Elections 2015 Kinana aanza ziara ktk Majimbo 64. Magufuli aunda kikosi kazi... Mkapa, Kikwete nao wajipanga!

Elections 2015 Kinana aanza ziara ktk Majimbo 64. Magufuli aunda kikosi kazi... Mkapa, Kikwete nao wajipanga!

MUHIMU: Mshahara wa Raisi na mawaziri uwekwe hadharani ili tujue tunawalipa sh.ngapi kwa mwezi.
 
Bad timing. Zimebaki siku 10 Magufuli anataka kurudia kampeni kule kote alikopita. Watanzania walisha msahau kabisa.... hahahaa. Na akirudia kama mtoa Topic alivyo andika hapa lazima atakutana na zomea zomea kwani watanzania walio wengi walishaamua kwamba " Lowassa atosha ".
 
Tupo vizuri... Mnajua mambo tuliyoyafanya katika majimbo 208!!! CCM is back again where it belongs!! Thanks Comrade MAGUFULI for making us laughing again!!!

Kwa sanduku la kura Hapana. Labda ki vingine. ccm wapumzike. Inatosha.
 
Wahenga walinena mfa maji haiishi/haachi kutapatapa.

Juzi katika jukwaa la kampeni ndg. A. Kinana aliponda sana tabia ya kuongoza nchi kwa vikao mara sijui jopo. Leo mwaunda majopo mengine?

Hakika pumzi imekata.
 
Dah, maccm vituko haviishi. Ina maana Kikwete alikuwa hajui hata kero za wananchi, alikuwa hajui maeneo yatakayoongeza mapato haraka!!! Naona mmechanganyikiwa, mgombea wenu Pombe amekuwa kama headless chicken
 
Unakusanyaje maoni two weeks before watu kupiga kura?

Je ilani imetokana na inputs zipi endapo ni sasa ndio mmeanza kukusanya maoni?
 
Sijaona jinsi ya kushughulikia ufisadi,mikataba mibovu ya uwekezaji,viwanda,ujenzi wa reli na bandari.Ukawanaji ulio sawa wa keki ya taifa.Mwisho ni maisha yale yale.Nauelewa sana ule wimbo wa ccm ni ile ile hivyo haina jipya.
 
Dkt. Magufuli amelipa jopo hili majukumu yafuatayo:

1. Kuchunguza na kupendekeza maeneo ambayo Serikali itabana matumizi, ikiwemo manunuzi ya umma, posho za vikao na matumizi ya magari, ili atoe maamuzi kuanzia siku ya kwanza atakapoapishwa;

2. Kuchunguza na kupendekeza maeneo ambayo Serikali itaongeza mapato mara moja bila hatua za kibajeti kuanzia siku ya kwanza atakapoapishwa;

3. Kuchunguza na kupendekeza maboresho makubwa katika mfumo wa utendaji na utumishi na ufanisi katika Serikali;

4. Kupitia kodi na ushuru wenye usumbufu kwa wafanyabiashara wa ngazi zote, wakulima, wafugaji na wavuvi iwapo unaweza kurekebishwa bila kuathiri bajeti ya Serikali inayotekelezwa sasa.

5. Kupitia sheria zote za nchi na kuorodhesha Sheria ambazo zinapaswa kubadilishwa haraka ili kuharakisha mabadiliko ya kweli na ya haraka ambayo ameyaahidi kwa Watanzania;

6. Kupitia na kuorodhesha masuala yote na kero zote zinazosubiri maamuzi ya Serikali ili atoe maamuzi kuanzia siku ya kwanza atakapoapishwa.

7. Kupendekeza miundo na idadi ya Wizara na kutengeneza rasimu za mikataba ya kazi kwa Mawaziri, Makatibu Wakuu na watendaji wengine wakuu atakaowateua mara baada ya kuapishwa.

8. Kupendekeza njia za haraka za kumaliza kero za watumishi wa umma, hasa walimu, askari, madaktari na wauguzi, ili aanze nao kazi wakiwa na ari na morali ya kusukuma mabadiliko ya kweli.

9. Kutengeneza rasimu ya mpango-kazi wa utekelezaji wa Ilani ya CCM na ahadi alizozitoa kwenye kampeni, hasa upatikanaji wa ajira kwa haraka na umeme wa uhakika;

10. Kupendekeza muundo wa kitaasisi na utaratibu muafaka wa kutekeleza ahadi ya kutoa shilingi milioni 50 kwa kila kijiji na mtaa nchini.

Dkt. Magufuli ameazimia kuanza kazi mara moja kwa bidii kubwa na maarifa mapya.


Imetolewa na:-

January Makamba
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa
Mjumbe wa Kamati ya Kampeni
LOWASSA anatisha mnatumia jina lake kumnadi mgombea wenu?
 
Kuna taarifa zimechapishwa na magazeti kuwa kuna mgombea urais ameunda jopo la wataalamu wa kumsaidia.Jopo hilo mbona lipo tangu 2013?Kuna taasisi inaitwa Presidential Bereau,taasisi hii ina wataalamu wengi wanaomshauri Rais.Sasa hilo jopo lingine ni la nini kama sio propaganda?
 
Kuna taarifa zimechapishwa na magazeti kuwa kuna mgombea urais ameunda jopo la wataalamu wa kumsaidia.Jopo hilo mbona lipo tangu 2013?Kuna taasisi inaitwa Presidential Bereau,taasisi hii ina wataalamu wengi wanaomshauri Rais.Sasa hilo jopo lingine ni la nini kama sio propaganda?
 
Back
Top Bottom