakumwaga kwenye gari la nafaka. Baada ya hapo mkulima atatumia ( Claas Quadrant 3200 RC T) Kukusanya makuti yaliyoachwa chini. Makuti hayo baadhi yataenda kuingia kwenye mtambo wa kuzalisha umeme straw power plant au biogas power plant. Baada ya makuti haya kutumika kuzalisha umeme ule uji utakao bakia Kama taka za mwisho ni bidhaa adhimu Sana ambapo mkulima atatumia tena shambani Kama liquid fertilizer. Baadhi ya makuti yanataingizwa kwenye machine kuyakandamiza na kukausha maji halafu kutumika kutengenezea bidhaa mbali mbali Kama mbao (chip wood) au matofali (straw block)
Shambani pia mkulima ataweza kuweka viwanda mbali mbali kama kiwanda cha mafuta ya alizeti (vegetable oil distillation factory) Kiwanda cha gas (katika kutengeneza umeme wa biogas patazalishwa kwa wingi gesi ya methane ambayo utaweza kuzalisha umeme ama kuiandaa kwa ajili ya matumizi ya nyumbani) pia kiwanda cha unga (wheat and corn flour milling factory)
Shamba hili litahitaji matrekta makubwa ambayo ndiyo yanaongoza kwa ufanisi duniani. Hapa nazungumzia trakta Kama Case IH Quadtrac 620 walau moja,Case IH Quadtrac STX 375 pia moja,Case IH Maxxum 130 CVR moja na mengine pia machine za kuandalia na kupandia shamba Kama Gregoire Besson Semi Mounted Plough, Farmet Kompaktomat K1570, Bourgault 3420-100 Paralink Hoe Drill, Horsch Maestro 36 row na nyingine hizi zote ni za kuandaa shamba pamoja na kupanda
Pia shamba la ukubwa huu linahitaji Agricultural Drone Korec eeBe SQ,hii ni drone ya teknologia ya Hali ya juu Sana,kazi yake kwa kutumia kamera zake maalumu inaonesha uwiano wa maji baada ya kumwagilia,rutuba katika udongo,adhari za magonjwa na wadudu,kiwango cha mbolea kinachohitajika sehemu maalumu. Kwa kutumia GPS system technology taarifa hizi itazituma katika mashine zingine zote ili kujua sehemu fulani kipindi kingine panahitaji maji zaidi au mbolea zaidi au dawa zaidi. Na mwisho wa siku kwa kutumia data kutoka kila mashine Kama vile combine havester ambayo pia wakati inavuna inapima pia na wingi wa mavuno pamoja na ukubwa wa puche iliyovunwa kwenye GPS location flani kwahiyo unajua sehemu fulani ulipata mavuno machache au mengi kwa sababu gani. Hapa pia panahitajika Agricultural Drone DJI MG 1 walau ziwe kumi, hizi hutumika kwa ajili ya kupulizia dawa na kumwagilia liquid fertilizer, zinaruka umbali wa mita 3 kutoka kwenye mmea na moja inamwagilia upana wa mita 5, pilot mmoja anaweza kuziendesha 5 kwa pamoja. Hizi zinawasiliana na mashine zingine zote kujua wapi pakuwekwa kiasi gani cha mbolea au dawa japo pia mbolea hii unaweza pia kiimwagilia kwa kutumia irrigation system inayofungwa mwanzoni.
Shamba hili linahitaji miundo mbinu madhubuti shambani kwa maana ya barabara, silos za kuhifadhia nafaka ( grain silo plant) walau 3 za tani 5000, na 3 za tani 3000. Magari ya usafirishaji,magari ya moto (fire truck ya kuzima moto)mizani ya kupia nafaka,kituo cha kujazia mafuta,Majengo ya viwanda,Majengo kwa ajili ya kuhifadhia makuti( jengo la chuma lisilo na umeme ili kuepuka hatari ya moto) na jengo la karakana kwa ajili ya kutengeneza mbao,matofali na bidhaa zitokanazo na mbao. Pia Majengo ya makazi kwa ajili ya wafanya kazi,ofisi pia kanteen ya chakula.
Mradi wa shamba hili unahitaji walau mtaji wa billion 11 za kuanzia (initial investment)na kwa kipindi cha miaka walau mitano na kuendelea faida yake kubwa inapaswa irudi shambani ambapo kwa ukamilifu wake billion 25 zitatosha kuwa mtaji wa kuendesha shamba hili kwa uwezo wake kamilifu. Mtaji huu kwa kiasi kikubwa utategemea msamaha wa kodi katika kuingiza machine zote za kilimo nchini. Shamba hili linauwezo wa kuzalisha tani 110,000 za chakula kwa mwaka kwa ajili ya masoko ya ndani Kama azam,azania na milling factory zingine pia baadhi ya mazao kwa ajili ya masoko ya nje,hapa patalimwa mahindi,ngano,shairi,maharage,alizeti pamoja na viazi. Shamba hili linauwezo wakuzalisha tani 350,000 mpaka 400,000 za makuti ambazo zingiweza kupotea aridhi lakini hapa zitatengeneza umeme mpaka mega watt 15 au 45,000,000 Nm³ Methane gas. Kwa bajeti hiyo niliyoiweka ya kuanzia (initial investment) ya billion 11,hapa unaweza kuweka mtambo wa umeme wakuzalisha mega watt 1.5 kwa maana nyingine unaweza ukahudumia umeme kwa mkoa mzima kupitia shamba hili
Pamoja na faida zingine katika shamba hili, kwa kutumia mashine na matrekta makubwa yaliyopo shambani hapa itawasaidia wakulima wote wa pembembezoni mwa shamba wenye mashamba yenye ukubwa wa ekari 1000 na kuendelea kutumia mashine hizi wakati hazina kazi shambani,ambapo kwa muda mrefu wa kuendelea kufanya hivo wakalima Hawa watajijengea uwezo wa kuweza kuagiza mashine zao wenyewe kutoka nje za ukubwa huo. Pia umeme utakao zalishwa hapa unaweza kuelekezwa katika vijiji vya Jirani na mwingine kuwekwa katika grid ya taifa kwa makubaliano na tanesco. Pia kwa kutumia machine Kama seed dressing machine na zingine patazalishwa mbegu bora kabisa kwa ajili ya wakulima wa pembeni na kwa ajili ya biashara,pia mbolea inayotoka katika mtambo wa umeme na gesi unaweza kulitosha shamba Hili pamoja na wakulima wa pembembezoni na kwa ajili ya biashara pia.
Kiuhalisia unahitaji muda mrefu wa ujuzi katika kilimo kuweza kuendesha shamba la ukubwa huu. Hakuna linaloshindikana,kwa kupitia mashamba madogo ya hekari chini ya elfu moja watanzania wanaweza kudhamiria kujijenga kiujuzi na pia kwa kuwatembelea wenzetu na kutumia wataalamu wa ndani ikawezekana watanzania wakawaida kabisa kumiliki na kuendesha mashamba ya namna hii. Mtaji wa pesa nyingi namna hii unapatikana huko huko shambani. Wapo watanzania wengi waliowekeza katika mazao ya muda mrefu hapa nazungumzia machungwa,maembe,maparachichi mkonge na mengine tena wakiwa wameanza kwa kipato kidogo lakini leo hii wanatengeneza mabilioni ya shilingi. Bila kubadilisha mitazamo yetu katika kuiendea sekta hii ya kilimo na kuamua kudhamiria kufanya kilimo chenje kujenga uchumi wetu mkubwa wa taifa zima,wazungu wataendelea kutucheka na kutushangaa kwamba kwanini tumejifunga akili zetu na kushindwa kudhubutu kutumia aridhi yetu kujiendeleza na kuweza kushindana na mataifa makubwa kiuchumi. Binafsi nathubutu kusema kwamba aridhi tuliyonayo kwa ajili ya kilimo ni mali kubwa tuliyopewa na Mwenyezi Mungu kuliko madini,mafuta au gesi ambazo kila siku tunakimbizana nazo.
Upvote
9