Kinachoigharimu Simba ni kupoteza focus katika nyakati muhimu

Kinachoigharimu Simba ni kupoteza focus katika nyakati muhimu

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Simba imefanya usajili mzuri sana msimu huu na imepambana sana katika mashindano yote ambayo imeshiriki mpaka sasa.

Mechi zote ambazo Simba imepoteza msimu huu au kutoka sare ni kwa sababu ya makosa ambayo chanzo chake kikuu ni kupoteza focus au umakini. Hii inaonyesha timu ni imara sana ila inahitaji kuliangalia hilo maana kila siku linaigharimu timu.

Mechi na Yanga, kupoteza focus kuliifanya ipoteze mechi ambayo ingeweza kabisa kuisha sare. Mechi na Coastal, Fountain Gate, kule CAF mechi ya kwanza dhidi ya Costantine wote mnajua nini kilitokea katika mechi hizi, kupoteza umakini.

Nitagusia matukio matatu ya nje ya uwanja yaliyotokea hivi karibuni ambayo kwa mtazamo wangu nilijua tu yanaenda kuigharimu Simba kwa njia moja ama nyingine. Matukio yote haya naweza kuyaingiza katika tatizo kuu la kupoteza umakini wa nini timu inahitaji na uzito wa jambo lililo mbele.

Soma Pia: FT | Simba SC 2-2 Azam FC | NBC Premier League | Benjamin Mkapa | 24 Februari, 2025

1. Kauli ya Ahmed Ally kuwaita Azam inzi wa chooni. Kwa nini umpe mpinzani hasira ya kupambana dhidi yako? Hii kauli ilinishangaza sana kutolewa kipindi hiki. Focus!

2. Video ya wachezaji wa Simba wakiongozwa na captain Zimbwe kuingia mazoezini jana huku wanacheza muziki. Hakukuwa na umuhimu wa kufanya kitendo hadharani kipindi hiki. Kufanya kitendo kile kuelekea mechi ngumu kama ya leo kinaleta picha ya kwamba wachezaji wameridhika, kwamba wamemaliza na inaonyesha dharau kwa mpinzani wako. Hiki ni kipindi cha kukaa kimya na kumkimbiza mwizi kimya kimya. Focus!

3. Kitendo cha kuruhusu wachezaji waende kwenye harusi ya Aziz Ki. Nilimuona Chamou kwenye harusi ya Aziz Ki, sina uhakika wachezaji gani wengine walikuwepo. Ni jambo la kushangaza kuona Chamou alikosa mechi ya Namungo kisa harusi ya Aziz Ki. Ile mechi, Che Malone angeumia kama alivyoumia leo, Simba haikuwa na mbadala wake kwenye benchi. Hili jambo lilinifikirisha sana, nikajiuliza maswali mengi. Yaani mpinzani wako kaamua kufanya upuuzi katikati ya msimu na wewe unajiunga katika upuuzi wake? Nafikiri kuna hali ya kutotambua uzito wa upinzani wa Yanga wa ndani na nje ya uwanja katika mapambano haya ya ubingwa.

Pamoja na kwamba msimu huu Simba inajenga timu ila ikikosa ubingwa ijilaumu tu yenyewe. Yanga hapo kati walivurugana sana. Ilihitaji tu kukeep focus ndani na nje ya uwanja baasi.

Nafasi ya Simba kuchukua ubingwa bado ipo ingawa kwa makosa haya imekuwa ngumu zaidi. Kilichobaki ni kuhakikisha inashinda mechi zote zilizobaki ikiwemo derby.
 
Huwezi kuwa bingwa beki akiwa shabalala miaka 39

Huwezi kuwa bingwa kiungo mkabaji akiwa Ngoma miaka 41 na sio mzuri kwenye kukaba

Huwezi kuwa bingwa striker wako akiwa Ateba, ana kg 117, tuheshimu football ⚽

Huwezi kuwa bingwa beki akiwa Che Malon, akitiwa pressure ya Max, Aziz ki, Mzize na Pacome laZima ataachoa goli 6

Huwezi kuwa bingwa namba 10 akiwa Ahoua, nzito mno, kufunga Kwa penalty, watu wana Pacome, Aziz ki, max na Chama

Huwezi kuwa bingwa Kwa kutegemea penalties na red card ♦️ zitokee

Kuhusu Valentine Nouma kuhudhiria harusi ya Aziz ki
Hawa wote wanatoka Burkina Faso, kwenda kum support mwenzake kwenye japo kubwa kama ndoa sio vibaya
 
Huwezi kuwa bingwa beki akiwa shabalala miaka 39

Huwezi kuwa bingwa kiungo mkabaji akiwa Ngoma miaka 41 na sio mzuri kwenye kukaba

Huwezi kuwa bingwa striker wako akiwa Ateba, ana kg 117, tuheshimu football ⚽

Huwezi kuwa bingwa beki akiwa Che Malon, akitiwa pressure ya Max, Aziz ki, Mzize na Pacome laZima ataachoa goli 6

Huwezi kuwa bingwa namba 10 akiwa Ahoua, nzito mno, kufunga Kwa penalty, watu wana Pacome, Aziz ki, max na Chama

Huwezi kuwa bingwa Kwa kutegemea penalties na red card ♦️ zitokee

Kuhusu Valentine Nouma kuhudhiria harusi ya Aziz ki
Hawa wote wanatoka Burkina Faso, kwenda kum support mwenzake kwenye japo kubwa kama ndoa sio vibaya
Ukifanya harusi unashauriana na nduguzo ili ratiba ya harusi iendane na ratiba zao, kama kuna wa kusafiri wajipange, nk. Ni wazi Aziz Ki hakuzingatia ratiba za hao kina Chamou na wenzie au hawana umuhimu huo kwake unaotaka kuwapa.

Nilisema mwanzoni mwa msimu, ili Simba imfunge Yanga na iweze kupambania ubingwa inabidi urafiki wa wachezaji upigwe stop mpaka mwishoni mwa msimu. Kilichofanyika kimeonyesha udhaifu mkubwa sana wa kiuongozi. Yaani unaweka rehani mechi yako kisa kuhudhuria upuuzi wa mpinzani wako?

Hayo mengine sitayajibu.
 
Simba imefanya usajili mzuri sana msimu huu na imepambana sana katika mashindano yote ambayo imeshiriki mpaka sasa.

Mechi zote ambazo Simba imepoteza msimu huu au kutoka sare ni kwa sababu ya makosa ambayo chanzo chake kikuu ni kupoteza focus au umakini. Hii inaonyesha timu ni imara sana ila inahitaji kuliangalia hilo maana kila siku linaigharimu timu.

Mechi na Yanga, kupoteza focus kuliifanya ipoteze mechi ambayo ingeweza kabisa kuisha sare. Mechi na Coastal, Kengold, kule CAF mechi ya kwanza dhidi ya Costantine wote mnajua nini kilitokea katika mechi hizi, kupoteza umakini.

Nitagusia matukio matatu ya nje ya uwanja yaliyotokea hivi karibuni ambayo kwa mtazamo wangu nilijua tu yanaenda kuigharimu Simba kwa njia moja ama nyingine. Matukio yote haya naweza kuyaingiza katika tatizo kuu la kupoteza umakini wa nini timu inahitaji na uzito wa jambo lililo mbele.

Soma Pia: FT | Simba SC 2-2 Azam FC | NBC Premier League | Benjamin Mkapa | 24 Februari, 2025

1. Kauli ya Ahmed Ally kuwaita Azam inzi wa chooni. Kwa nini umpe mpinzani hasira ya kupambana dhidi yako? Hii kauli ilinishangaza sana kutolewa kipindi hiki. Focus!

2. Video ya wachezaji wa Simba wakiongozwa na captain Zimbwe kuingia mazoezini jana huku wanacheza muziki. Hakukuwa na umuhimu wa kufanya kitendo hadharani kipindi hiki. Kufanya kitendo kile kuelekea mechi ngumu kama ya leo kinaleta picha ya kwamba wachezaji wameridhika, kwamba wamemaliza na inaonyesha dharau kwa mpinzani wako. Hiki ni kipindi cha kukaa kimya na kumkimbiza mwizi kimya kimya. Focus!

3. Kitendo cha kuruhusu wachezaji waende kwenye harusi ya Aziz Ki. Nilimuona Chamou kwenye harusi ya Aziz Ki, sina uhakika wachezaji gani wengine walikuwepo. Ni jambo la kushangaza kuona Chamou alikosa mechi ya Namungo kisa harusi ya Aziz Ki. Ile mechi, Che Malone angeumia kama alivyoumia leo, Simba haikuwa na mbadala wake kwenye benchi. Hili jambo lilinifikirisha sana, nikajiuliza maswali mengi. Yaani mpinzani wako kaamua kufanya upuuzi katikati ya msimu na wewe unajiunga katika upuuzi wake? Nafikiri kuna hali ya kutotambua uzito wa upinzani wa Yanga wa ndani na nje ya uwanja katika mapambano haya ya ubingwa.

Pamoja na kwamba msimu huu Simba inajenga timu ila ikikosa ubingwa ijilaumu tu yenyewe. Yanga hapo kati walivurugana sana. Ilihitaji tu kukeep focus ndani na nje ya uwanja baasi.

Nafasi ya Simba kuchukua ubingwa bado ipo ingawa kwa makosa haya imekuwa ngumu zaidi. Kilichobaki ni kuhakikisha inashinda mechi zote zilizobaki ikiwemo derby.
Mnakula mpira.? Wabongo siwaewi kabisa
 
Ukifanya harusi unashauriana na nduguzo ili ratiba ya harusi iendane na ratiba zao, kama kuna wa kusafiri wajipange, nk. Ni wazi Aziz Ki hakuzingatia ratiba za hao kina Chamou na wenzie au hawana umuhimu huo kwake unaotaka kuwapa.

Nilisema mwanzoni mwa msimu, ili Simba imfunge Yanga na iweze kupambania ubingwa inabidi urafiki wa wachezaji upigwe stop mpaka mwishoni mwa msimu. Kilichofanyika kimeonyesha udhaifu mkubwa sana wa kiuongozi. Yaani unaweka rehani mechi yako kisa kuhudhuria upuuzi wa mpinzani wako?

Hayo mengine sitayajibu.
We unajionyesha jinsi Gani unaichukulia mpira kama uadui
Kwa mchezaji mpira ni kazi tu
Ipo siku Nouma anaweza kucheza na Aziz ki iwe Simba , Yanga au popote na wanatoka Taifa Moja,
Mtu laZima uhudhurie jambo la mwenzako kumpa support
Kwaiyo wewe ukifanya kazi NMB hutao
Msalimia mfanyakazi wa CRDB
 
Mkuu umeongea vilevile kama ambavyo nimetoka kuongea na wanangu mtaani.

Ni ni ukweli usiopingika kuwa weakness ya Simba ipo kwenye kilele cha furaha ya kuishika mechi.

Simba akiwa anaongoza ndio moment ambayo unaweza kushuhudia makosa mengi kuliko kipindi ambacho ametanguliwa na anasaka bao la kusawazisha.

Hii kitu imetugharimu sana na tukiiruhusu ikue basi itaenda kujijenga na kufanya kuwa sehemu ya utamaduni wetu.

Niishie hapa maana mengi niliyotaka kuyasema zaidi umeyaelezea.
 
Mkuu umeongea vilevile kama ambavyo nimetoka kuongea na wanangu mtaani.

Ni ni ukweli usiopingika kuwa weakness ya Simba ipo kwenye kilele cha furaha ya kuishika mechi.

Simba akiwa anaongoza ndio moment ambayo unaweza kushuhudia makosa mengi kuliko kipindi ambacho ametanguliwa na anasaka bao la kusawazisha.

Hii kitu imetugharimu sana na tukiiruhusu ikue basi itaenda kujijenga na kufanya kuwa sehemu ya utamaduni wetu.

Niishie hapa maana mengi niliyotaka kuyasema zaidi umeyaelezea.
Sawa tumekuelews
 
Mkuu umeongea vilevile kama ambavyo nimetoka kuongea na wanangu mtaani.

Ni ni ukweli usiopingika kuwa weakness ya Simba ipo kwenye kilele cha furaha ya kuishika mechi.

Simba akiwa anaongoza ndio moment ambayo unaweza kushuhudia makosa mengi kuliko kipindi ambacho ametanguliwa na anasaka bao la kusawazisha.

Hii kitu imetugharimu sana na tukiiruhusu ikue basi itaenda kujijenga na kufanya kuwa sehemu ya utamaduni wetu.

Niishie hapa maana mengi niliyotaka kuyasema zaidi umeyaelezea.
Hizo back passes ndio mchawi wa Simba
 
Huwezi kuwa bingwa beki akiwa shabalala miaka 39

Huwezi kuwa bingwa kiungo mkabaji akiwa Ngoma miaka 41 na sio mzuri kwenye kukaba

Huwezi kuwa bingwa striker wako akiwa Ateba, ana kg 117, tuheshimu football ⚽

Huwezi kuwa bingwa beki akiwa Che Malon, akitiwa pressure ya Max, Aziz ki, Mzize na Pacome laZima ataachoa goli 6

Huwezi kuwa bingwa namba 10 akiwa Ahoua, nzito mno, kufunga Kwa penalty, watu wana Pacome, Aziz ki, max na Chama

Huwezi kuwa bingwa Kwa kutegemea penalties na red card ♦️ zitokee

Kuhusu Valentine Nouma kuhudhiria harusi ya Aziz ki
Hawa wote wanatoka Burkina Faso, kwenda kum support mwenzake kwenye japo kubwa kama ndoa sio vibaya
Liateba leo liliomba penalti 1 hiyo hadi nikacheka 😀😀
 
Huwezi kuwa bingwa beki akiwa shabalala miaka 39

Huwezi kuwa bingwa kiungo mkabaji akiwa Ngoma miaka 41 na sio mzuri kwenye kukaba

Huwezi kuwa bingwa striker wako akiwa Ateba, ana kg 117, tuheshimu football ⚽

Huwezi kuwa bingwa beki akiwa Che Malon, akitiwa pressure ya Max, Aziz ki, Mzize na Pacome laZima ataachoa goli 6

Huwezi kuwa bingwa namba 10 akiwa Ahoua, nzito mno, kufunga Kwa penalty, watu wana Pacome, Aziz ki, max na Chama

Huwezi kuwa bingwa Kwa kutegemea penalties na red card ♦️ zitokee

Kuhusu Valentine Nouma kuhudhiria harusi ya Aziz ki
Hawa wote wanatoka Burkina Faso, kwenda kum support mwenzake kwenye japo kubwa kama ndoa sio vibaya
NGOMA SIO KIUNGO MKABAJI NI KIUNGO NO 8, KIUNGO MKABAJI NI YUSUPH KAGOMA.
 

Attachments

  • FB_IMG_17404367409773926.jpg
    FB_IMG_17404367409773926.jpg
    369.4 KB · Views: 1
Mkuu umeongea vilevile kama ambavyo nimetoka kuongea na wanangu mtaani.

Ni ni ukweli usiopingika kuwa weakness ya Simba ipo kwenye kilele cha furaha ya kuishika mechi.

Simba akiwa anaongoza ndio moment ambayo unaweza kushuhudia makosa mengi kuliko kipindi ambacho ametanguliwa na anasaka bao la kusawazisha.

Hii kitu imetugharimu sana na tukiiruhusu ikue basi itaenda kujijenga na kufanya kuwa sehemu ya utamaduni wetu.

Niishie hapa maana mengi niliyotaka kuyasema zaidi umeyaelezea.
Kuna mambo ya kurekebisha kwenye mechi za simba
1.Kuridhika pale wanapoongoza hata kwa goli 1
2.Kukata punzi dk za jioni kipindi cha pili
3.Kocha awe anaanza hata na baadhi ya wachezaji wa kawaida ili wanaoingia waje kuleta mabadiliko zaidi .
4. Substitution iwe kwa mda unaofaa siyo dk zinaisha na goli limesawazishwa halafu anaanza kukurupuka.
 
Huwezi kuwa bingwa beki akiwa shabalala miaka 39

Huwezi kuwa bingwa kiungo mkabaji akiwa Ngoma miaka 41 na sio mzuri kwenye kukaba

Huwezi kuwa bingwa striker wako akiwa Ateba, ana kg 117, tuheshimu football ⚽

Huwezi kuwa bingwa beki akiwa Che Malon, akitiwa pressure ya Max, Aziz ki, Mzize na Pacome laZima ataachoa goli 6

Huwezi kuwa bingwa namba 10 akiwa Ahoua, nzito mno, kufunga Kwa penalty, watu wana Pacome, Aziz ki, max na Chama

Huwezi kuwa bingwa Kwa kutegemea penalties na red card ♦️ zitokee

Kuhusu Valentine Nouma kuhudhiria harusi ya Aziz ki
Hawa wote wanatoka Burkina Faso, kwenda kum support mwenzake kwenye japo kubwa kama ndoa sio vibaya
Waafrika Magharibi wanasapotiana sana popote pale duniani.
 
SIKU NINAANDIKA HAPA, SIMBA INAPASWA KUFANYA SAJILI ZA MABORESHO ZISIZOPUNGUA TANO.

TIMU BADO SANA KUFIKA WALAU NUSU WA ILE YA 2019.

WAACHANE NA.
1. Joshua Mutale.
2. Karabue Chamoe.
3 .Agustine Okejepha.
4. Dese Mukwala.
5. (Ngoma).
6 Manula.

MABORESHO YA SAJILI.
Beki wa kati NO 5.
Kiungo mkabaji No 6.
Kiungo mshambuliaji 10.
Mshambuliaji No 9.

Hadi leo sijapata majibu kwanini Fadru alisajili mchezaji mmoja tu Dirisha Dogo, ilinishangaza sana!!!!!!!!

Au ndio kuvizia ma Free Agent.

NIMEMALIZA
 
SIKU NINAANDIKA HAPA, SIMBA INAPASWA KUFANYA SAJILI ZA MABORESHO ZISIZOPUNGUA TANO.

TIMU BADO SANA KUFIKA WALAU NUSU WA ILE YA 2019.

WAACHANE NA.
1. Joshua Mutale.
2. Karabue Chamoe.
3 .Agustine Okejepha.
4. Dese Mukwala.
5. (Ngoma).
6 Manula.

MABORESHO YA SAJILI.
Beki wa kati NO 5.
Kiungo mkabaji No 6.
Kiungo mshambuliaji 10.
Mshambuliaji No 9.

Hadi leo sijapata majibu kwanini Fadru alisajili mchezaji mmoja tu Dirisha Dogo, ilinishangaza sana!!!!!!!!

Au ndio kuvizia ma Free Agent.

NIMEMALIZA
bado huwa hamtaki Simba iachane na kina Shabalala na Kapombe...weakness kubwa kwa Simba ipo kupitia beki zake za kushoto na kulia. Shabalala na Kapombe wameshazeeka sasa hawawezi kucheza katika hali za ushindani wa kiwango cha juu. Iangalie Simba inavyotaabika inapokutana na timu yenye mawinga wazuri wenye kasi.

Shabalala ni mbovu kupiga crosses, mbovu kutoa pasi na mara nyingi haonekani wakati timu inaposhambulia na hata kushambuliwa pia. Leo alikuwa anasababisha kina Che malone na baadae Chamouh watoke katika nafasi zao waje kumkabia yeye nafasi yake, kitendo ambacho ni hatari sana.
 
1. Gibril Silla ndio winga mgumu zaidi kumkaba ligi kuu kuliko winga yoyote mabeki wote wanalijua hili.

2. Shabalala alikuwa anacheza Beki wa kushoto yaani no .
Kwa mbinu za kisasa kabisa Mtu anayewajibika kumsaidia beki wake ni kiungo mkabaji 6,8.

3 .Shabalala 3 hawezi kusaidiwa na Beki No 5 Never Ever narudia.
SHABALALA BEKI NO 3 HAWEZI KUSAIDIWA NA BEKI NO 5
BEKI ANAYEWEZA KUMSAIDIA ZIMBWE NI BEKI NO 4 AMBAYE NI HAMZA. Ambaye huwa anakuwa upande wa kushoto.
angalia mpira ki Ufundi na sio ki shabiki maandazi.

Shabalala kufichiwi makosa na Beki No 5 ni Uongo Mtakatifu
Uongo Pr max
Uongo wa hali ya Juu.
 
Back
Top Bottom