mokala1989
JF-Expert Member
- May 4, 2013
- 2,236
- 728
#hapakazitu. tarehe 26/10/2015 alfajiri kabla ya jogoo hajawika watu watasaga meno kwa kutoamini kilichotokea tanzania!
Mmh!! Mbona kama wanaandaa ilani mpya ya uchaguzi??
Ama kweli Magufuli ni mgombea huru.
Ni dalili za anguko la ufalme wa shetani hapo Octoba 25
One word, Lowassa!
Chagua CCM,Chama cha AMANI.AMANI kwanza,mengine baadaye.
Jamaa wanaandaa 'ilani' mpya. wameona iliyopo haiwashawishi watanzania.
Yaani mnachunguza wakati mlisema matatizo ya watanzania mnayajuwa...!!!
Anyway baneni matumizi na ongezeni juhudi kwenye haya
1. Fungeni wote wa mishahara hewa
2. Halmashauri zenye hati chafu watieni ndani wote
3. Kamata wakwepa kodi wote
4. Futa misamaha ya kodi
Habari kutoka Lumumba zinasema Maraisi Wastaafu wameamua kupanda Majukwaani Kumsaidia Magufuli.Tunawasihi sana Wasitumie lugha za MATUSI VITISHO Na UONGO Kwani wao kama Viongozi hawastahili kufanya hivyo Na yule ALIYETUTUKANA ETI WATANZANIA WATAKA MABADILIKO NI WAPUMBAVU Na MALOFA ASIRUDIE TENA.
Wana bodi!
Hali ya CCM ni mbaya sana. Hawakutegemea kabisa kuwa watanzania watawakataa kama inavyotokea sasa. Na katika ku-panic na kuonyesha taharuki wamejikuta wanafanya mambo yanayozidi kuwafumbua wananchi macho na kuiona CCM ni kundi la matapeli:
1; Matusi ndio imekuwa ilani yao ya uchaguzi.
2: Magufuli ameshindwa kujinadi kwa kutumia jina la CCM na badala yake anajinadi kama mgombea binafsi.
3: Na kali ya funga kazi ni hii iliyotokea leo: wamekuja na mpango wa maandalizi ya ilani mpya huku ile ya zamani wakiwa wameitupa. Hebu oneni huu utapeli:
My take: CCM wanazidi kuonyesha utapeli, ulaghai na kuwa ni wale wale wala hawakuwa wamejiandaa. Hivi kweli inaweza kuingia akilini mtu kusema Chama kilichotawala muda wote huu haya mambo kilikuwa hakiyajui na sasa ndio wameshtuka na wanaanza kuchunguza? Si ni kwasababu wameona hali ni mbaya ndio maana wanakuja na mipango mipya huku hata iliyopo kwenye ilani haijatekelezwa?