Kinachotushinda Wabantu kuchora na kupanga miji ni nini?

Kinachotushinda Wabantu kuchora na kupanga miji ni nini?

Tuachane na suala la mpango mji, nyanja ipi ya kimaendeleo ambayo tunaimudu kwa ufanisi?

Kama kila sehemu ni utumbo tu kwanini tutarajie hapo kwenye mipango miji kutakua na afadhari?

Jibu la swali lako ni rushwa na nafasi kushikiliwa na watendaji wasiokua na uwezo
 
Tuachane na suala la mpango mji, nyanja ipi ya kimaendeleo ambayo tunaimudu kwa ufanisi?

Kama kila sehemu ni utumbo tu kwanini tutarajie hapo kwenye mipango miji kutakua na afadhari?

Jibu ni kwamba nafasi zinashikiliwa na watendaji wasiokua na uwezo
Swali. Wewe kama baba/mama mwenye nyumba, watoto wako watajipangia ramani ya Kiwanja cha familia yako hovyo hovyo, ukawachekea na kuwaacha tu ?
 
Ajabu ni kwamba Maafisa mipango miji wapo humuhumu na pengine wamechangi HII MADA
 
Sio kuchora na kupanga tu, bali hata kuheshimu kile tulichokipanga na kukichora tunashindwa

Wee angalia Sinza zilivyomegwa open space na uchafu wa misururu ya vibanda unavyoendekezwa

One of the former PM akiwa bado kazini unakuta nyumbani kwake ana mabanda ya ng'ombe ktk eneo ambalo ni makazi ya Viongozi wa juu

Ukiangalia background yake yeye na ng'ombe walikuwa kama part and parcel of the family

Kwa hiyo kuna vitu mpaka vitoke kwenye mabongo yetu itachukua Karne kadhaa
 
Tuachane na suala la mpango mji, nyanja ipi ya kimaendeleo ambayo tunaimudu kwa ufanisi?

Kama kila sehemu ni utumbo tu kwanini tutarajie hapo kwenye mipango miji kutakua na afadhari?

Jibu la swali lako ni rushwa na nafasi kushikiliwa na watendaji wasiokua na uwezo
Tunamudu kuwadhibiti Chadema na kutukuza viongozi...
 
Huruma na mipango ya mhe William Mkapa,.kuleta sera ya uboreshaji ardhi na makazi naona iliharibu sana. Watu walipojua ukivamia eneo unaboreshewa kukaa hapo hapo,, sasa nchi ni kama vichuguu vinavyoota hovyo, hovyo. Hakuna maeneo ya kupumzika/bustani kama mnazi mmoja Dsm. Mswahili mapumziko yetu ni vilabu vya pombe, vijiwe vya draft na vibanda vya Simba na Yanga.
Uko sahihi kabisa, ule mpango wa MKURABITA haukuwa suluhisho
 
Kizazi Cha elfu 2000 na watu Fulani wa 90s wanaweza wakafanya kitu (Pakitokea mabadiliko ya kwlikweli)

Maana ni aibu mpaka watu waelfu wasiweze kufanya angalau ata kitu kama kupanga mji kwenye zama hizi tunazoona mataifa mengine wanavyokuwa makini juu ya vitu mbalimbali,

Japo Kuna watu wanapenda sana kuleta dharau juu ya wengine.(Kizazi Cha elfu 2000 kitaona aibu kwenye Dunia hii ya Sasa hivi na aibu itapelekea kujituma na kuweaka usahihi wa mambo japo ata Kwa udogp tu,kisha maboresha yatafuatia
Yani hata Gaza wametushinda. Aibu
 
Unavyoona hapo siyo maua au mchoro wa kompyuta ni muonekano wa mji toka angani.

Hivyo sio vibox ni plots zilizochorwa na kupimwa tayari. Yani miundombinu imetangulia kabla ya watu kuanza kuishi.

Mazingira haya utayaona kwa jamii nyingine lakini sio kwa Wabantu. Sisi tuna shida gani?
Rushwa tumuachie nani shida ndio hiyo
 
Hapa mtahani choo kikiharibika ukitaka kukijenga tu ni lazima upate kibari Kwa mjumbe sembuse nyumba na wanafanya hivi Ili kisimamia mpango mji wa eneo husika lakini ukiuangalia mtaa wenyewe uliivyo upo hovyo kabisa Sasa sijui wajumbe Huwa wanasimamia mchoro wa mpango mji Gani?(Watendaji)

Kipindi Cha Magifuli kulikuwa na ujengaji wa barabara za mitaa ndio nikaona plan iliyokuwako kabla ya mtaa lakini haikufuatishwa watu wemejenga wakaifuta kabisa barabara,watu wemejenga mpaka kwenye njia za maji afu wanalalamika mafuriko,serikali ikataka kubomoa watu wakabisha kuwa wao wapo Toka kitambo🤓
Alafu unasikia nyumba Iko karibu na barabara
 
Ajabu ni kwamba Maafisa mipango miji wapo humuhumu na pengine wamechangi HII MADA
Inawezekana kweli wapo, lakini hata wakipeleka mapendekezo ya kitaalam, wafanya maamuzi wana vipaumbele vyao. Inabidi uangalie chanzo halisi cha tatizo vinginevyo utalaumu watu bure.
 
Afisa mipango miji hawezi kuanzisha tu mradi wa kupanga makazi bila budget wala back up ya wanasiasa. Kila kipande cha ardhi unachokiona mjini kina mwenyewe, lazima ufuate utaratibu wa kukitwaa ndio ukipange. Na hapo ndio picha linapoanza.

Lakini shida kubwa ilianza mara baada ya waswahili kuchukua nchi kutoka kwa wakoloni, mambo mengi yaliachwa yaende kwa kudra tu, miji mingi haina hata master plan, mwisho mazoea ya squatters yakajengeka.

Kurekebisha hilo tatizo itakuwa gharama sana na Mimi naona hilo litafanyika na vizazi vya mbele sana baada ya sisi kupotea kabisa.
Duh! Mkuu hata miji mipya wanashindwa, mana kweli tumekosea toka awali lakini vipi maeneo yasiyokaliwa, kwanini mipango isifanyike mapema?
 
Hapa mtahani choo kikiharibika ukitaka kukijenga tu ni lazima upate kibari Kwa mjumbe sembuse nyumba na wanafanya hivi Ili kisimamia mpango mji wa eneo husika lakini ukiuangalia mtaa wenyewe uliivyo upo hovyo kabisa Sasa sijui wajumbe Huwa wanasimamia mchoro wa mpango mji Gani?(Watendaji)

Kipindi Cha Magifuli kulikuwa na ujengaji wa barabara za mitaa ndio nikaona plan iliyokuwako kabla ya mtaa lakini haikufuatishwa watu wemejenga wakaifuta kabisa barabara,watu wemejenga mpaka kwenye njia za maji afu wanalalamika mafuriko,serikali ikataka kubomoa watu wakabisha kuwa wao wapo Toka kitambo🤓
= kibali.

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Siasa ndo inaharibu mambo...
Enzi hizo jiji la Mwanza lilikuwa na mradi wa sustainable cities program, mjamaa mmoja akapel3kwa nje kusomea mipango miji degree ya uzamili... aliporejea tu alikaa miezi michache tu akateuliwa kuwa DED...
 
Hata Syria iliyotoka vitani bado kuna mipango mizuri na michoro mizuri kuliko sisi tusiokua na vurugu.
kwa kweli sisi akili zetu ni za kuvukia barabara. Pale kokobeach parking mwaka wa 3 huu city inachukua mapato kuweka sakafu hawataki ni matope matupu. na bado hawaweki taa fukwe nzima giza wakati investiment zake ni kubwa sana.

watanzania hawa weledi, watanzania hawawezi fikiri kwa manufaa yao na vizazi vyao. namalizia watanzania ni washamba wa maendeleo
 
Ardhi Sio kipaumbele cha Serikali, Huwezi kupanga Ardhi ambayo siyo ya kwako. Tanzania tuna sheria ya Utwaaji Ardhi, Kabla ya kuchora Hayo maua unayo yaona na hivyo vibox, inatakiwa ulipe kwanza Fidia.

Nani analipa hiyo fidia? Serikali Ardhi sio kipaumbele chake, hivyo fidia atalipa pale ambapo kuna Kipaumbele chake. Huko kwingine acha kujiendee. Ndio maana Si Ajabu kukuta Kijiji kiko ndani ya Hifadhi, Eneo la Uwanja wa ndege limevamiwa, n.k

Miji yetu itaweza kupangika vyema kama Serikali italipa Kipaumbele suala la Ardhi kwa maana ya;
1. Upangaji
2. Upimaji
3. Kusimamia Uendelezaji. Tofauti na Hapo tutakua na Makazi Holela (Squatter) nchi nzima.
 
Back
Top Bottom