Tetesi: Kinana agoma kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya CCM

Tetesi: Kinana agoma kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya CCM

Status
Not open for further replies.
Kuchafulia kwa lipi? Au kusemwa wewe ndiyo unaita kuchafuliwa! Acha watu watoe maoni yao. Uhuru wa maoni ndiyo tunaoutaka. Mkapa baada ya kuondoka madarakani alisemwa sana sana yeye na mke wake! Mwinyi hivyo hivyo!
wanataka wasafishwe; eti tuwapake mafuta ya nazi wameremete!!

Unamjua Makamba alitukana watu wa Tarime matusi ya nguoni hadharani alipozomewa wakati wa kampeini fulani za uchaguzi mdogo wa kujaza kiti cha Chacha Wangwe.
 
Ndiyo facts na dynamics za maisha hizo; hakuna Kiongozi ambaye ni malaika; la kufanya ni kusubiri naye amalize muda wake kwa mujibu wa Katiba, afuate mwingine, ambaye naye atakuja na ya kwake.
Huenda hukukusudia kuyaandika uliyoandika hapa, bali yametoka tu bila ya tafakuri.

Hizo unazoziita 'facts' zitakuwa zina kasoro kama zinahitaji mabavu kuzitekeleza ili kukidhi matakwa ya mtu mmoja anayelazimisha ziwe 'facts'.

Na kama hali hiyo ndiyo unayoiita 'dynamics' za maisha, usisahau pia kwamba ni 'dynamics' hizo hizo watakazotumia watu wengine kukataa kunyanyaswa.

Kwa hiyo hizi unazoziita 'facts' (zilizopinda) hazina 'absolute' yoyote kama unavyotaka kuzifanya zionekane hivyo.

Huyo anayetafuta kugeuza taratibu zilizoko ndani ya chama (ambazo ndio 'facts' zenyewe, na kuzigeuza ziwe za manufaa kwake binafsi, hata CCM ambayo ni mbovu itawapata baadhi ya wachache watakaopinga juhudi hizo.
.
Makamba na Kinana, sina sababu yoyote ya "kuumizwa" juu yao.
Wao ni sehemu ya CCM mbovu inayoendelea hadi leo. Kuniumiza kwao ni kukumbuka juhudi walizofanya 2015 hadi kutufikisha hapa tulipo leo kwa kutuletea huyu asiyetaka hata kutambua uwepo wa taratibu unazoziita 'facts', yeye akitunga 'facts' zake pembeni kabisa ya zile zilizotumika ndani ya chama miaka yote.

Hii unayoita 'fact' ya mtu kustaafu na kuwa kama mzoga usioweza kutambua lolote ndani ya chama walichokitumikia miaka yote, in aina ya 'fact' feki.
Mwalimu Nyerere hakuikubali 'fact' ya kipuuzi kama hiyo.
 
Huenda hukukusudia kuyaandika uliyoandika hapa, bali yametoka tu bila ya tafakuri.

Hizo unazoziita 'facts' zitakuwa zina kasoro kama zinahitaji mabavu kuzitekeleza ili kukidhi matakwa ya mtu mmoja anayelazimisha ziwe 'facts'.

Na kama hali hiyo ndiyo unayoiita 'dynamics' za maisha, usisahau pia kwamba ni 'dynamics' hizo hizo watakazotumia watu wengine kukataa kunyanyaswa.

Kwa hiyo hizi unazoziita 'facts' (zilizopinda) hazina 'absolute' yoyote kama unavyotaka kuzifanya zionekane hivyo.

Huyo anayetafuta kugeuza taratibu zilizoko ndani ya chama (ambazo ndio 'facts' zenyewe, na kuzigeuza ziwe za manufaa kwake binafsi, hata CCM ambayo ni mbovu itawapata baadhi ya wachache watakaopinga juhudi hizo.
.
Makamba na Kinana, sina sababu yoyote ya "kuumizwa" juu yao.
Wao ni sehemu ya CCM mbovu inayoendelea hadi leo. Kuniumiza kwao ni kukumbuka juhudi walizofanya 2015 hadi kutufikisha hapa tulipo leo kwa kutuletea huyu asiyetaka hata kutambua uwepo wa taratibu unazoziita 'facts', yeye akitunga 'facts' zake pembeni kabisa ya zile zilizotumika ndani ya chama miaka yote.

Hii unayoita 'fact' ya mtu kustaafu na kuwa kama mzoga usioweza kutambua lolote ndani ya chama walichokitumikia miaka yote, in aina ya 'fact' feki.
Mwalimu Nyerere hakuikubali 'fact' ya kipuuzi kama hiyo.
Usipindepinde kama nyoka; naona sasa unaandika kutoka pande zote ziwekanazo. mambo yote uliandika hapo ni poumba tupu.

Kwanza elewa kuwa kutoa ushauri kuhusu sera ni tofauti na kulalamika kuwa unachafuliwa binafsi; na kutoa ushauri haina maana lazima ushauri huo ukubaliwe na aliyeko madarakani, ndivyo demokrasi ilivyo. Nyerere alishauri mabenki yasizwe lakini Mkapa akayauza. Nyerere alizuia Azimio la Arusha lisifutwe, lakini Mwinyi akalifuta kule Zanzibar; Nyerere alikuwa akiongelea sera, hakuwa naongelea kuchafuliwa na mtu, na bado viongozi walioko madarakani walipuuza sehemu ya ushauri wake.

Pili: kama huumizwi na hao jamaa zako, hii ilikuwa topiki kuwahusu wao, imekuvuta nini kuwatetea. Kama unaichukia CCM yoteM, na unajua wao ni sehemu ya CCM usingechukua sides; ungewaacha wafu wazikane wao kwa wao. Unachozungumza hapa ni kuwa CCM yao ilikuwa nzuri kuliko CCM ya leo, halafu bado unasema CCM huitaki; come on.

Mengine yote uliyoandika hayana yoyote; labda wewe ni defense lawyer anayehanganika kwa nguvu sana kucreate any possible doubt kwenye facts zilipo mbele. Kama hujui facts bali unatafuta yale yanayokufurahisha ndiyo uone ni facts na yale yasiyokufurahisha siyo facts basi una matatizo ya kiakili na itakuwa ni vigumu kukusaidia. Mtu asiyeona hata ukimwashia taa za floodlight za Watt 10000 bado hataona.
 
mambo yote uliandika hapo ni poumba tupu.
Halafu ukahangaika sana kuzijibu 'pumba'! Ni nani aliyepungukiwa na akili hapo?
Kwanza elewa kuwa kutoa ushauri kuhusu sera ni tofauti na kulalamika kuwa unachafuliwa binafsi;
Kuingiliwa mawasiliano ambayo ni ya mtu na mtu faragha, sio kuvunjiwa heshima? Tena watu wanaofanyiwa kitendo hicho wakiwa wastaafu, ambao kwa raia wa kawaida angedhani ni watu wanaoheshimika ndani ya chama!

Kama wanayo madudu yao yaliyogundulika ndani ya chama, haya yasingeweza kushughulikiwa kwa taratibu za kichama huko huko ndani ya chama?

Sasa unajitoa ufahamu. Ni sehemu ipi Kinana na Makamba walipolalamikia kuwa "ushauri wao hausikilizwi". Kwa hiyo malalamiko yao hayo ndio iliyokuwa sababu ya wao kudukuliwa mawasiliano yao?
Kwanza elewa kuwa kutoa ushauri kuhusu sera ni tofauti na kulalamika kuwa unachafuliwa binafsi; na kutoa ushauri haina maana lazima ushauri huo ukubaliwe na aliyeko madarakani, ndivyo demokrasi ilivyo. Nyerere alishauri mabenki yasizwe lakini Mkapa akayauza. Nyerere alizuia Azimio la Arusha lisifutwe, lakini Mwinyi akalifuta kule Zanzibar; Nyerere alikuwa akiongelea sera, hakuwa naongelea kuchafuliwa na mtu, na bado viongozi walioko madarakani walipuuza sehemu ya ushauri wake.
Pamoja na yote hayo, Mwalimu Nyerere hakudhalilishwa na hao uliowataja. Hakudukuliwa maongezi yake, na wala hakuitwa kwenye kamati za kipuuzi kuchunguza malalamiko yake.
Huna hata akili ya kutofautisha hali hizi mbili ambazo ziko wazi kabisa?

Mwalimu alikuwa na uhuru na haki ya kusema alichoona hakiko sawa, na heshima yake haikudhalilishwa na Mwinyi, na Mkapa. Huyu unayetetea wewe ana nini cha ziada watu wasitoe maoni yao?
Pili: kama huumizwi na hao jamaa zako, hii ilikuwa topiki kuwahusu wao, imekuvuta nini kuwatetea. Kama unaichukia CCM yoteM, na unajua wao ni sehemu ya CCM usingechukua sides; ungewaacha wafu wazikane wao kwa wao. Unachozungumza hapa ni kuwa CCM yao ilikuwa nzuri kuliko CCM ya leo, halafu bado unasema CCM huitaki; come on.
Hapa pia unaonyesha upungufu wa uwezo wako wa kufikiri.
Kuna pande mbili zinazohusika kwenye mzozo huo.

Kutoshangilia upande ulioko wewe hakuna maana kwamba naunga mkono upande usioupenda wewe.

Anayechukua jukumu la kukiuka taratibu na kujifanya yeye ndiye mwenye haki ya kujua na kuamua kila kitu, tena kwa kujinufaisha yeye mwenyewe, hiyo ni sifa ambayo ni nzito zaidi inayovuta hisia za kuipinga bila lazima ya kusifia huo upande wa pili.

Kiufupi ni kwamba hapo mwanzo nilikupa 'credits' ambazo kumbe huzistahiri kabisa. Pale kwenye "Uwanja wa Chato" nilidhani umeghafirika tu, kumbe ndio kawaida yako.
 
Wakati Membe akitamba kuwa alienda mbele ya kamati ya maadili ya CCM kuwafunda na kuwaelimisha kuhusu mambo mbalimbali, Kinana amegoma kufika mbele ya kamati hiyo.

Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika, Kinana ameona ni kama kudharauliwa kwa kuitwa kuhojiwa mambo ambayo kimsingi ni malalamiko aliyotoa kuhusu namna alivyokuwa akipakwa matope na mtu anayejiita Cyprian Musiba. Inaelezwa kuwa aliyetakiwa kuitwa ni Musiba na siyo Kinana.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi ndani ya chama, Kinana jana ijumaa alitakiwa kuwepo mbele ya kamati hiyo ya maadili lakini alisubiriwa hadi jioni na hakuna taarifa yoyote rasmi iliyopatikana juu ya kutokuhudhuria kwake mbele ya kamati hiyo.

Aidha hakutuma ujumbe wowote wa udhuru kuelezea kuhusu yeye kushindwa kufika mbele ya kamati hiyo kama ilivyopangwa.

Tusubiri tuone.
Acha uongo Membe katamba wapi kuwa amewafunda na kuwaelimisha kamati ya maadilio?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom