Kilombero Sugar Yaandaa Mkutano wa Wadau wa ndani 2025

Kilombero Sugar Yaandaa Mkutano wa Wadau wa ndani 2025

News TZ

Senior Member
Joined
Jun 17, 2015
Posts
132
Reaction score
75
WhatsApp Image 2025-02-06 at 4.16.42 PM (2).jpeg

Morogoro, 6 Februari 2025. Kampuni ya sukari Kilombero, leo imeandaa Mkutano wa Wadau ambao umewakutanisha na viongozi wapya wa serikali za mitaa pamoja na wadau wengine kutoka bonde la kilombero muhimu kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kujadili mikakati ya kimaendeleo.

Mkutano huu, uliofanyika katika makao makuu ya kampuni, umetumika kama jukwaa la kuwakaribisha viongozi wapya wa serikali za mitaa, kuimarisha mahusiano, na kuboresha mawasiliano kati ya Kilombero Sugar na wadau wake wa ndani. Majadiliano yalijikita katika maendeleo ya Mradi wa Upanuzi wa Kiwanda cha K4, mkakati mpana wa biashara wa kampuni, na uundaji wa hifadhidata ya kina ya wadau ili kurahisisha ushirikiano na usambazaji wa taarifa.

Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mh.Dunstan kyobya, akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , ameipongeza kampuni ya sukari Kilombero kwa kujitolea kuendeleza ushirikiano na wadau wa ndani.

"Dhamira ya Kampuni ya sukari Kilombero ya kuweka mawasiliano ya wazi inastahili kupongezwa. Njia hii ni muhimu katika kujenga imani na kuhakikisha kwamba wadau wote wanapata taarifa sahihi kuhusu shughuli za kampuni na mipango yake ya baadaye," amesema Mh. Kyobya.

Hata hivyo Waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa Afrika mashariki, ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Mikumi Mh. Denis Londo, amesisitiza umuhimu wa kudumisha ushirikiano baina ya kampuni na jamii, Sukari ya Kilombero. Amebainisha kuwa ushirikiano huu unapaswa kubaki imara na utumike katika kushughulikia masuala ya jamii

Mkurugenzi wa Uhusiano na mawasiliano wa kampuni ya sukari Kilombero Bw. Derick Stanley, amesisitiza umuhimu wa mazungumzo ya wazi na uwazi katika kujenga ushirikiano endelevu.

"Mkutano huu umetupa fursa ya kipekee kujadiliana na viongozi wa serikali za mitaa na wadau kuhusu maendeleo muhimu ya biashara. Kwa kushirikiana, tunaweza kuleta maendeleo ya kiuchumi yatakayowanufaisha kampuni na jamii tunazozihudumia," amesema Bw. Stanley

Akiorodhesha malengo ya mkutano huu Meneja wa Mawasiliano na Mahusiano kwa Wadau wa Kilombero Sugar, Victor Byemelwa, amezungumza yafuatayo.

Ukaribisho wa Viongozi Wapya wa Serikali za Mitaa – Kuwatambulisha viongozi wapya kwenye shughuli za Kilombero Sugar na kuimarisha ushirikiano kwa maendeleo ya pamoja.

Taarifa ya Maendeleo ya Mradi wa Upanuzi wa Kiwanda cha K4 – Kutoa muhtasari wa maendeleo na mkakati wa muda mrefu wa mradi huu, ambao unalenga kuongeza uzalishaji wa sukari na kuchochea ukuaji wa uchumi wa ndani.

Uundaji wa Hifadhidata ya Wadau – Kuanzisha mfumo rasmi wa kuhifadhi taarifa za wadau ili kuboresha mawasiliano na ushirikiano.

Ripoti ya Robo Mwaka – Kuwapatia wadau taarifa za maendeleo ya kila robo mwaka, ikiwemo mafanikio ya kampuni.

Kwa kuimarisha ushirikiano na wadau wa ndani, Kilombero Sugar inaendelea kuonesha dhamira yake ya kuendesha biashara kwa njia endelevu na kuchangia maendeleo ya jamii. Mkutano huu ni hatua muhimu katika kujenga ushirikiano wa muda mrefu unaounga mkono ukuaji na mafanikio ya pamoja.
WhatsApp Image 2025-02-06 at 4.16.43 PM.jpeg

WhatsApp Image 2025-02-06 at 4.16.42 PM (1).jpeg

-MWISHO-

Mawasiliano kwa Vyombo vya Habari

Victor Byemelwa

Meneja wa Mawasiliano na Mahusiano na Wadau

📧 Vbyemelwa@illovo.co.tz



 
Back
Top Bottom