Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 95,871
- 116,627
Hivi kwanini huku kwetu tembo wameanza kupungua kwa kasi sn hawavamii tena kwenye makazi yetu shida ni nini?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
kwa ujinga wao wanahisi tunaishi kwa hisani yaoHivi Kinana na ccm wanafikiri hii nchi ni Mali Yao. Yaani wanaona kutenda matakwa ya wananchi na kuheshimu katiba kama ni hisani ya rasi. Sikio la kufa halisikii dawa. Ccm wanafikiri kila anaye wakosowaji ni chadema. Na kila anaye wapiga ni chadema. Ipo siku Hawa maccm watajikuta wanapambana na watu wasio kuwa na kiongozi kama vilivyo tokea sudani. Ndio wa tafuta pakujificha na itakuwa too late.
Naunga mkono hoja..vyombo vya habari mmetuangusha.
..mlipaswa muandae mdahalo unaohusu miswada iliyopelekwa bungeni.
..mnaweza kufanya hivyo sasa hivi ili wananchi wajue ukweli.
..andaa mdahalo wa makatibu wakuu wa vyama.
Najipanga kwa hilo 2025, kwa kuanzia uwe unanifuatilia nina kipindi Channel Ten kila Jumapili saa 3:00 usiku, marudio ni Jumatano saa 9:30 Alasiri. Kipindi cha jana ni hiki
View: https://youtu.be/cQiwZySjhsg?si=-4HRmye7ClGDrC0C
P
Huyu anadhani hapa tubna deal na meno ya tembo......KINANA AITAKA CHADEMA KUTHAMINI NIA NJEMA YA RAIS SAMIA KATIKA MARIDHIANO.
Na Mwandishi Wetu
MAKAMU Makamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Abdulrahman Kinana, amesema nia njema iliyooneshwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kutaka maridhiano inapaswa kuendelezwa na vyama vyote vya siasa.
Aidha, amevishauri vyama vya siasa vya upinzani hususan CHADEMA kuacha kufanya maandamano yasiyo na msingi badala yake wathamini utayari wa Dk. Samia katika kuhakikisha nchi inapiga hatua kubwa katika maendeleo yakiwemo ya demokrasia.
Kinana ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wazee wa mkoa wa Dar es Salaam, ambapo alitumia muda mwingi kuzungumzia, maridhiano yaliyoingiwa kati ya CCM, CHADEMA na vyama vingine vya upinzani nchini.
Kinana aliitaka CHADEMA kueleza ukweli kuhusu mambo mazuri yaliyopatikana baada ya kuwepo kwa maridhiano ikiwemo serikali kukipatia chama hicho ruzuku ya Sh. bilioni 2.7 ambayo waliikataa kwa miaka mitatu nyuma.
Akielezea kuhusu sheria mpya, Kinana alisema pamoja na uzuri wake ikiwemo kuzingatia maoni ya wadau wakiwemo CHADEMA wenyewe, lakini bado kinasema haifai.
“Nilifikiri sheria hii mpya wangesema itatufikisha mbali zaidi, lakini wao wanasema hii haifai, basi turudi kule. Sheria ya sasa ni bora kwa muundo, kwa maudhui, kwa malengo, kwa dhamira sijui mnanielewa?. Nitumie nafasi hii kuwasihi ndugu zangu wa CHADEMA waungane na Watanzania waachane na mandamano, waangalie dhamira ya Rais.
“Hivi Rais na baraza lake la mawaziri kama wasingepeleka hii sheria mpya ya uchaguzi nani angemlazimisha? Lakini Rais busara imemuongoza akasema hapana hebu twende pamoja na mimi ndio mtetezi mkubwa wa maridhiano na ustahimilivu. Hebu tupeleke sheria mpya bungeni na kila hoja aliyopelekewa, aliyoambiwa kwamba haya ndio maoni ya wadau Rais akasema sawa, nakubali,” amesema.
== ==
Hakuna vyombo vya habari hapa, ni makanjanja tu wa kuganga njaa..vyombo vya habari mmetuangusha.
..mlipaswa muandae mdahalo unaohusu miswada iliyopelekwa bungeni.
..mnaweza kufanya hivyo sasa hivi ili wananchi wajue ukweli.
..andaa mdahalo wa makatibu wakuu wa vyama.