Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

Kilimo cha vitunguu (saumu na maji): Ushauri na Masoko

Nina mzigo utatoka January kama gunia 200 ntakucheki wakati ukifika
Mkuu ulifanikiwa kutoa kitunguu January? Vipi Bei yake ilisimamaje? Nataka nianze mkulima ili nije kutoa hiyo miezi ila natamani kujua bei uwa kwa kipindi hiko zinakuwaje
 
Mkuu ulifanikiwa kutoa kitunguu January? Vipi Bei yake ilisimamaje? Nataka nianze mkulima ili nije kutoa hiyo miezi ila natamani kujua bei uwa kwa kipindi hiko zinakuwaje
Bei ya vitunguu hsifanani, msimu wa mvua bei iko juu sana na miezi kuanzia April hadi June.
Kwasasa inachezea 70 hadi 90k
 
Malila unaweza kunipa mwanga kidogo kuhusu bei za hayo maeneo ya Ruaha na hayo mengine kama unafahamu. Nataka nikasurvey na angalau kabla sijaenda huko nijue bei ya kununua kwa eka au ya kukodi kwa eka.

Kilimo Kwanza!
umeshapewa direction unataka upewe nn ,funga safari nenda
 
Nililima mang'ola kijiji cha kisiriri mwaka 2010 mzee mmoja akaniambia mwanangu umetoka chuo huku hatulimagi kwa kufuata elimu njoo nyumbani nikupe dawa uwekee uzio shamba lako na kwa vile shamba lako liko njiani watu wenye macho mabaya watahamisha mazao hutopata kitu, basi nikamshirikisha jamaa yangu tuliyekua tunafanya naye hiyo project akaniambia nimesomea kilimo Mimi ni mtaalamu hapo tuzingatie madawa, mbolea maji hachana na mambo ya kishirikina basi mzee nikamtolea nje akaniambia hili shamba mkilikinga mtatoa scania mbili na nusu ila mkipuuza hamtopata kitu, ebwana we kuja kuvuna tulipata gunia kumi, next year nikasema sikubali nikaenda kwa mzee mmoja milimani huko akanipa dawa nililima mahindi sio vitunguu manake kule ilikua ukikodisha shamba la kulima vitunguu unapovuna unaweka mahindi, nilfuata vigezo na masharti aisee alikuja jamaa na fuso nikamuuzia mahindi mabichi ekari sits, nilivyokunja pesa nilisepa nimevaa pensi na vesti niliacha begi na kila kitu, manake kule walikua na msemo kua mgeni hata aje na mil 500 tutamfirisi hadi akose nauli ya kurudi alikotoka so nilisepa kama nipo around vile sikubeba chochote zaidi ya mapene, mang'ola wale wambulu, mang'ati na wanyiramba Wa kitongoji cha kisiriri niliwavulia kofia kwa uchawi, na historian ya hicho kitongoji cha kisirri ni kijiji kipo iramba huko so wale wachawi waliofukuzwa iramba ndo wakaja kukaa hapo mang'ola na kuliita hill eneo kisiriri.
Mkuu unachosema kinaweza kuwa kweli mimi nikijana wa 20+ ila nimelima misimu mitatu katika Mkoa wa Dodoma nachoweza kusema Jambo lolote la kuleta mafanikio lazima ulilinde maana husda ya binadamu katika maisha yetu ni KUBWA
Nilianza kulima nikiwa na miaka 20 ufuta ekari 5 sikupata vizuri nikandondoka ila nikajaribu dengu ekari 18 nikapata magunia 48 hela msimu unaofata nikalima dengu tu ekari 30 nikapata magunia 90 but yote ilikuwa mavuno ya chini ila kujipa moyo kilimo cha mvua.... sasa niliishiwa nguvu mwaka unaofata ile nasema nayanyuka kwa nguvu nikajaribu ekari 50 za dengu hakuna kitu kilichoota kabisa pale hahaha mpaka leo sijawahi kulima tenah ila kilimo kina pesa sana me nimeiona katika umri mdogo sana na naamini nitarudi tenah now acha nitafute nguvu kwa kuendesha bolt na vibarua tofauti tofauti ila unachosema wewe ni kweli kilimo ushirikina sana sana ila ndo jamii zetu lazima ulinde mali kaka la siivyo wachawi ni wnegi na wamangati ndo wanaongoza
 
Back
Top Bottom