Kina dada tupunguze maamuzi yasio ya muhimu kwa kaka zetu waingiapo kwenye ndoa zao

Kina dada tupunguze maamuzi yasio ya muhimu kwa kaka zetu waingiapo kwenye ndoa zao

Evelyn Salt

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
70,916
Reaction score
141,437
Amani iwe kwenu,

Napenda kushare hili, tabia ya sisi kina dada kushindwa kutambua na kuthamini nafasi za mawifi zetu kwa makusudi, kwa kujitoa ufahamu au kutokujua kwa bahati mbaya, hadi inafikia mahali tunakua na maamuzi yasio ya lazima kwa kaka zetu.

Wapendwa hakuna mtu asietambua umuhimu wa ndugu kwani wao ndio wanajua wapi wametoka, mangapi wamepitia pamoja hadi kufika mahali walipo, lakini sidhani kama ni sababu ya kushindwa kutambua na kuthamini kuwa ndugu (kaka) ameishaongeza jukumu lingine (mme) kiasi kwamba kuendelea kujiona kwamba dada una uhuru wa maamuzi kwake.

Undugu upo palepale tena upo sana lakini ni vema maamuzi ya kaka kwa mambo ya familia aachiwe mkewe (wifi), labda tu kama dada umeombwa ushauri,binafsi naona kumfanyia kaka maamuzi wakati tayari ana mkewe ni kutafutana tu migogoro na wifi na inawezekana hata kuwa moja ya sababu za mawifi kutopendana mfano dada kumpangia kaka ake matumizi na mgawanyo wa pesa kiasi hiki kaka nunua kioo, kiasi kile nunua mswaki na kiwi kingine peleka bank wtf!

Nafasi ya mke ni nini sasa? Tutajatukanwa mambo ya nguoni jamani tuone tumeonewa, hivi hata wifi akija gundua dada mtu ndio mpangaji wa matumizi ya nyumbani kwake atajisikiaje?Na kaka nae anawezaje kuruhusu huu ulofa katika familia yake?

Inawezekanaje dada kwenda kwa kaka na kujimwaga mwaga hadi chumbani kwake ilhali sio geto ni chumba chake na mkewe?inawezekana kukaa na kaka na unamlisha chakula ilhali mkewe yupo? Uzungu au rusha roho?

au kutembea njiani na kaka mshikane mikono afu mke pembeni kajibebea zake kipochi, ni upendo wa ndugu sawa, ila huwa hauna mipaka? Tunapenda ndugu zetu tena upendo wetu haupimiki lakini ni vema upendo uwe na mipaka especially ndugu zetu wakishajiongezea jukumu lingine la mke/mme ni hayo tu ni mawazo yangu tu we unawazaje?
 
Ila me nafikiri mwanaume (kaka) ndo anatakiwa asimame kiume (awe na msimamo), otherwise ataendeshwa na madada zake hadi ndoa imshinde. Asipowaruhusu dada zake kumtawala, basi hakuna atakayemtawala. Na huyo dada wa kumpangia kaka ake matumizi yeye hana familia ajipangie matumizi yake khaaa!! Mwanaume ndo kichwa cha familia yake na sio dada zake. Kichwa kikitetereka Kila kitu kitaharibika
 
unaanzaje kuingilia ndoa yangu kama wifi?? sahau kabisa maana ukijaribu siku ya 1 tu sikufumbii macho
 
kwenye maamuzi sawa... ila kwenye kushikana mikono na kulishana punguza wivu kidogo, vitu vya kawaida hivyo!!!
 
Hahaa daaah umenikumbusha....mimi na kaka yangu ninayemfuata tangu tupo wadogo tunapendana kishenz...yan ni marafiki haswaaa...tukikaa pamoja full kutaniana, kupigana,kukimbizana yan full raha. Sasa juzi tu hapa hata kaja kututambulisha mkewe mtarajiwa. Bas my elder sista kaniambia nianze ku-maintain distance maana keshakuwa na wake sasa...yaan ni furaha iliyochanganyika na machungu
 
Mnalishana chakula na dada yako mkeo amekaa pembeni...?mbaya zaidi ukute ukiwa na yeye hufanyi hivyo

hiyo ni kama mazoea, tumefanya hivyo tangu watoto... leo nijizuie kwa kuwa mke yupo karibu!!? kwanza unaanzia wapi kumuonea wivu dada wa damu wa mme wako kisa kulishana
 
Ila me nafikiri mwanaume (kaka) ndo anatakiwa asimame kiume (awe na msimamo), otherwise ataendeshwa na madada zake hadi ndoa imshinde. Asipowaruhusu dada zake kumtawala, basi hakuna atakayemtawala. Na huyo dada wa kumpangia kaka ake matumizi yeye hana familia ajipangie matumizi yake khaaa!! Mwanaume ndo kichwa cha familia yake na sio dada zaje

Mawifi tuna mambo teh usione twaambiwa tuna gubu kama ndugu wa mme
ndo haya mambo ta kushindwa kujua mipaka hadi tunaingilia mawifi kwenye majukumu yao
 
Mawifi tuna mambo teh usione twaambiwa tuna gubu kama ndugu wa mme
ndo haya mambo ta kushindwa kujua mipaka hadi tunaingilia mawifi kwenye majukumu yao

Sasa hapo wanandoa ndo inabidi muwaonyeshe mipaka yao kwa vitendo tena kuwa "bibi wewe mwisho wako ni hapa, huku ndani hakukuhusu". Ukiwaendekeza madada wasiojitambua kweli ndoa itakushinda huku unashuhudia. Na Sisi mawifi tupunguzage kuingilia ndoa za kaka zetu, yetu yanatushinda kisa kushadadia ya kaka eeh.
 
Evelyn Salt

Hii nzuri hasa kwa wanawake wa ki leo..
Mimi tangu nimebalee dada yangu hajawai ingia gheto kwangu mpaka saivi najitegemea na alinisaidia kuhamisha vitu kipindi nahama hama lakini hakuwai kuingia chumbani kwangu.
Mazoe mengine ni Upumba*vu na ulofa
 
Last edited by a moderator:
Hahaa daaah umenikumbusha....mimi na kaka yangu ninayemfuata tangu tupo wadogo tunapendana kishenz...yan ni marafiki haswaaa...tukikaa pamoja full kutaniana, kupigana,kukimbizana yan full raha. Sasa juzi tu hapa hata kaja kututambulisha mkewe mtarajiwa. Bas my elder sista kaniambia nianze ku-maintain distance maana keshakuwa na wake sasa...yaan ni furaha iliyochanganyika na machungu
dada ako wa ukweli sana bonge la wifi kama mie vile teh
mipaka lazma dada uwe na yako mke awe na yake
 
hiyo ni kama mazoea, tumefanya hivyo tangu watoto... leo nijizuie kwa kuwa mke yupo karibu!!? kwanza unaanzia wapi kumuonea wivu dada wa damu wa mme wako kisa kulishana

Unapoamua kuoa mambo mengine ulozoea inabidi uyapunguze kama sio kuyaacha kabisa.ujue kwamba upo kwako na mkeo sio kwenu na mama, baba na nduguzo.
Fanya vile ungependa utendewe.ka bado hujamaliza mazoea (yale sio lazma) ambayo hayatakua na afya kwenye ndoa ni bora ukajipa mda zaidi kabla ya kuoa.
 
Huyo ni wifi au Mke mwenza? Siwezi kumruhusu dada yangu anizoee kiasi hicho, matumizi anipangie, mezani anilishe heh! Uzungu utakuwa umenishinda aisee.
Ila wakati mwingine, sisi wanaume ndio chanzo, kwa sababu mpaka dada kuingilia mambo yako ya ndani ni dalili kuwa kakuona zuzu kwa kiasi fulani na anajaribu kukuongoza.
 
Back
Top Bottom