Elections 2010 Kimya cha CHADEMA kikubwa

Elections 2010 Kimya cha CHADEMA kikubwa

Mzee wetu Mhe. FREDERICK SUMAYE atueleze nini kinaendelea kati yake na viongozi wakuu wa CHADEMA? Ni juzi tu tarehe 16 Juni majira ya sa 3.15 asubuhi maeneo ya Protea Hoteli iliyopo Oysterbay nilimuona kwa MACHO YANGU mheshimiwa huyu akiwa kwenye gari yake aina ya Landcruiser namba T634 AKN akipokelewa na vigogo wa CHADEMA akiwemo Mhe. MBOWE, DR. SLAA na aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA BOB MAKANI na kuelekea kwenye chumba cha mikutano. Walijifungia kwenye chumba hicho takribani saa mbili na zaidi hadi mishale ya saa 5.20 hivi asubuhi ndipo kigogo huyu alipoondoka eneo hilo. Uswahiba huu umeanza lini??

Nampa HEKO! Napenda kumweleza kuwa kama CHADEMA wamempenda basi atueleze tumpigie debe kwani hadi sasa CHADEMA haijawa wazi nani atagombea kinyangányiro cha kiti cha Urais mwaka huu wa uchaguzi. Pengine bado CHADEMA wanawinda majeruhi wa CCM??

Rai yangu kwa Mheshimiwa SUMAYE ni kwamba, haki kikatiba anayo inayomlinda katika upigaji na upigiwaji wa kura ila mzee, wenzio wa upande wa pili wanayo taarifa hiyo? Au unacheza rafu?

Namtakia kila lililo kheri kwenye mazungumzo yake kuelekea utekelezaji wa demokrasia.
Kuwa wazi, usijifiche una kila haki.

mimi, Chilomo Chiwale

Embu tueleze na wewe ulikuwa unafanya nini hapo? Wewe ulienda kufanya mkutano na nani?
 
Chilomo Chiwale, hii sasa unaharibu, hata kama ni kweli uliyashuhudia hayo, hizo ni faragha za watu, umezileta hapa ili ama kumuharibia, ama kiharibia Chadema, kwani hata kama alikuwa analitafakari ombi lolote toka Chadema, na kabla hajafikia maamuzi, wakasikia limeibukia JF, si ata ghairi?.

Ndio maana kuna wakati mwingine, unasikia jambo, unashuhudia jambo, unalihifadhi mpaka upate uhakika.

Chilomo unawezekana wewe ukawa ni membe wa kundi la manyoka wa TISS, umetumwa kazini kwako kufuatilia, sasa unamfitinisha na Chadema ili kumuharibia mafao yake?!.

Sumaye ni mtu huru kama walivyo wengine ana uhuru wa kukutana na yoyote popote bila kuvunja sheria yoyote, hivi unajua hata Zitto ni rafiki na JK, ukiwaona wanacheka na kutembeleana, sio ndio utalianzisha Zitto huyooo...CCM.

CHADEMA ENDELEZENI MIKAKATI, SYSTEN ON OPARATION MPAKA NDANI YA JF!

BROTHER PASCO LOOH!!! unanitisha ndugu yangu, hata hivyo najifunza. Kumbe sikutakiwa kulizungumza hili ni mapema mno? Lakini kama utakuwa makini mimi nimeuliza swali tu.
 
thank you mganyizi kwa kunipa moyo kwani nilishaanza kuogopa kuwa huenda nimekurupuka pia sina haki ya ku share yale niliyoyaona.

Naamini jf ipo kwa ajili ya kujuzana. Najifunza pia. Nimeshakaribia.

Wala usiwe na hofu we dare to talk openly, vikao vya Lowasa na kundi lake vilikuwa vinaripotiwa hapa hata wakikutana porini kwenye mbuga za wanyama huko Manyara. Wala hujavunja sheria yeyote. Hata hivyo JF tunapenda zaidi ushahidi ili kupata uhakika wa jambo. Kwakuwa wewe ndiyo source weka hata picha basi.

By the way kama chadema watamuweka Sumaye sidhani kama watapata mafanikio makubwa. Sumaye alikuwa waziri Mkuu kwa miaka 10 hakufanya mengi, pia alichafuliwa sana kama si kuchafuka. Sumaye hawezi kuwa na muarobaini wa matatizo tuliyonayo sasa, we need serious leaders Chadema wangemshawishi Dr. Salim vinginevyo wamuunge mkono Prof. Lipumba.

Binafsi siamini kama Sumaye anaweza kukutana na viongozi wa chadema for a serious political talks ndani ya jiji la Dar es Salaam. Wangeweza kukutana nje ya Dar tena hata nje ya nchi kabisa. Kama hii ni kweli basi makubaliano yao yamefikia hatua za juu sana na Sumaye ameshafanya maamuzi na yupo tayari kwa liwalo na liwe.
 
Mzee wetu Mhe. FREDERICK SUMAYE atueleze nini kinaendelea kati yake na viongozi wakuu wa CHADEMA? Ni juzi tu tarehe 16 Juni majira ya sa 3.15 asubuhi maeneo ya Protea Hoteli iliyopo Oysterbay nilimuona kwa MACHO YANGU mheshimiwa huyu akiwa kwenye gari yake aina ya Landcruiser namba T634 AKN akipokelewa na vigogo wa CHADEMA akiwemo Mhe. MBOWE, DR. SLAA na aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA BOB MAKANI na kuelekea kwenye chumba cha mikutano. Walijifungia kwenye chumba hicho takribani saa mbili na zaidi hadi mishale ya saa 5.20 hivi asubuhi ndipo kigogo huyu alipoondoka eneo hilo. Uswahiba huu umeanza lini??

Nampa HEKO! Napenda kumweleza kuwa kama CHADEMA wamempenda basi atueleze tumpigie debe kwani hadi sasa CHADEMA haijawa wazi nani atagombea kinyangányiro cha kiti cha Urais mwaka huu wa uchaguzi. Pengine bado CHADEMA wanawinda majeruhi wa CCM??

Rai yangu kwa Mheshimiwa SUMAYE ni kwamba, haki kikatiba anayo inayomlinda katika upigaji na upigiwaji wa kura ila mzee, wenzio wa upande wa pili wanayo taarifa hiyo? Au unacheza rafu?

Namtakia kila lililo kheri kwenye mazungumzo yake kuelekea utekelezaji wa demokrasia.
Kuwa wazi, usijifiche una kila haki.

mimi, Chilomo Chiwale

Pamoja na kuwa unajifanya kuwa ni mgeni humu lakini wewe ni mzoefu sana tu. Uliwezaje kwenda kuichokonoa hii thread ilikojificha. Ndiyo maana tunasema kuwa nyie watu pamoja na kujifanya smart lakini hamna kitu kwani mnaacha footprint kibao nyuma. Wewe tumia jina lako hilo hilo
 
u want to tell me kimya cha chadema kimeibuka na Sumaye?
 
Dr Slaa ameshavuka kwa mbali hii ngazi ya UBUNGE. Anaogopa nini kugombea URAIS? Atachelewachelewa kama alivyofanya SAS tangu mwaka 1985 hadi akaja kuchukua fomu 2005! Ikawa tayari kila kitu hakiko upande wake.
Dr Slaa, bila kuikamata IKULU sasa huko mbeleni itakuwa vigumu sana kwako. Wala jitihada zako BUNGENI na ndani ya majukwaa ya CHADEMA havitatusaidia sana WATANZANIA.
 
Dr Slaa ameshavuka kwa mbali hii ngazi ya UBUNGE. Anaogopa nini kugombea URAIS? Atachelewachelewa kama alivyofanya SAS tangu mwaka 1985 hadi akaja kuchukua fomu 2005! Ikawa tayari kila kitu hakiko upande wake.
Dr Slaa, bila kuikamata IKULU sasa huko mbeleni itakuwa vigumu sana kwako. Wala jitihada zako BUNGENI na ndani ya majukwaa ya CHADEMA havitatusaidia sana WATANZANIA.


I think Dr Slaa akisikia huu ujumbe anaweza kubadiri mawazo yake
 
rais bado kwa tanzania kutoka upinzani ..................upinzani ndio kwanza unahitaji kupigania majimbo.
 
mhhh mambo haya mazito kama ni kweli
 
Huu ndo mshindo wenyewe sasa Gooooo dr SLaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Back
Top Bottom