Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Habari,
Nina mpango wa kulima viazi mviringo msimu ujao wa mvua, ila sina uzoefu na wala sijawahi kulima naomba kwa yoyote mwenye kujua vya zaidi kuhusu kilimo cha viazi mviringo anijuze. Nataka kulima ekari moja, labda kwa ufupi nijue ntatumia mbegu kiasi gani? Napandaje? navuna baada ya miezi mingapi?
Asanteni kwa kunisaidia.
Salama mkuu, faida ipo katika hiki kilimo?Mkuu mimi niliwahi kulima viazi ulaya mwaka juzi Eneo lilikuwa ekari Mbili,Ktk Kilimo hiki inategemea sana Nature ya Udongo wa eneo husika,Mimi nililima Njombe,Kwa kawaida Mbegu huwa ni kati ya gunia 5-7, kwa eneo la ekari moja,Mbolea ya kupandia hutumika DAP au NPK, na kukuzia ni UREA au CAN au SA,Madawa yanayotumika kwenye Viazi yapo ya Aina mbili; Dawa za Ukungu na dawa za kuua wadudu waharibifu, Dawa za Ukungu ni km vile Ridomil, Glider, Linkonil, n.k.Na dawa za kuua wadudu waharibifu ni km vile Wilcron, Banofos, Mocron, nk.Kulima kunaanza mapema kabisa kabla ya mvua za mwanzo,na ni vema Mvua ya kwanza inaposhuka kiazi kiwe tayari kimepandwa shambani.
Tuelekeze hivo vya mifukopanda vile vya kwenye mifuko ndo vinatoka vingi kuliko vya shambani.
Vizuri ukaenda mbeya ukatembelee wakulima wakupe semina hapa naona mabwanashamba huwa hawapiti.
Nyanda za Juu Kusini MagharibiSomo zuri. Viazi ulimwa mikoa gani zaidi?
Mbeya, Njombe, Kilimanjaro, Arusha na Tanga kidogoSomo zuri. Viazi ulimwa mikoa gani zaidi?