Kinachoendelea Kampala University ni kama utapeli, matokeo ya Wanafunzi 300+ wa Udaktari yana utata, Serikali itusaidie Wanafunzi

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Chuo cha Kampala University hiki ambacho kipo Gongo la Mboto kina shida kubwa sana, najua wengi mnajua kimewahi kufungiwa siku za nyuma kutokana na magumashi mengi ambayo kimekuwa kikifanya.

Serikali iingilie kati kuangalia hiki chuo, sisi wanafunzi ambao tupo chuoni hapo tunapitia wakati mgumu.

Mfano sasa hivi wanafunzi wa Diploma ya Udaktari wa mwaka wa kwanza na mwaka wa pili matokeo yetu yote yameonesha ni incomplete wakati sisi tumeshafanya kila kitu, chuo kinatulazimisha tuendelee na mwaka wa tatu wakati wanatambua wazi kuwa kufanya hivyo lazima huko mbele ya safari tudunde.

Tumeshaenda hadi Wizara ya Afya ambao ndio wanaosimamia mitihani yetu, wao wanasema tatizo lipo upande wa chuo.

Wanachojua wao kuna vitu havijakamilika na kama tumeambiwa tulipe ada ya mwaka wa tatu wakati matokeo ni incomplete maana yake wanataka wale ada zetu huku wakitambua hakuna uwezekano wa Kwenda mbele.


============

SERIKALI YATOA UFAFANUZI YADAI CHUO KIMEFANYA UDANGANYIFU

Mkurugenzi wa Mafunzo kutoka Wizara Afya, Dk Saitore Laizer amesema:

“Hao wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wapili hawakufundishwa, chuo hakikuwafundisha, huwa tunakuwa na utaratibu wa kuhakiki wakati au baada ya mitihani.

“Baada ya mtihani tukabaini kuwa hao wanafunzi kuna masomo hawajafundishwa hata nusu ya syllabus, na chuo kimefanya udanganyifu mkubwa sana

Tusipokuwa makini tutauana huku duniani, kilifanyika kikao cha pande zote, chuo wakari makosa na kuandika barua jinsi ya kuziba hizo nafasi ili wanafunzi waweze kufundishwa vizuri ili mambo yao yaendelee.”

Kuhusu madai ya wanafunzi kusema kuwa wamekamilisha kila kitu na ndiyo maana wakaruhusiwa kufanya mitihani, Mkurugenzi anasema: “Hawakukamilisha, hapo wenye tatizo ni chuo.”

Kuhusu malalamiko ya wanafunzi kuwa wameshalipa ada na wanatakiwa kulipa tena amesema: “Hicho ni chuo binafsi, hatuingilii masuala ya ada. Hayo malalamiko yanaweza kwenda NACTE.”

Alipoulizwa kwa nini waliruhusu wanafunzi kufanya mitihani wakati wanatambua chuo hakikukamlisha taratibu ambazo zinatakiwa, anasema: “Udanganyifu kwenye mitihani unaweza kugundulika wakati wowote.”

“Tulichoamua ni lazima wanafunzi wafundishwe kile ambacho hawakufundishwa kisha watafanya mitihani tena, lakini hapohapo na sisi tutafanya uhakiki wetu kwa njia tunazozijua.”

Tukiwauliza nini kinachoendelea wanatuzungusha tun a kutupiga danadana, wanataka tulipe ada tu.

Serikali iingilie kati na kutusaidia, kuna mambo mengi hayapo sawa katika hiki chuo.

Kuna baadhi ya wanafunzi wameshakata tamaa ya kuendelea na masomo ukizingatia tunalipa ada kubwa, wengine tunatoka familia dun, hivi inakuwaje unafika mwisho wa masomo na hauwezi ku graduate, unamueleza nini yule ambaye amekuwa akikupa fedha ya ada

Kuna watu wanaishia kulia tu hatuna msaada.
 
Hiyo incomplete imesababishwa na nini, maana kama mme clear sioni logic ya kujaziwa incomplete.......jaribuni kuwaona TCU
 
Unaposema incomplete unamaanisha nini eleza kiundani
 
Ooops Mbona kama wewe ndo ujielewi mkuu [emoji848]
 
Unaposema incomplete unamaanisha nini eleza kiundani
Maana ya incomplete maana yake ni mwanafunzi hajakizi vigezo kufanya mtihan wa mwsho ila wanafunzi wamekizi vigezo na wamefanya mtihan wa mwisho ila matokeo ya wanafunzi wote yameletwa kama hayajakizi vigezo hakuna solution yeyote waliochukua isipokua kuwagawa katika makundi mawili
 
Ni vizuri kuwa makini wakati wa kuchagua Vyuo vya kusoma, maana Vyuo vingine kama hiko KIU hata waajiri wakiona tu Cheti chake wanatupa kwenye dustbin!!naongea kwa uzoefu kwa sehemu 3 tofauti nilizojitolea Idara ya HR
 
Unabisha au unachotaka kubisha nini ..mimi ndugu yangu ni muhanga wa hio kitu hadi chuoni nimefika sijapata majibu
Kuna tatizo ndugu, tena kubwa sana katika hicho chuo
 
Mnakwenda shule kuchezea? Mahudhurio yanakuwa aje hafifu hadi unakosa sifa ya kufanya mitihani? Mbio kulaumu chuo!
 
kwanini mliacha vyuo vyooote vilivyojaa mkaenda kusoma KAMPALA?
 
Hao wanafunzi ni takribian mia tano na wote wamelipa ada
Mnakwenda shule kuchezea? Mahudhurio yanakuwa aje hafifu hadi unakosa sifa ya kufanya mitihani? Mbio kulaumu chuo!
Hivi kwa akili timamu unaamini kua wanafuzi wote washindwe kutimiza mahuzurio hayo ni utetezi wao tu chuo hakuna ukwli hapo yani hakuna hata mwanafunzi mmja alietimiza mahuzurio ..na usipotimiza mahuzurio hutakiwi kukaa kwenye mtihan wala unakua sio eligible student sasa wanafunzi wote waliofanya mtihan wametimiza mahuzurio na waliokua hawajatimiza mahu
 
Sio kweli Academic register anachoongea coz three days before NACTE examination walifk kwa ajili ya kufanya verification kama wanafunzi wako verified kufanya exams or not, na baada ya apo watu wakawa selected kufanya mitihn although sio wote coz wengn waliambia wana incomplete kabla ya mtihn. Sasa issue ya attendance inatokea wap apo na kwann kama wameona mahudhurio ni sabb wakaamua kuturuhusu kufanya mtihn..!? Kampala you guys you are not serious..tunataka sababu ya incomplete and by the way hakuna mwanafunzi alofanya fujo ata mmoja coz namba za mtihn zenyew mlitupa usiku wa kuamkia day ya exams na fujo izo zimefanyika mda gn...Kampala tell the truth and be honest kwakwel
 
Kwa hili hapana AR coz watu all the time tupo chuo na tuna attend kwenye vipindi, huwez sema clinical medicine yote wanafunzi 200+ hakuna ata mwanafunzi mmoja alifikia 90% ya mahudhurio kwakwel hapna AR
 
Sio kweli Academic register anachoongea coz three days before NACTE examination walifk kwa ajili ya kufanya verification kama wanafunzi wako verified kufanya exams or not, na baada ya apo watu wakawa selected kufanya mitihn although sio wote coz wengn waliambia wana incomplete kabla ya mtihn. Sasa issue ya attendance inatokea wap apo na kwann kama wameona mahudhurio ni sabb wakaamua kuturuhusu kufanya mtihn..!? Kampala you guys you are not serious..tunataka sababu ya incomplete and by the way hakuna mwanafunzi alofanya fujo ata mmoja coz namba za mtihn zenyew mlitupa usiku wa kuamkia day ya exams na fujo izo zimefanyika mda gn...Kampala tell the truth and be honest kwakwel
 
Fact, haiwezkn kukaa kweny mtihn if you are not eligible kufanya mtihn...they tried their level best kujitoa kweny matatiz but seriously kampala wametuhalibia maisha yatu, time na pesa pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…