Kilimo cha Viazi Mviringo (Viazi Ulaya) na Masoko Yake

Makambuya

Member
Joined
Dec 6, 2011
Posts
45
Reaction score
3


Kwa mwana JF yeyote mwenye ujuzi na uzoefu wa kilimo cha viazi naomba anipe detail kuhusu kilimo hicho.

Yaani kwa mfano, nikitaka kulima hekari moja natakiwa kuwa mtaji wa kiasi gani? Na vipi namna ya kupata shamba? Msimu unaanza mwezi wa ngapi? Jinsi ya kulima na tahadhari za kuchukua wakati wa kilimo hiki. Pia, ningejua masoko yake yapoje inaweza kusaidia kwangu na kwa wengi.

Please naomba msaada.

BAADHI YA WADAU WENGINE WANAOHITAJI KUJIFUNZA KUHUSU KILIMO HIKI
Naombeni kujua garama za kilimo cha viazi ulaya ukilima hekari moja. Msaada juu ya:
  • Mbegu
  • Madawa
  • Kulima
Na mengine nisiyoyajua asanteni sana, location ni Lushoto.


MAJIBU YA WADAU KUHUSU KILIMO HIKI



KUHUSU KILIMO BORA CHA VIAZI MVIRINGO
Viazi mviringo au kwa jina jingine viazi ulaya ni jina ambalo hutumika kutofautisha zao hili na zao la viazi vitamu. Zao hili ni muhimu kati ya mazao ya mizizi katika maeneo ya miinuko ya Afrika mashariki.

Katika maeneo ya miinuko zaidi, zao hili huwa na mavuno makubwa zaidi kwa zao la mahindi na hukua kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Viazi mviringo hutumika sana kama zao kuu la chakula hapa nchini na pia husafirishwa katika maeneo ya mbali kama vile Kampala, Mombasa na Dar es salaam.

Hapa Tanzania viazi mviringo kuzalizwa katika maeneo yenye miinuko ya kaskazini kama vile Moshi, Arusha, Lushoto na meneo ya kusini yenye miinuko kama vile Njombe mkoani Iringa na wilaya za mkoa wa Mbeya. Pia maeneo ya Morogoro yenye miinuko hususani Tarafa ya Mgeta yameonekana kuweza kuzalisha zao hili kwa wingi.

II. MMEA WA KIAZI ULIVYO

Kiazi ni mzizi wa mmea unaovimba ukiwa chini ya ardhi na kuwa na vijicho vingi, ambavyo baada ya miezi 2 – 3 vijicho hivi huchipua na kuota shina, kijicho kimoja huweza kutoa zaidi ya shina 1 ambapo hutoa vitawi vingine.

Pingili zilizopo kwenye shina hutoa mizizi inayomea chni ya ardhi na miisho yake huvimba na kuwa kiazi. Viazi nyenye ngozi nyeupe huwa na maua meupe na ile yenye rangi hutoa maua ya rangi aidha pinki, bluu au zambarau.

Katika mzunguko wa ukuaji kiazi huendelea kukua hata baada ya maua kutoka; ili mradi kuwe na na unyevunyevu wa kutosha kwenye udongo na yasiwepo magonjwa.

II. HALI YA HEWA

MVUA :-


Viazi huhitaji mvua za kiasi cha sentimita 25 kwa wiki ambazo hutakiwa kuendela kwa muda wa miezi 3 .5 hii huweza kukuza viazi na kupata mavuno mazuri.

JOTO
Viazi hukua vizuri zaidi kwenye baridi kwa mwinuko wa mita 1,800 kulikoni kwenye joto. Maeneo machache ya mwinuko wa mita 1,500 huweza kukuza viazi, japo pia hukua kwenye mwinuko wa mita 2,900.

UDONGO
Viazi hutoa mavuno mazuri kwenye udongo usiokuwa mzito na unaopitisha maji kwa urahisi. Udongo wenye viini lishe vya kutosha au kuongeza samadi na mbolea za viwandani.

IV. AINA ZA VIAZI
Aina zote za viazi zimeingizwa Afrika Mashariki kutoka Ulaya ambako huzalishwa kwa wingi

i. DUTCH ROBIJN – KUTOKA HOLLAND
– Ndani ni njano
– Inavumilia kidogo ugonjwa wa ukungu
– Hushambuliwa sana na Mnyauko Bakteria
– Hupendwa na walaji wengi

ii. ROSLIN – KUTOKA SCOTLLAND
– Ngozi yake ni nyeupe
– Ndani ni nyeupe
– Huvumulia ugonjwa wa ukungu

iii. KERR’S PINK – NGOZI YAKE NI NYEUPE AU NYEKUNDU
– Ndani ni nyeupe
– Hushambuliwa sana na ukungu na Mnyauko Bakteria

iv. ATZIMBA – KUTOKA MEXICO
– Huvumilia ugonjwa wa ukungu

V. MBEGU ZAKUZALISHA VIAZI
Viazi vyenye umbile dogo hutumika kama mbegu, hutakiwa kuwa na upana wa sentimita 3 – 6. Kiasi cha robo tatu za tani huhitajika kuotesha ekari 1 sawa na tani 1.85 kwa hekta 1.

Mbegu hazitakiwi kuhifadhiwa kwenye giza nene kwani zitaanza kutoa vichipukizi virefu vyeupe.

VI. KUANDAA SHAMBA
Shamba linatakiwa kuandaliwa vituta vidogo vidogo kwa nafasi ya sentimita 75 kutoka tuta hadi tuta, hiihusaidia kuhifadhi udongo na maji na hutoa nafasi nzuri wakati wa upanukaji wa viazi.

Inashauriwa pia kama matuta hayajatumika basi ni muhimu kujaza udongo kwenye shina kwani pingili za chini kwenye shina ni lazima zifunikwe na udongo ili zitoe viazi kwa wingi na hivyo mavuno huongezeka.

VII. KUOTESHA VIAZI
Viazi hutakiwa kuoteshwa mara karibu kabisa na mvua zinapotaka kuanza kuchelewa kuotesha kutapunguza kipindi cha ukuaji wa ile mizizi ili iwe viazi na hivyo kukabiliwa na kipindi cha ukavu.

Uoteshaji hufanyika kwa mikono na mbegu ziwekwe chini udongo kwa kina cha sentimita 10. Kama mbegu zitaoteshwa bila matuta basi zioteshwe kwa kina cha sentimita 15 na kufunikwa na udongo mchache na wakati wa palizi udongo utaongezwa ili kuongeza utoaji wa viazi kwa wingi. Nafasi ya kuotesha ni sentimita 75 toka mstari hadi mstari na sentimita 23 – 30kwa mche hadi mche.

VIII. MBOLEA
Viazi hustawi vizuri zidi kwenye udongo ulioongezwa samadi na ni muhimu chimbiwe katika kina kirefu. Mbolea za viwandani zinazotakiwa ni zile zenye Nitrogeni kwa kiasi cha kilo 22 – 45 kwa ekari; zenye Chokaa P2O5 kwakilo 45 – 65 kwa ekari.

Ni vyema kuongeza mbolea na samadi wakati kuna mategemeo mazuri ya mavuno kwa kuzingatia kuwa mbegu zilizooteshwa hazina magonjwa ya aina yoyote.

IX. PALIZI
Zao la viazi likioteshwa kwa nafasi zilizoshauriwa basi huweza kufunika ardhi yote na hivyo kugandamiza magugu, hii husaidia kwa kipindi cha wiki 6 za mwanzo. Katika mpando wa matuta, basi huwa ni kuondoa magugu na kujaza udongo kwenye mashina.

X. KUVUNA
Uvunaji wa viazi hufanyika kwa kutumia jembe la mkono, viazi vikishang’olewa kutoka chini ya udongo visiachwe kwa muda mrefu kwani vitabadilika rangi na kuwa kijani.

Ili kuifanya ngozi ya viazi kuwa ngumu na isiharibike kirahisi basi mashina yote yanyofolewe wiki 2 – 3 kabla ya kuvuta viazi juu ya udongo. Baada ya viazi kuvunwa haviwezi kuhifadhiwa kwa muda mrefu kwani huanza kuchipua.

Viazi huweza kuhifadhiwa kwenye ardhi, lakini si zaidi ya wiki 6 kwani vitakabiliwa na magonjwa na kushambuliwa na minyoo fundo.

XI. MAVUNO
Mavuno huwa mengi kama utunzaji wa kitaalamu umezingatiwa ikiwa ni pamoja na kudhibiti magonjwa, kutumia aina zinazostahimili magonjwa. Kiasi cha tani 6 – 8 kwa ekari huvunwa,sawa na tani 15 – 20 kwa hekta.

KUHIFADHI :-
Uhifadhi wa zao hili ni mgumu, hivyo inashauriwa kuwa sehemu iliyotengwa kwa biashara iuzwe mapema, sehemu ya kutumia nyumbani ihifadhiwe katika banda au ghala safi lenye sakafu, lisilo na unyevu, mwanga wala joto- liwe na hewa safi na ya kutosha.

Vinginevyo husababisha viazi kuota haraka. Viazi vilivyowekwa ghalani visilundikwe kwa kina kirefu, visambazwe ili visipate joto.

XII. WADUDU
Vidukari:-

Ni wadudu wadogo wanaoshambulia majani na mashina kwa:
– kufyonza utomvu na kusababisha kunyauka kwa mmea.
– Majani kujikunja kuelekea juu.
– Majani kuwa magumu
– Mimea kudumaa
– Pia hubeba vimelea aina ya virusi ambao huathiri mimea.
– Pia hueneza ugonjwa wa virus.

TIBA:- Wakati wa utunzaji wa mbegu za viazi ni muhimu kupiga dawa ya wadudu ili kuepuka kupuliza shambani kwani dawa nyingi itapotea.

NONDO WA VIAZI :-
Wadudu huathiri viazi vilivyooteshwa wakati ambao sio wa msimu wa viazi. Viwavi wanaoanguliwa huingia ndani ya viazi na kusababisha kuoza. Pia huingia ndani ya viazi wakati vikiwa stoo.

KUZUIA :-
– Otesha viazi katika kina kinachoshauriwa au zaidi ya sentimita 3 kwani kiwavi aingiae ndani ya hawezi kuchimba kina kirefu na inulia matuta wakati viazi vinakuwa, hii husaidia kuzuia nondo kutaga mayai.
– Viazi vyote vilivyochimbwa ni muhimu viwekwe kwenye mifuko na mapema kabla ya alasiri ili kuepuka nondo kutaga mayai.
– Vikihifadhiwa stoo majani ya aina ya LANTANA CAMARA yaweza kutumika.

TIBA :-
Wakati viazi vikiwa stoo, dawa ya unga ya Aldrin hutumika kwenye viazi vya mbegu.

Nyunyizia majani ya viazi wakati mmea ukiwa na mwezi 1 dawa aina ya Dipterex, Diazon, Thiodan, Permethrin, ACtellic au Sumithion.

KAMA NI VIAZI VYA KULA BASI TUMIA PYRETHRUM.

MINYOOFUNDOO :-
Hushambulia viazi vilivyoachwa kwa muda mrefu ardhini na kwenye ardhi iliyoathirika na mmomonyoko.

KUZUIA :-
– Usioteshe mbegu ambazo zimeshambuliwa na wadudu.
– Andaa shamba mapema ili masalia yote ya mazao yaweze kuoza ili kutoruhusu makazi ya minyoo fundo.

MBAWAKAVU :-
Ni wadudu wadogo ambao hutafuna majani na kuacha matundu matundu.

KUZUIA :
Tumia dawa aina ya Malathion, Thiodan

MUHIMU: Pamoja madhara ya wadudu pia hueneza magonjwa mbali mbali ya mimea, hivyo kutunza shamba kuwa safi hasa kupalilia; kuchimba na kutupa mbali maotea pamoja na masalia yote na kubadilisha viazi na vipando kama maharage, mahindi, hupunguza madhara.

Credits: farmersmarket.co.tz
 
Muone afisa ugani aliyepo karibu nawe atakusaidia.
 
I have forgotten much but still remember mbatata za urojo Forodhani. Viazi mviringo hadi Uyole, Mbeya. Wondering if there are GMO varieties suitable for coastal regions.
 
Habari wadau,

Mimi ni mwajiriwa lakini pia mwaka jana niliamua kujaribu kulima kujaribu bahati yangu.

Nililima viazi mviringo (Ulaya) heka tatu kwa majaribio huko mpakani mwa njombe na ludewa.sasa nimepigiwa simu (mi naishi Dar) kuwa viazi vimeshakomaa na viko tayari kuvunwa, lakini tatizo ni bei iko chini kupita matarajio yangu.

kwa kiroba cha debe sita za viazi ni elfu 30.sasa bei hiyo imenikatisha tamaa sana kwa sababu nilitegemea ingekuwa elfu 40 na zaidi,na mpaka sasa sijaenda huko kuvuna kwa sababu hiyo.

Naomba ushauri kama kuna mtu anajua kuhusu hii biashara ya viazi na hasa soko kwa hapa Dar na mambo mengine kwa sababu sijawahi fanya biashara hii kabla.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
 
Ni vema ukaenda shambani kuvuna chagua viazi vizuri visiwe vidogo sana wala makuuuubwa pakia zako kwenye gunia sijui kama mitaa hiyo wanaruhusu lumbesa,shona vizuri tafuta gari lete sokoni MABIBO pale aka mahakama ya ndizi tafuta dalali utauza bei nzuri sijajua juzi na jana leo bei yake ila J3 bei ya gunia ilikuwa kati ya 80000 to 110000.
 

Asante kwa ushauri mkuu.
 
Mkuu angalia, kama kiazi chako kimeshatoka, vuna peleka sokono fasta. Kuanzia february mwishoni kiazi toka Makete,Mby na pande za Kipengere kitafurika sokoni, hali hiyo itadumu mpaka may mwishoni, vinginevyo unaweza tunza ikawa mbegu.
 
Mkuu angalia, kama kiazi chako kimeshatoka, vuna peleka sokono fasta. Kuanzia february mwishoni kiazi toka Makete,Mby na pande za Kipengere kitafurika sokoni, hali hiyo itadumu mpaka May mwishoni, vinginevyo unaweza tunza ikawa mbegu.

Nimekupata kiongozi wacha nifanye fasta. Thanks
 

Kaka nimepita MABIBO SOKONI bei imeshuka sana ukilinganisha na bei uliyotaja hapo juu.bei ni shs 60000 mpaka 65000, labda kama utakuwa na Dalali unamfahamu pale sokoni itakuwa poa ukanipa namba yake.
 
kaka nimepita MABIBO SOKONI bei imeshuka sana ukilinganisha na bei uliyotaja hapo juu.bei ni shs 60000 mpaka 65000, labda kama utakuwa na Dalali unamfahamu pale sokoni itakuwa poa ukanipa namba yake.
Hahaha kaka hiyo ndo kawaida ya bei za masoko nadhani itakuwa soko limetapika (mzigo mwingi) coz week ile niliyokuwepo gari zilikuwa kama 15 hv so kulikuwa kweupe kabisa ndo mana ikawa juu, mengineyo nimeku-PM.
 
Kavune uuze hivyo hivyo urudishe pesa yako mimi nililima Makete vimekomaa bei zipo chini sana ni sh 20,000 kwa gunia ninaenda next week nivune halafu nipande ngano itanipa faida zaid. Ukisubir zaid utakuja kuuza elfu 18 gunia better save now!
 
kavune uuze hivyo hivyo urudishe pesa yako mimi nililima makete vimekomaa bei zipo chini sana ni sh 20,000 kwa gunia ninaenda next week nivune halafu nipande ngano itanipa faida zaid. Ukisubir zaid utakuja kuuza elfu 18 gunia better save now!

Makete upande upi mkuu, wa Ikuwo au kule Magoma/Bulongwa/Matamba?

Kuna mchezo unachezwa vizuri sana kule Uwanji, kuna jamaa wa Itaka Mby, huwa wananunua viazi vya Ikuwo Uwanji wanavifanya mbegu ktk kipindi hiki. Sijui hawa jamaa waligundua nini ktk viazi vya kutoka kanda ile kwa kipindi hiki. Bado nafanya utafiti. Walisema hata vya Njombe huwa wanavigeuza mbegu ya kiazi cha kutoa June.

Bado mkulima wa malimbichi anaishi kwa mashaka sana.
 
Habari,

Nina mpango wa kulima viazi mviringo msimu ujao wa mvua, ila sina uzoefu na wala sijawahi kulima naomba kwa yoyote mwenye kujua vya zaidi kuhusu kilimo cha viazi mviringo anijuze. Nataka kulima ekari moja, labda kwa ufupi nijue ntatumia mbegu kiasi gani? Napandaje? navuna baada ya miezi mingapi?

Asanteni kwa kunisaidia.
 
Vizuri sana bila kusahau siku hizi ukitaka kuwa na Mafanikio wekeza katika mahitaji ya kila siku kwa binaadam especialy Chakula.
 
Panda vile vya kwenye mifuko ndo vinatoka vingi kuliko vya shambani.

Vizuri ukaenda Mbeya ukatembelee wakulima wakupe semina hapa naona mabwanashamba huwa hawapiti.
 

Wapi shamba lilipo? Aina ya udongo, n.k
 
Ndugu yangu Elungata nisaidie vya kwenye Mifuko ni vipi?
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…