SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Shambulizi la kigaidi mji wa Macomia mwezi jana.
- Oparesheni ya SADC na jeshi la Rwanda.
- Interest ya Kagame katika vita za wengine.
Wa kwanza kufika hapa Msumbiji ni jeshi la Rwanda. Kwa makubaliano ya siri yalowekwa na raisi wa Msumbiji, Felipe Nyusi, na raisi wa Rwanda, Paul Kagame, polisi 300 na wanajeshi 700 wanaingia nchini kuanzia tarehe 9 July, 2021.
Kikosi hiki maalum kinaongozwa na jenerali Innocent Kabandana (pichani) kabla ya hapo baadae kuja kupandishwa cheo kuwa Lt. General kwa oparesheni kubwa yenye matunda hapa nchini Msumbiji.
Siku sita baadae, tarehe 15 July, ndo' kikosi cha SADC kinaingia hapa. Kikosi hiki kina jumla ya wanajeshi 2,200 wengi wao wakitokea Afrika Kusini ambapo ndo' pia anatokea kamanda wa kikosi hiki cha SADC, jenerali Xolani Mankayi. (pichani)
Kwa pamoja, makamanda hawa wawili, Innocent Kabandana (wa Rwanda) na Xolan Mankayi (wa SADC) wanashirikiana na kamanda mwenyeji, Cristovao Chume (pichani), kupanga misheni ya kupambana na magaidi wa Ansar al-sunna.
Jeshi la Rwanda linakabidhiwa mji wa Palma na Mocimboa de Praia na lile la SADC linapewa miji kama vile Nangende, Mueda na Muidumbe.
Kuanzia hapo, magaidi ya Ansar al-sunna yakaepuka kufanya mashambulizi makubwa kwenye miji mikubwa, badala yake wakawa wanashambulia kidogo na kukimbia (small hit-and-run raids), haswa vijiji vidogo visivyo na ulinzi ama kambi ndogo za jeshi zisizokuwa chini ya uangalizi.
Oktoba 2022, magaidi wanavamia maeneo mapya kabisa ambayo hayakuwahi kushambulia hapo kabla. Maeneo ya kusini mwa Cabo Delgado kama vile Namumo, Balama na Montepuez na sio tena kaskazini kama vile Palma na Mocimboa de Praia.
Baadae magaidi wanakuja na mkakati maalum. Wakiendelea kushambulia kule kusini, wanafanya tukio kubwa kaskazini kwa kuvuka mpaka wa Tanzania na kushambulia vijiji vya Kitaya na Michenjele kule Mtwara.
Wanaharibu, kuteka na kuua.
Lengo lao kugawa 'attention' ya vikosi hivi vipya ndani ya Msumbiji, vigawanyike kuzingatia kaskazini na pia kusini mwa Cabo ili wapate mwanya wa udhaifu kushambulia zaidi.
Bahati mbaya mpango huu hauzai matunda na mpaka kufikia ukomo wa mwaka 2022, oparesheni ya kuwadhibiti inafanikiwa kuwapunguza kwa idadi kubwa sana.
Ripoti ya UN Security Council inasema kati ya magaidi 2,500 mpaka 3,000 walipoteza maisha kwenye oparesheni hii.
Matokeo yake tunakuja kuuuona mwaka 2023 kama mwaka tulivu zaidi tofauti na miaka ya nyuma tangu pale 2017. Kwa sasa ni wastani wa matukio 11 kwa mwezi ukilinganisha na hapo 2022 kulipokuwa na wastani wa matukio 36 kwa mwezi.
Ndani ya mwaka huu (2023), Ansar al-sunna wanabadili mbinu na kuanza kutumia 'winning hearts and minds' strategy. Mbinu ya kushinda na kuvutia mapenzi ya watu kwa kutembelea jamii maeneo ya Macomia na Mocimboa ili kufanya nao biashara na kuwaambia wao si watu wabaya.
Hivyo mambo yanatulia kidogo.
Lakini kwenye kimya hiki, kinakuja kishindo kikubwa sasa kuanzia mwanzo wa mwaka 2024.
Mwaka unaanza kwa tabu.
Siku ya tarehe 21 January, magaidi wanashika kijiji cha Mucojo na kuweka sheria kali kwenye mavazi, haswa kwa wanawake, na wanapiga marufuku uuzwaji na unywaji wa pombe, lakini chini ya wiki mbili wanadhibitiwa na kuondoshwa.
Wiki moja mbele, tarehe 31, wanashambulia msafara wa wanajeshi na kusababisha vifo vya wanajeshi wawili.
February 9, wanashambulia eneo la Mazeze na kuchoma makanisa yaliyokuwa yanahifadhi watu.
Lakini kilele cha mwaka huu ni siku ile ya Ijumaa, tarehe 10 mwezi wa tano katika mji wa Macomia.
Siku hiyo, kwenye majira ya alfajiri, magari yalobebelea wanaume zaidi ya mia mbili wenye silaha za moto, yanavamia Macomia kupitia magharibi (Xinavane), kusini (Bangala) na mashariki (Nanga) ili kuwakuta wanajeshi wa Msumbiji katikati.
Swala la kufumba na kufumbua, mvua ya risasi inaanza kushuka kila kona.
Kujiokoa roho zao, watu wanakimbilia huko porini na mashambani.
Simu inaita upesi kwa jeshi la Rwanda pamoja na la SADC kuwa Macomia hali ni tete na unahitajika msaada wa haraka sana.
Magari yalobeba wanajeshi wa RDF na SADC yanatoka mji wa Pemba, mji mkuu wa jimbo la Cabo Delgado, na kuanza safari ya kwenda kuokoa jahazi huko Macomia.
Baada ya mapambano makali, mabwana wanazidiwa na kuondoka lakini baada ya dakika arobaini na kitu, wanarudi tena na mapambano yanazuka upya.
Ni mpaka tarehe 12 May, baada ya siku mbili, ndipo jeshi la Msumbiji na washirika wake wanafanikiwa kuurejesha mji wa Macomia mikononi.
Serikali ya Msumbiji, kwa ajenda wanayoijua wao wenyewe, wanaficha maswahibu yalotokea katika huu mji lakini shida huwezi kufumba macho na mdomo wa kila mtu.
Waliokuwapo wanasema waliona miili ya watu kuanzia kumi mpaka ishirini na tatu. Wanajeshi kadhaa waliuawa, maduka kadhaa yaliporwa na pia 'ambulance' moja ilibebwa.
Hivyo kwa hali hii, tofauti kidogo na hapo nyuma, hatuwezi tukasema hali ni shwari hapa jimboni Cabo Delgado.
Sasa kwenye nyakati hizi za mashaka, 'members' wa SADC, hususani Afrika ya Kusini, Botswana na Lesotho, zinaondoa majeshi yao hapa nchini Msumbiji.
Kama haitoshi, oparesheni yenyewe ya SADC inatarajiwa kufikia mwisho rasmi tarehe 15 July mwaka huu.
Just imagine.
Lakini ajabu upande wa pili, kwa wenzetu wa Rwanda, ambaye si hata mwanachama wa SADC, mambo ni kinyume kabisa na hawa wengine.
Kwanza jeshi hili, kwa namna ya pekee, limejichimbia kwenye mioyo ya wanamsumbiji, wanajeshi wake wanaaminika zaidi ya wenyeji wao linapokuja kwenye swala la uadilifu na ufanisi.
Mara kadhaa, wanajeshi wa Msumbiji wanaleta shida kwa wananchi. Wanafanya uonevu. Wanaiba. Wananchi wanaita wanajeshi wa Rwanda kuja kuwatetea na kweli wanaupata msaada.
(pichani wananchi wa Msumbiji wakiwa wamebebelea picha za Kagame na Nyusi)
Lakini pili, wakati wengine wanabeba mabegi kuondoka hapa nchini Msumbiji kama tulivyoona hapo juu, Rwanda ndo' kwanza anasogeza kiti chake apate kuketi vizuri.
Jenerali Karuretwa (pichani), kiongozi wa ushirikiano wa kijeshi kimataifa nchini Rwanda, anasema;
"Kuondoka kwa majeshi ya SADC nchini Msumbiji kunatufanya tuchukue hatua fulani ... tutawapa mafunzo wanajeshi wa Msumbiji ili kuyachukua maeneo yaliyoyoachwa na jeshi la SADC na pia tutaongeza idadi ya wanajeshi kucover maeneo zaidi."
Mbali na fungu la pesa linalotoka Umoja wa Ulaya (EU) kwenda kwa Rwanda, jenerali Karuretwa anasema kuguswa kwa Rwanda katika oparesheni za kutunza amani ni matokeo ya mauaji ya kimbari, mwaka 1994.
Kama watunza amani wa Umoja wa Mataifa wasingeliwatelekeza, basi wangelinusurika na kikombe kile cha mauaji, hivyo wanaujua umuhimu wa kuitunza amani.
Ikumbukwe mbali na Msumbiji, Rwanda wana jeshi lao kule jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) tangu walipopeleka kikosi chao cha kwanza Januari, 2014 baada ya makubaliano ya Kagame na Raisi Faustine Touadera.
Mpaka kufikia sasa wanajeshi wa Rwanda katika nchi hiyo ni zaidi ya alfu moja, wakiwa hapo kwa makubaliano rasmi ya kuisaidia nchi hii maskini barani Afrika kupambana na waasi wanaoitaka serikali kwa udi na uvumba.
Achilia mbali hapo, tarehe 15 April 2023, Raisi Kagame anafunga safari mpaka nchi ya Benin kukutana na Raisi Patrice Talon ambaye katika kikao anamuahidi kumpatia msaada wa jeshi kupambana na magaidi wanaotokea mipaka ya kaskazini.
Sasa yote haya Rwanda anayafanya kwa gharama ya kitu gani?
Ananufaika vipi na wanajeshi wake waliotapakaa Afrika kupambana na kifo uso kwa uso?
Bila ya shaka kuna mchezo Rwanda anaucheza na mchezo huo unamwingizia zaidi kuliko vile anavyopoteza. Na hii inamfanya autake mchezo zaidi na zaidi.
Kwenye mchezo huu, mbali na kocha mwenyewe bwana Kagame, kapteni si mwingine bali kampuni ya CRYSTAL VENTURES Ltd (CVL). Kampuni yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 500 za kimarekani.
Kampuni hii iliyoanzishwa 1995, ni mkono wa kuume wa chama tawala hapa Rwanda (RPF) na inashikilia karibia kila nyendo ya kiuchumi katika nchi hii kwa kupitia makampuni yake madogo madogo yanayosimama kama matawi.
Mkono wa kampuni hii unagusa kuanzia sekta ya kilimo, madini, ujenzi na hata ulinzi.
Kuanzia 2014, wawakilishi wa kampuni hii wanaambatana na serikali yao kwenda nchini Afrika ya kati, nchi ambayo Rwanda imepeleka wanajeshi wake kupambana na waasi, na tokea hapo wamekuwa wakifungamana na Afrika ya kati kwa makubaliano kadhaa.
Mojawapo ni lile la mwezi wa 9, 2021 ambapo tawi la CVL, Vogueroc, linaidhinishwa na serikali ya Afrika ya kati kufanya uvumbuzi wa migodi ya dhahabu na almasi nchini humo.
THERE'S NO FREE LUNCH.
Hata kule nchini Msumbiji mkondo ni huohuo.
Habari ni zilezile.
Mpaka muda huu unaposoma hapa, tayari makampuni matatu ya CVL; Macefield Ventures, NPD Ltd na Strofinare, yapo kwenye ardhi ya nchi hiyo kwa shughuli mbalimbali chini ya makubaliano ambayo wanayafahamu Felipe Nyusi na Kagame.
Taratibu, shughuli za ujenzi na ulinzi binafsi katika nchi hii, vinaanza kuhodhiwa na makampuni ya Rwanda.
Wataishia wapi na ingali wanazidi kujitanua hivi sasa wakiachwa peke yao na SADC?
Na nini hatma ya Ansar al-sunna mbele ya mabwana hawa wa Rwanda na sisi Tanzania tuliopakana nao?
Bila shaka tutalibakiza jeshi letu hapo Msumbiji, hata kama ni kwa gharama kubwa, lakini yatakayojiri huko mbeleni bado hatujajua.
Ngoja na tuone.
- Oparesheni ya SADC na jeshi la Rwanda.
- Interest ya Kagame katika vita za wengine.
Wa kwanza kufika hapa Msumbiji ni jeshi la Rwanda. Kwa makubaliano ya siri yalowekwa na raisi wa Msumbiji, Felipe Nyusi, na raisi wa Rwanda, Paul Kagame, polisi 300 na wanajeshi 700 wanaingia nchini kuanzia tarehe 9 July, 2021.
Kikosi hiki maalum kinaongozwa na jenerali Innocent Kabandana (pichani) kabla ya hapo baadae kuja kupandishwa cheo kuwa Lt. General kwa oparesheni kubwa yenye matunda hapa nchini Msumbiji.
Siku sita baadae, tarehe 15 July, ndo' kikosi cha SADC kinaingia hapa. Kikosi hiki kina jumla ya wanajeshi 2,200 wengi wao wakitokea Afrika Kusini ambapo ndo' pia anatokea kamanda wa kikosi hiki cha SADC, jenerali Xolani Mankayi. (pichani)
Kwa pamoja, makamanda hawa wawili, Innocent Kabandana (wa Rwanda) na Xolan Mankayi (wa SADC) wanashirikiana na kamanda mwenyeji, Cristovao Chume (pichani), kupanga misheni ya kupambana na magaidi wa Ansar al-sunna.
Jeshi la Rwanda linakabidhiwa mji wa Palma na Mocimboa de Praia na lile la SADC linapewa miji kama vile Nangende, Mueda na Muidumbe.
Kuanzia hapo, magaidi ya Ansar al-sunna yakaepuka kufanya mashambulizi makubwa kwenye miji mikubwa, badala yake wakawa wanashambulia kidogo na kukimbia (small hit-and-run raids), haswa vijiji vidogo visivyo na ulinzi ama kambi ndogo za jeshi zisizokuwa chini ya uangalizi.
Oktoba 2022, magaidi wanavamia maeneo mapya kabisa ambayo hayakuwahi kushambulia hapo kabla. Maeneo ya kusini mwa Cabo Delgado kama vile Namumo, Balama na Montepuez na sio tena kaskazini kama vile Palma na Mocimboa de Praia.
Baadae magaidi wanakuja na mkakati maalum. Wakiendelea kushambulia kule kusini, wanafanya tukio kubwa kaskazini kwa kuvuka mpaka wa Tanzania na kushambulia vijiji vya Kitaya na Michenjele kule Mtwara.
Wanaharibu, kuteka na kuua.
Lengo lao kugawa 'attention' ya vikosi hivi vipya ndani ya Msumbiji, vigawanyike kuzingatia kaskazini na pia kusini mwa Cabo ili wapate mwanya wa udhaifu kushambulia zaidi.
Bahati mbaya mpango huu hauzai matunda na mpaka kufikia ukomo wa mwaka 2022, oparesheni ya kuwadhibiti inafanikiwa kuwapunguza kwa idadi kubwa sana.
Ripoti ya UN Security Council inasema kati ya magaidi 2,500 mpaka 3,000 walipoteza maisha kwenye oparesheni hii.
Matokeo yake tunakuja kuuuona mwaka 2023 kama mwaka tulivu zaidi tofauti na miaka ya nyuma tangu pale 2017. Kwa sasa ni wastani wa matukio 11 kwa mwezi ukilinganisha na hapo 2022 kulipokuwa na wastani wa matukio 36 kwa mwezi.
Ndani ya mwaka huu (2023), Ansar al-sunna wanabadili mbinu na kuanza kutumia 'winning hearts and minds' strategy. Mbinu ya kushinda na kuvutia mapenzi ya watu kwa kutembelea jamii maeneo ya Macomia na Mocimboa ili kufanya nao biashara na kuwaambia wao si watu wabaya.
Hivyo mambo yanatulia kidogo.
Lakini kwenye kimya hiki, kinakuja kishindo kikubwa sasa kuanzia mwanzo wa mwaka 2024.
Mwaka unaanza kwa tabu.
Siku ya tarehe 21 January, magaidi wanashika kijiji cha Mucojo na kuweka sheria kali kwenye mavazi, haswa kwa wanawake, na wanapiga marufuku uuzwaji na unywaji wa pombe, lakini chini ya wiki mbili wanadhibitiwa na kuondoshwa.
Wiki moja mbele, tarehe 31, wanashambulia msafara wa wanajeshi na kusababisha vifo vya wanajeshi wawili.
February 9, wanashambulia eneo la Mazeze na kuchoma makanisa yaliyokuwa yanahifadhi watu.
Lakini kilele cha mwaka huu ni siku ile ya Ijumaa, tarehe 10 mwezi wa tano katika mji wa Macomia.
Siku hiyo, kwenye majira ya alfajiri, magari yalobebelea wanaume zaidi ya mia mbili wenye silaha za moto, yanavamia Macomia kupitia magharibi (Xinavane), kusini (Bangala) na mashariki (Nanga) ili kuwakuta wanajeshi wa Msumbiji katikati.
Swala la kufumba na kufumbua, mvua ya risasi inaanza kushuka kila kona.
Kujiokoa roho zao, watu wanakimbilia huko porini na mashambani.
Simu inaita upesi kwa jeshi la Rwanda pamoja na la SADC kuwa Macomia hali ni tete na unahitajika msaada wa haraka sana.
Magari yalobeba wanajeshi wa RDF na SADC yanatoka mji wa Pemba, mji mkuu wa jimbo la Cabo Delgado, na kuanza safari ya kwenda kuokoa jahazi huko Macomia.
Baada ya mapambano makali, mabwana wanazidiwa na kuondoka lakini baada ya dakika arobaini na kitu, wanarudi tena na mapambano yanazuka upya.
Ni mpaka tarehe 12 May, baada ya siku mbili, ndipo jeshi la Msumbiji na washirika wake wanafanikiwa kuurejesha mji wa Macomia mikononi.
Serikali ya Msumbiji, kwa ajenda wanayoijua wao wenyewe, wanaficha maswahibu yalotokea katika huu mji lakini shida huwezi kufumba macho na mdomo wa kila mtu.
Waliokuwapo wanasema waliona miili ya watu kuanzia kumi mpaka ishirini na tatu. Wanajeshi kadhaa waliuawa, maduka kadhaa yaliporwa na pia 'ambulance' moja ilibebwa.
Hivyo kwa hali hii, tofauti kidogo na hapo nyuma, hatuwezi tukasema hali ni shwari hapa jimboni Cabo Delgado.
Sasa kwenye nyakati hizi za mashaka, 'members' wa SADC, hususani Afrika ya Kusini, Botswana na Lesotho, zinaondoa majeshi yao hapa nchini Msumbiji.
Kama haitoshi, oparesheni yenyewe ya SADC inatarajiwa kufikia mwisho rasmi tarehe 15 July mwaka huu.
Just imagine.
Lakini ajabu upande wa pili, kwa wenzetu wa Rwanda, ambaye si hata mwanachama wa SADC, mambo ni kinyume kabisa na hawa wengine.
Kwanza jeshi hili, kwa namna ya pekee, limejichimbia kwenye mioyo ya wanamsumbiji, wanajeshi wake wanaaminika zaidi ya wenyeji wao linapokuja kwenye swala la uadilifu na ufanisi.
Mara kadhaa, wanajeshi wa Msumbiji wanaleta shida kwa wananchi. Wanafanya uonevu. Wanaiba. Wananchi wanaita wanajeshi wa Rwanda kuja kuwatetea na kweli wanaupata msaada.
(pichani wananchi wa Msumbiji wakiwa wamebebelea picha za Kagame na Nyusi)
Lakini pili, wakati wengine wanabeba mabegi kuondoka hapa nchini Msumbiji kama tulivyoona hapo juu, Rwanda ndo' kwanza anasogeza kiti chake apate kuketi vizuri.
Jenerali Karuretwa (pichani), kiongozi wa ushirikiano wa kijeshi kimataifa nchini Rwanda, anasema;
"Kuondoka kwa majeshi ya SADC nchini Msumbiji kunatufanya tuchukue hatua fulani ... tutawapa mafunzo wanajeshi wa Msumbiji ili kuyachukua maeneo yaliyoyoachwa na jeshi la SADC na pia tutaongeza idadi ya wanajeshi kucover maeneo zaidi."
Mbali na fungu la pesa linalotoka Umoja wa Ulaya (EU) kwenda kwa Rwanda, jenerali Karuretwa anasema kuguswa kwa Rwanda katika oparesheni za kutunza amani ni matokeo ya mauaji ya kimbari, mwaka 1994.
Kama watunza amani wa Umoja wa Mataifa wasingeliwatelekeza, basi wangelinusurika na kikombe kile cha mauaji, hivyo wanaujua umuhimu wa kuitunza amani.
Ikumbukwe mbali na Msumbiji, Rwanda wana jeshi lao kule jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) tangu walipopeleka kikosi chao cha kwanza Januari, 2014 baada ya makubaliano ya Kagame na Raisi Faustine Touadera.
Mpaka kufikia sasa wanajeshi wa Rwanda katika nchi hiyo ni zaidi ya alfu moja, wakiwa hapo kwa makubaliano rasmi ya kuisaidia nchi hii maskini barani Afrika kupambana na waasi wanaoitaka serikali kwa udi na uvumba.
Achilia mbali hapo, tarehe 15 April 2023, Raisi Kagame anafunga safari mpaka nchi ya Benin kukutana na Raisi Patrice Talon ambaye katika kikao anamuahidi kumpatia msaada wa jeshi kupambana na magaidi wanaotokea mipaka ya kaskazini.
Sasa yote haya Rwanda anayafanya kwa gharama ya kitu gani?
Ananufaika vipi na wanajeshi wake waliotapakaa Afrika kupambana na kifo uso kwa uso?
Bila ya shaka kuna mchezo Rwanda anaucheza na mchezo huo unamwingizia zaidi kuliko vile anavyopoteza. Na hii inamfanya autake mchezo zaidi na zaidi.
Kwenye mchezo huu, mbali na kocha mwenyewe bwana Kagame, kapteni si mwingine bali kampuni ya CRYSTAL VENTURES Ltd (CVL). Kampuni yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 500 za kimarekani.
Kampuni hii iliyoanzishwa 1995, ni mkono wa kuume wa chama tawala hapa Rwanda (RPF) na inashikilia karibia kila nyendo ya kiuchumi katika nchi hii kwa kupitia makampuni yake madogo madogo yanayosimama kama matawi.
Mkono wa kampuni hii unagusa kuanzia sekta ya kilimo, madini, ujenzi na hata ulinzi.
Kuanzia 2014, wawakilishi wa kampuni hii wanaambatana na serikali yao kwenda nchini Afrika ya kati, nchi ambayo Rwanda imepeleka wanajeshi wake kupambana na waasi, na tokea hapo wamekuwa wakifungamana na Afrika ya kati kwa makubaliano kadhaa.
Mojawapo ni lile la mwezi wa 9, 2021 ambapo tawi la CVL, Vogueroc, linaidhinishwa na serikali ya Afrika ya kati kufanya uvumbuzi wa migodi ya dhahabu na almasi nchini humo.
THERE'S NO FREE LUNCH.
Hata kule nchini Msumbiji mkondo ni huohuo.
Habari ni zilezile.
Mpaka muda huu unaposoma hapa, tayari makampuni matatu ya CVL; Macefield Ventures, NPD Ltd na Strofinare, yapo kwenye ardhi ya nchi hiyo kwa shughuli mbalimbali chini ya makubaliano ambayo wanayafahamu Felipe Nyusi na Kagame.
Taratibu, shughuli za ujenzi na ulinzi binafsi katika nchi hii, vinaanza kuhodhiwa na makampuni ya Rwanda.
Wataishia wapi na ingali wanazidi kujitanua hivi sasa wakiachwa peke yao na SADC?
Na nini hatma ya Ansar al-sunna mbele ya mabwana hawa wa Rwanda na sisi Tanzania tuliopakana nao?
Bila shaka tutalibakiza jeshi letu hapo Msumbiji, hata kama ni kwa gharama kubwa, lakini yatakayojiri huko mbeleni bado hatujajua.
Ngoja na tuone.