Kimeumana Vanilla Njombe: Ni utapeli mtupu

Nadhani Mariki Boy hujawafuatilia hawa walima vanilla wa Njombe na utaratibu wao, vinginevyo hilo suala la kutafuta miche ya migomba na Jatropha kama chanzo cha kivuli usingelisema hapa.
Sure Mkuu sijawafuatilia lkn kwa ninavyo fahamu vanilla huwezi kulima bila kuchanganya na Migomba au Jatropha plant lkn kama wanatumia Green house ni sawa Mkuu
 
Mkuu na we uko chaka mana binafs nina uzoefu wa kutosha na vanilla. Kuna kg 300 nimekosa mteja hata wa tsh 400000@kg. Hawa jamaa wa njombe nilijua tu ni suala la muda. Ukitaka kujua kilio cha vanilla nenda kagera.
Kweli niko porini aisee. Ningekuwa Njombe bc ningeshapigwa.😭
 
Hii kitu ikiruhusiwa na ukawekwa mfumo rahisi wa kuipeleka kwenye masoko ya nje Ulaya na Marekani naacha kila nachofanya naingia kwenye hiki kilimo !

Ikiruhusiwa haitakua na bei nzuri itakua kawaida kama mahindi uku mkoani..ule uharamu pia unaongeza bei kidogo
 
Ya tz unanunua sh ngap. Kumbuka tunaongelea kile ulichosema kuwa unanunua na kuuza. Habar ya bei ya kule tuiache kwanza!

Mimi naishi nje ya nchi na ninanunua ya Madagascar kila wakati
Kweli nimesema nanunua na kuuza lakini sijasema ya Tanzania bali nimeongelea soko la Dunia

Nilijaribu sana kupata wauzaji wa Vanilla nyumbani bila mafanikio au ahadi hewa au vikwazo vingine

Kununua Madagascar ni rahisi sana kwani makampuni yako kwenye mitandao na ni straight forward hakuna kona kona unawasiliana nao kwa e-mail na mnayamaliza na anakutumia details zote

Nisamehe kama umeelewa kuwa nachukua mzigo bongo maana huko nilishindwa kabisa
 
Haooo jamaa uliowatajaa ni shida tupuu Mkuuu

Sent from my SM-A260F using JamiiForums mobile app
 
Na hapa Morogoro nimesikia Radio moja ya dini ikitangaza hayo mambo ya kitapeli ya vanilla eti bei ya mche mmoja Ni 5,000/ na ada ya mafunzo Laki mbili.
Umenikumbusha yale matangazo ya ufugaji samaki na sungura waliosemekana kuhutajika Israel. Wanatoa matangazo ya aina hiyo na kukuonesha soko kumbe biashara yao ni vifaranga, vikishakuwa utajijua mwenyewe.
 
Nimekuelewa. Nitaftie soko la nje. Kuna stock ya average 400kg toka muunganiko wetu wakulima wa kienyeji. Na tz tusipopunguza urasimu na awareness kwa wakulima kuhusu international marketing and trade bas wakulima wadogo tutazid kunufaika kidogo. Vanilla ya kagera ni grade A yenye vanillin 2-3%, humidity 25-35%, length 17cm lakin soko hakuna. Kampun ya Mayawa iliyoodhi zao na soko imeganda. Waganda wanaichukua kagera kimagendo wanauza nje inaonekana wao ndo east african big exporters km ya tanzanite. Tz wasomi ndo wanaleta vya udalali na kutuharbia biashara.
Najiuliza kwanini baloz zetu arabun, scandnavia na germany hawatusaidii kupata masoko ya uhakika. Sasa elimu ya ujamaa inafeli kuvuka mipaka
 

Mkuu kwanza poleni sana kwa kadhia hizo zinazowapitia
Kama utakuwa ni mfuatiliaji wa threads za kilimo utakuwa umeona hili zao limezungumziwa sana humu na mimi nilikuwa mmoja wa wachangiaji

Kupata vibali vyote ndio shida Tz sijui huwa wanamkomoa nani na anaeumia sio mkulima tu bali hata wanaotaka kufanya biashara huko na wengi hukumbia

Yaani unaweza kupata usafirishaji wa Mbuzi kutoka Somalia kwenda Uarabuni kwa Urahisi kuliko kupata kibali home
Tuna kila kitu ila ukiangalia masoko makubwa ya Ulaya utakuta mbogamboga na matunda yanatokea Uganda na Kenya na sio Tz

Mkuu Kilograms 400 ni nyingi mno mimi huwa nanunua kidogo sana ukilinganisha na mzigo huo ila kama mtajitangaza kwenye website hamuwezi kukosa wanunuzi ila ni kujihadhari tu na matapeli kwani wana mbinu nyingi sana
Nakutakia kila la kheri
 
We mdau una theory. Wengine tayar miaka 10 nyuma tumejihusisha na hili zao. Unaambiwa tatzo si mfumo wa uendeshaj wa uwekezaj bali ni huu mkanganyiko wa bei si halisia mana hawajaanza wao. Na hawatauza mbinguni. Mfano wako wa barrick unaweza usilenge hoja ya mezan. Mbaya zaid walipojitangaza tumewaaproach wanunue zilizo tayar hawatak hata nusu ya bei wanayojitangaza. Amini tu watu wanawekeza kwa expectations kubwa wakat ni next to impossibility. Kupigwa ndo huko. Hata historia ya mmojawapo akiwa na kipind cha greenhouse inaongeza nia ovu kwao. Lakin tuliwashtua kipind wamejitokeza itv na v8 kuwa mkuwe makin. Ila nawakubal kwa uwezo wao mkubwa wa kujibrand na kushawishi. Binafs nailaum serkal inawajua watu wake hawa hawa wanaopigwa hata kijinga kwa tuma humu. Usalama wa Taifa na uchumi wa nchi haviachan wangewauliza had soko lao na mikataba yao. Na insurances zao. Na comparative studies. Na baloz zikahusika. Ujue watu wamekopa, wastaafu wamewekeza. Pesa ndefu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…