Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

ah

Ahsante mbegu yenye kutoa mazao yanayokubarika sokoni la ndani na la nje
Haswa vinapendwa vitunguu vyekundu so meru super,neptune,jambar ziko poa ,hata red bombay ina vitunguu vyekundu sema tatizo ni vinatoa mabomba (boltingl sana tatizo ambalo kwenye improved na hybrid hakuna so kila mbegu inakua kitunguu
 
Hii topiki muhimu sana. Nataka kuja kuanza kulima vitunguu na mboga mboga kwa ujumla. Nawaza maswali mengi sana na ntawatafuta wa dau humu.
 
Mkuu mbegu nenda Sokoni Au kwa mkulima chugua vitunguu vilivyokauka vizuri na visiwe na makovu kisha viachanishe linaloshinda kimoja kimoja Yani kambegu kamoja kamoja ila usimenye maganda kama vile vya kupikia vitenganishe halafu viache na maganda yake kisha hapo vitakuwa Tayari kwa kupanda

 
Hilo la mvua inaweza kuwa kweli kak..
Nilipanda kitunguu heka 5, nilipo anza kuvuna siku hiyo hiyo ilinyesha mvua kiangazi nikala hasara sikupata kitu
Duuuh, ni sehemu gani huko? Locals nomaa
 
JAMANI EEEH UKIAMUA KULIMA WE LIMA CHA MUHIM MIMI NINACHO SHAURI NI KUANGALIA SOKO LIKOJE NI KWELI KWA SASA KITUNGUU SOKONI KIMEJAA LAKIN MPAKA UKALIMA NA KUJA KUVUNA LETS SAY MWEZ WA PILI AU TATU HAKUTAKUWA NA KITUNGUU SOKONI. HUO NDO UKWELI KUMBUKENI NA CHENYEWE NI PERISHABLE PIA WAKAT WA MASIKA KUKIPATIA NI IISUE SAANA. ILA KWA WAJANJA KAMA SISI HUU NDO MUDA PEKEE WA KLIMA KITU NGUU.

NI KWELI NDUGU ZANGU WAKAT WA MASIKA KITUNGUU NI SHIDA SAANA BUT TAKE IT FROM ME UKIFANIKIWA JAMANI UTAPIGA HELA KISHENZI
TAFTA MBEGU NZURI NA MADAWA MBEGU ZAAKO ZOOTE ZIWE F1
MFANO
1. RED CREOLE F1
2. RED BOMBAY F1
3. NEPTUNE F1
4. TAJIRIKA F1
HAPO UTAPIGA HELA KISHENZI SAANA AISEEE
 
Kitunguu chenye bei nzuri kinaanzia december to april, wakati huo wanaotamba na mzigo sokoni ni wale wenye uwezo wa kumwagilia tu. Lakini ukilogwa ukalima wakati wa masika may to september sokoni mzigo huwa mwingi kupita kiasi na bei yake hudondoka sana. Soko la kuanzia december to april wateja wanafuata mzigo wenyewe shambani tena kwa bei ya juu. Ukiwa na mzigo njoo tu hata hapa jukwaani uache namba ya simu uone huo usumbufu wa madalali.
 
Ukipata jibu pia unitag mm pia nimelima kama eka 2 za hii kitu na ndo mara yangu ya kwanza kujiingiza kwenye kilimo
MKUU NAOMBA NAMBA YAKO, NAOMBA MREJESHO WA PROJECT YAKO, NATAKA PIA KUINGIA HUKO, HOPE TUTABADIRISHANA MAWAZO JUU YA HII MIRADI.
 
wakuu wa jf nimepata eneo huko kagera. halituamishi maji kama mlivyoeleza ila ni kichanga flani hivi je linafaa kwa mbegu gani? vp kuhusu mbolea na madawa upatikanaji wake, na aina gani ni bomba zaidi. nisaidieni.
 
Inategemea na unapopanda lakini gharama zake sio chini ya 2,700,000/= kuanzia kukodi shamba hadi kuvuna kwa Ruaha Iringa. Mauzo yake hutegemea sana upatikanaji wa vitunguu kwenye soko.

Ukiwezakuvuna na kuuza mwenyewe rejareja bei inaanzia 100/= kwa kilo kama utauzia shambani bei inaanzia 50,000/= hadi 230,000/= kutegemea na uwingi wake sokoni. Mavuno inategemea na matunzo yako na vita ulivyopambana na wadudu waharibifu pia "imani yako" na mbegu uliyotumia. Kifupi ni biashara inayohitaji kujidhatiti hasa kwa kuwa na ufahamu wa kila kitu na usimamizi mzuri kuanzia mwanzo hadi siku unafikisha sokoni mzigo maana risk zipo nyingi.

Kuna wanaofanikiwa hasa pale utakapoweza kucheza vizuri timing ya mvua na forces za demand and supply, pia usikutane na pembejeo feki
 
Mimi nimevuna mwezi huu nimeamua kuvihifadhi kwanza ili niuze kuanzia mwezi december hadi march kama soko litakua zuri.
Unalima mkoa gani mm nataka nianze kulima mwezi huu sijachelewa?

Sent from mTalk
 
Habari,
Nimepata maeneo nzega nahitaji kuanza kilimo cha umwagiliaji na ufugaji kwa pamoja,je ni mazao gani na mifugo gani vinavyostawi nzega?
 
Habari wana jamvi mwebyewe uelewa wa hili zao na mahari ambo pazuri kwakilimo hiki naomba tuwasiliane ani pm.naitaji kuanza kilimo rasmi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…