Kim Jong Un wa North Korea atangaza kutumia mabomu ya nyuklia kuipiga Korea Kusini iwapo atachokozwa!

Kim Jong Un wa North Korea atangaza kutumia mabomu ya nyuklia kuipiga Korea Kusini iwapo atachokozwa!

Joined
Jan 6, 2022
Posts
56
Reaction score
336
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un ametishia kutumia silaha za nyuklia kuiangamiza Korea Kusini iwapo itashambuliwa, vyombo vya habari vya serikali vimeripoti Ijumaa, baada ya Rais wa Korea Kusini kuonya kwamba ikiwa Korea Kaskazini itatumia silaha za nyuklia itakuwa ni “mwisho wa utawala wake.”

Matamshi haya makali si mapya, lakini yanakuja wakati wa mvutano kwenye peninsula ya Korea na ni wiki chache baada ya vyombo vya habari vya Korea Kaskazini kuonyesha picha za Kim akitembelea kituo cha kurutubisha uranium, ambacho huzalisha malighafi za silaha za nyuklia.

Akiwa kwenye ziara ya kambi ya jeshi katika sehemu ya magharibi ya nchi hiyo Jumatano, Kim alisema iwapo Korea Kusini ingejaribu kuvamia uhuru wa Korea Kaskazini, Pyongyang “itazitumia bila kusita nguvu zote za mashambulizi ilizo nazo, ikiwemo silaha za nyuklia,” Shirika la Habari la Serikali la Korea Kaskazini (KCNA) liliripoti Ijumaa.

“Iwapo hali hiyo itatokea, kuwepo kwa kudumu kwa Seoul na Jamhuri ya Korea hakutawezekana,” Kim aliongeza, akitumia jina rasmi la Korea Kusini.

Uhasama kati ya viongozi hao wawili wa Korea umeendelea kutokota mwaka huu, huku Korea Kaskazini ikionekana kuongeza juhudi za uzalishaji wa silaha za nyuklia na kuimarisha uhusiano wake na Urusi, hali ambayo imeongeza wasiwasi mkubwa Magharibi kuhusu mwelekeo wa taifa hilo lililojitenga.

Matamshi ya Kim yanaonekana kuwa majibu ya moja kwa moja kwa Rais wa Korea Kusini Yoon Suk Yeol, ambaye Jumanne alionyesha kombora la balistiki lenye nguvu zaidi la Seoul na silaha nyingine zilizoundwa kwa lengo la kuzuia vitisho vya Korea Kaskazini wakati wa gwaride la Siku ya Majeshi.

===================================================

North Korean leader Kim Jong Un threatened to use nuclear weapons to destroy South Korea if attacked, state media reported Friday, after South Korea’s president warned that if the North used nuclear weapons it would “face the end of its regime.”

The fiery rhetoric isn’t new, but comes at a time of tension on the Korean Peninsula and just weeks after North Korean state media released images of Kim visiting a uranium enrichment facility, which produces weapons-grade nuclear materials.

While touring an army base in the western part of the country Wednesday, Kim said if the South were to encroach upon the North’s sovereignty, Pyongyang “would use without hesitation all the offensive forces it has possessed, including nuclear weapons,” the state-run Korean Central News Agency reported Friday.

“If such situation comes, the permanent existence of Seoul and the Republic of Korea would be impossible,” Kim added, using the proper name for South Korea.

Hostilities between the two Korean leaders have been simmering this year as North Korea has appeared to have intensified its nuclear production efforts and strengthened ties with Russia, deepening widespread concern in the West over the isolated nation’s direction.

Kim’s comments appeared to come in direct response to South Korean President Yoon Suk Yeol, who on Tuesday showcased Seoul’s most powerful ballistic missile and other weapons designed to deter North Korean threats during a parade for Armed Forces Day.

Source: CNN
 
Siyo swala kumuagiza akosome, wewe uliyeleta hayo madai ndiyo uyayetee hapa
Katika vita ya dunia yeye alikuwa akisambaza silaha ili watu wapigane

kwa hiyo hukusoma kabisa ? kwamba hujui? Japan alipiga assets za USA ndio maana USA alimshambulia dk za mwishoni...
 

Attachments

  • Screenshot (403).png
    Screenshot (403).png
    107.8 KB · Views: 6
Katika vita ya dunia yeye alikuwa akisambaza silaha ili watu wapigane

kwa hiyo hukusoma kabisa ? kwamba hujui? Japan alipiga assets za USA ndio maana USA alimshambulia dk za mwishoni...
Hiyo ni tofauti na kugombanisha. Huyo alikuwa akisambaza supplies sababu ya kuwa na industrial capacity ya ku produce demands pia alikuwa na supply chain nzuri kwa ajili ya logistics.
Sioni ni namna gani hapo useme yeye ndiye aliwagombanisha. Mbona madai uliyoyatoa na ushahidi uliouleta havifanani na wala havijuani?
 
Hiyo ni tofauti na kugombanisha. Huyo alikuwa akisambaza supplies sababu ya kuwa na industrial capacity ya ku produce demands pia alikuwa na supply chain nzuri kwa ajili ya logistics.
Sioni ni namna gani hapo useme yeye ndiye aliwagombanisha. Mbona madai uliyoyatoa na ushahidi uliouleta havifanani na wala havijuani?
Huoni kama ni tatizo hilo , kupeleka pesa ndefu kwa watu wanaou watoto ,wanawatolea watu kinga kabisa iliyowekwa na umoja wa mataifa ili wakiuke sheria ya vita.
 
Bado hujadhibitisha Marekani amewagombanishaje.
Kumbe kitendo cha huyu kubaki na tamaduni za asili na huyu kuwa na tamaduni za kizungu ndio unaita kugombanishwa.
Hapo ndio uwezo wako wa kufikiri/ku reason ulipoishia?
 
Soma ndio utajua , mmoja ana tamaduni za wazungu na mwingine ana tamaduni za asili.
Dictatorship ndo tamaduni za asili?

Kwasababu South Korea imeamua kuwa nchi ya Democracy na uhuru ndo imeiga tamaduni za kizungu?
 
Back
Top Bottom