wana jf salam.
mimi ni kijana ambaye nategemea kuingia mtaani siku chache zijazo(nipo kdt cha 6)
kati ya sekta ambazo nafikiria kuwekeza ni katika kilimo kwani baba alipoondoka ardhi ndo rasmali kubwa aliyoiacha.
kutokana na kwamba nililelewa dar nina ufaham mdogo sana kuhusu kilimo ndo maana imenibidi kuwauliza ndugu zangu ili nijue la kufanya mara tu ninapomaliza elimu yangu ya sekondari na nitakapokuwa naendelea na elimu ya juu.
mashamba hayo yapo mkoani kagera wilaya ya ngara hivyo anayefahamu kuhusu kilimo hasa kwa maeneo husika naomba unifahamishe ili nijue la kufanya,
natanguliza shukurani.
Kilimo kinalipa sana hakuna biashara yenye ROI kubwa Kama Kilimo mkuu.Fanya utafiti utanambia kwa hili,hulipi kodi,pembejeo unauziwa bei Sawa na bure sasa si super profit hiyo Mungu akupe nini
Kilimo kinataka full participation na uwe na kipato kingine nje ya kilimo ili kukabili up and downs za kilimo. Kwenu Ngara kuna tatizo la manpower, migomba ndio hiyo inaliwa na ugonjwa, kahawa inayumba yumba ktk soko, sina hakika na kasheshe za Vanilla. Mazao mengine balaa liko ktk masoko huko kwenu. Sijui ardhi yenu ni kubwa kiasi gani, unaweza jaribu kufuga kienyeji wakati huu unaposoma.
Kama ungekuwa unaishi kule kule Ngara ningekushauri ukomae na kilimo, lakini kama utalima kwa njia ya simu, unaweza pata ugonjwa.
Uko wapi Malila
Nije kula shule ya kilimo na ufugaji kuku
Niko mkoani Lindi naangalia fursa za huku. Unajua kila siku lazima kujifunza. Huku kuku wa kienyeji wanauzwa bei ndogo, na hata mbuzi wanauzwa bei ndogo.
Unatisha mkuu!
Sikupatii picha miaka 10ijayo utakuwaje kiuchumi!
Utarudi lini dar nakuhitaji sana
Ntaingia Dar 22april na nitakuwepo kwa week moja,baada ya chai day naenda shambani.
Poapoa
Nitakutafuta
Mwalimu wako alikuwa kipofu afu akakupata mwanafunzi mwenye "spinal cord" tu.
Ili uwe mkulima haswa uende sua ukasome agriculture general
Hongera kwa mawazo ya kimapinduzi amini usiamini kilimo kinalipa sana alimradi tu usimamie kwa ukaribu sana ndio maana sasa wawekezaji wanakamata ardhi. Jaribu kuzalisha avocado pears grafted siku hizi zina soko kubwa sana hata nje kwani zinatumika pia kutengeneza product nyingi mbali na kuliwa kama tunda, kikubwa ni uzalishe kwa wingi
mkuu ila gambling inaeza kukutoa..au co?
Ntaingia Dar 22april na nitakuwepo kwa week moja,baada ya chai day naenda shambani.
Chai Day ni lini mkuu?
Tarehe 26april jumamosi saa nane na nusu. Ukumbi utatangazwa baadae.
Ikulu tu
Ha ha ha
Tukaribishane kwenye hiyo chai