Kilimo ni biashara pekee inayolipa kwa 100%


Mkuu ni mazao gani ulilima na ulilimia wapi, mbona gharama za nguvu kazi saidizi ni nafuu?
 

Hapa naona kama tunaingizana mjini. Kwa kawaida gharama ya tractor kwa walio wengi kwa heka ni 40-60 elfu. Halafu ulipaswa kutuambia ulilima zao ghani maana mbali ya maelezo yako mazuri huonyeshi ni zao gani ulilima na aina ya mbegu ndio maana naona kama unatudanganya. Pia hizo gharama zako za kulima hasa hao vibarua ziko chini sana kulinganisha na sehemu nyingi, au wewe ni mwalimu mkuu wa shule fulani hivyo unawatumia wanafunzi kukufanyia kwa bei hiyo?
 
Ni maindi ulilima au zao gani?
 
Acha kudanganya watu mtoa mda,kuandika hapa ni rais tu lakini utekelezaji wake ni mgumu sana.
Kilimo ni kamali kubwa sana hasa kilimo cha kutegemea mvua.
 
Inategemeana na sehem gharama za kulima kwa Trekta, kama huku napoishi ni 28,000/= kukodisha kama ni mahindi heka moja haizidi 100,000/= hutegemei mvua, maji ni ya mifereji ambayo gharama yake ni kila mwezi kunakuwa na msaragambo wa kusafisha mifereji.
Kila sehem kuna tofauti sana na sehem zingine
 

Kwenye suala la trekta 25 elf inawezekana.
Kwenye vibarua, bado ninaweza kumuamini japo kwa shida.
Kwenye mbegu hapo mpaka atuambie kwanza ni zao gani na alilimia wapi?
 

Ni wapi huko, na heka moja ya mahindi unavuna kiasi gani?
 
Ni kweli usemayo mkuu, lakini mbona wakulima ndio jamii masikini kabisa humu nchini kama kweli inalipa kihivyo?
Wengi wanafanya kilimo kwakuwa hawana namna nyingine ya maisha, hivyo malengo yao makuu ni kutibu njaa.
Ndio maana hata Kama kilimo kikimpa matokeo makubwa yaani yaliyozidi ile kuganga njaa, mkulima huyu hufanya ya ajabu.
Mfano mwaka jana Huko Mtwara na Lindi tulisikia vioja kedekede kama kuwanywesha mbwa bia. Tu kwasababu matokeo yamezidi malengo...
 
Nalima kibaya-Manyara heka inaanzia 25 elf

Mkuu mimi nalima katesh na Tanga. Katesh haipungui 40 kwa heka wakati Tanga ni 50. Mkuu ni kweli ni bei za tractor mnazungumzia au ni ng'ombe na punda?
 
Alafu ishu ya gharama za vibarua zinatofautiana kulingana na mtakavoelewana. Mfano mi navofaham, wakati nalima huwa nina kijana wangu ambae huwa nampelekea unga wa dona kindoo kidogo, dagaa sado moja, betry za tochi 4 na mafuta ya mboga lita. Nikivuna huwa nampa sehem ya nilichokipata kama vitunguu nampa gunia 5
 
Mkuu mimi nalima katesh na Tanga. Katesh haipungui 40 kwa heka wakati Tanga ni 50. Mkuu ni kweli ni bei za tractor mnazungumzia au ni ng'ombe na punda?
Mi nalima sehem inaitwa kikuletwa ipo wilaya ya hai heka kulima na trekta ni 28,000 mpaka 30,000 kama shamba lina pori
 

Hicho chakula ulichosema anakula muda gani? Wakati analima hapo shambani huwa analala wapi? Huwa unampa gunia tano, je huwa unapata gunia ngapi kwa heka?
 
Ulifanya kilimo cha umwagiliaji au?

Vipi gharama za kukodi shamba zako je?

Baada ya msimu wa mvua kuisha nategemea kuja pande hizo.
Ni kilimo cha umwagiliaji, dharama inategemeana na zao unalotaka kulima alafu pia inategemeana na shamba linatumia maji ya mifereji au ni la kutumia pump
 
Hicho chakula ulichosema anakula muda gani? Wakati analima hapo shambani huwa analala wapi? Huwa unampa gunia tano, je huwa unapata gunia ngapi kwa heka?
Baada ya mwez ndio unamuongezea dagaa na betry pia mafuta kama yameisha unamwongezea, Unga unakaa hata miez miwil. Anakaa shambani kuna kibanda. Vitunguu ndio huwa vinatoaga gunia nyingi hivo nampa idadi ya gunia kulingana na kiasi nilichopata na pia bei ya gunia
 

Duu huyo kijana umempata wapi, maana mimi nina vijana wawili wangalau wanakula kilo moja ya unga kwa siku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…