Kinachotokea kwa Mkude ni kuishi kimazoea

Albinoomweusi

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2016
Posts
3,433
Reaction score
8,585

"Sir Alex Ferguson kwenye Kanuni zake 9 kuhusu Nidhamu naomba nimnukuu kanuni namba 4, "Never ever, cede control" usikubali kupoteza Mamlaka yako mbele ya wachezaji"

"Kupitia hii Roy Keane alipokosoa wenzake mbele ya Media basi Fergie alivunja mkataba wake, Van Nisterloy na kipaji chake alipokosoa mamlaka akauzwa Real Madrid, hii ina maana hakuna mkubwa kuliko timu"

"Kinachotokea kwa Mkude ni kuishi kimazoea, yakajenga tabia, tabia ni kovu halifutiki kwa sabuni, Simba haipo kule alipozoea, wameset standards, asipobadilika atapata wakati mgumu sana, abadilike"

"Bila mkazo kwenye nidhamu, ipo siku Wachezaji watakupangia muda wa mazoezi, watakupangia aina ya mazoezi na watakupangia kikosi, lazima Sheria zifuatwe, hakuna mkubwa kuliko Taasisi"

Maneno ya Farhan Kihamu @jr_farhanjr kwenye SPORTS ROUND UP ya @cloudsfmtz
 
Mpira wa enzi za Ferguson siyo wa leo.

Sasa hivi wachezaji ni Institutions Kamili.
 
Mkude asilete kiburi Sasa hivi Simba Kuna wachezaji kibao ,Kama ameichoka Simba aondoke hata sisi tumeashaanza kumchoka kwa vitimbwi vyake
 
Aende popote yule mlevi Lwanga anatosha, nidhamu kwake limekuwa suala gumu sana.
 
Wamuachia afrahie penz na mkewe
Barbara waache kumsumbua Simba hamuwez Acha kuingilia mahusiano ya wachezaji wenu kila wakat
 
GSM ndiyo wanamvimbisha kichwa Mkude. Aende tu huko Yanga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…