Kinana: Msilaghaike na kikundi cha wasaka madaraka kwa mgongo wa hoja ya serikali tatu.

Kinana: Msilaghaike na kikundi cha wasaka madaraka kwa mgongo wa hoja ya serikali tatu.

Hahaaaahaa

Kila ukianzisha uzi wako wa propaganda huwa unaweka picha, vp pemba kamera ziligoma?

Hahaaa mtakufa kwa vihoro mwaka huu, Serikali tatu ni lazima sio ombi wala hisani.
Gonga hapa chini ili upate kile unachopenda kukiona

Lakini vile vile uache kudanganya wanaJF kuwa wewe ni mtoto wa kuzaliwa wa Mwl. Nyerere wakati hufahamu hata mlango wa nyumba yoyote ya Mwl. Nyerere.

Ulidanganya sana mpaka familia ya Mwl. Nyerere akaamua kuchukua maamuzi ya kukuonya kuhusu kutapeli watu kwa kutumia jina la Mwl. Nyerere.
Nilikuwa naongea na Joseph Butiku sasa hivi,na Mama Maria. Nimewauliza kuhusu huyu Yericko Nyerere. Hawamfahamu. Butiku amesema,watu wanajipa majina wanavyopenda; Adam Marwa ana mtoto wake mmoja tu,anaitwa Lumumba. Mimi[Butiku],mtoto wangu anaitwa Kaunda. Magige Nyerere ana mtoto anaitwa Moringe. Halafu Mama Maria akasema,Rose Nyerere ana mtoto anaitwa Luis Rwagasore,Mfalem wa Rwanda.
Kwa hiyo Butiku amesema huyu kijana kama angekuwa na namba ya simu,ningeweza kumtafuta,ili aweze kujieleza. Kwa hiyo nimempa Butiku namba ya simu ya Yericko Nyerere.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-tanganyika-na-zanzibar-221.html#post6613446
 
Nani kabaguliwa zaidi ya ile ya Lukuvi aliyosemea kanisani wasuruhusu uislam zanzibar?unaandika uharo tuu hapa.Kama ni serikali 2 kwa nini msirekebishe katiba iliyopo na mboreshe muungano kama mnavyotaka?kulikua na haja gani kuunda kuunda tume na kuiita katiba mpya wakati bado mnafikra za kizamani?
Ndugu, kwa akili na fikra zako unadhani kazi pekee ya Tume ya Katiba ilikuwa ni kubadilisha muundo wa serikali pekee.

Kuwa na watu wenye fikra na mtazamo kama wako, sina budi kusema kuwa, taifa lina safari ndefu katika mabadiliko endelevu kifikra na kimtazamo.
 
Wakati mwingine Mwanadiwani hoja zake zina mashiko,mm ni muumini wa serekali tatu ,hofu yangu kwa chama changu ni huu muungano wa UKAWA Naamini chama changu kinanguvu ya kutetea msimamo wa chama wa serikali tatu bila kuungana maana tuna mtaji wa wananchi,tunakubalika sana,UKAWA bado sijaikubali isije ikatuvuruga
 
Mnyika alikuwa sawa tu, tumefika hapa kwa uzembe na ujinga wa watu wachache sana
 
Hapo anaangalia maendeleo au anatukana ukawa? watahangaika sana nan wachumia tumbo? billion kujenga ukumb wa bunge,billion 70 tume ya warioba halaf mawazo ya wananch hawayatak ukawa imewashka pabaya hawa jamaa..waendelee kuwapa pilau tu wananch kweny mikutano yao lakn kwenye kura ya maon 3 ndo habareeeee 2 kzamaaan
 

Attachments

  • 1399187160396.jpg
    1399187160396.jpg
    58.3 KB · Views: 85
  • 1399187182720.jpg
    1399187182720.jpg
    63.2 KB · Views: 83
Ndugu, Kama CCM ingekuwa inahadaa wananchi basi isingepata fursa kutoka kwa wananchi hao hao kuiongoza nchii tokea uwanja wa siasa za vyama vingi uanzishwe kikatiba.

Wananchi asilimia ngapi ya watanzania wote ??. Au hilo hujajiuliza? Na huo uongozi hua mnaupata kwa njia ya haki na democrasia bila kutumia nguvu???kuwa muwazi basi!! Wali maharage na kanga na vibahasha huwa vinatafuta nini kwenye uchaguzi? Tuambie basi halafu vipi kuhusu kofia na t shirt mnao wadanganyia watanganyika wasio na uelewa wala elimu?? Tijibu basi! Na vipi kuhusu ununuzi wa shahada za wapiga kura wasio jitambua??? Lengo huwa ni lipi hapo?? Kama mnakubalika hayo yote huwa mnayafanya ya nini???si mtulie tu kama vyama vingine uchaguzi ufanyike bila nguvu wala vitisho ,rushwa,na wizi wa kura pamoja na kura feki muone majibu halali ya uchaguzi??tupe majibu pia asilimia ngapi ya wananchi wote tanzania wanapiga kura kulinganisha na idadi iliyo jiandikisha?? Ukitoa majibu sasahihi kwa maswali yangu hayo hapo nitaungana na wewe kuwa kweli ccm bado inahitajika.
 
Kinana ndo katibu wa vikao vya uchakachuaji wa maoni ya wananchi kwenye rasimu ya warioba, kwe kamati kuu ya ccm na Nec ya ccm! Dhambi ya uchakachuaji haiwezi kumwacha salama kamwe!
 
Toa huu uchafu hapa. Hivi serikali tatu ni hoja ya vyama vya upinzani au wananchi? Wachumia tumbo wakubwa nyie.
Serikali tatu sio hoja ya wananchi wacheni kuhadaa dunia. ccm wanakwenda kwenye uchanguzi kila siku na sera ya serikali mbili na wanakubalika. Hata Unguja juzi wamewabwaga upinzani uchaguzi mdogo. Mbowe eti anasema ccm inawahonga wajumbe wa bunge la katiba! Sasa ukawa mtabakiza kumtusi nani? Waasisi wanatukunwa, wabunge wamehongwa!
 
Watanzania wameonyesha mfano mzuri sana, kuwakataa UKAWA na hoja zao mfu.
 
Ndugu, Kama CCM ingekuwa inahadaa wananchi basi isingepata fursa kutoka kwa wananchi hao hao kuiongoza nchii tokea uwanja wa siasa za vyama vingi uanzishwe kikatiba.

inaonyesha siasa na dalili za ishara za kweli kuelekea siasa za kweli unazikwepa aisha kwa upofu wa kufundishwa au wa kupotosha .Si kweli ccm inashinda uchaguzi kwa nguvu ya hoja na kuungwa mkono na wapenzi wake bali ni ghiriba , kutumia vyombo vya dola kama usalama wa taifa, polisi, Madc, ma ded, tume ya uchaguzi , ma katibu kata, na rushwa ambayo inawaghraimu wapiga kura baada ya uchaguzi.Nikukumbushe majimbo ya masasi, nanyumbu na liwale ni ccm ilishinda kwa kishindo kama takwimu zinavyoeleza.lakini ni juzi tu mali na maisha ya watendaji zilikuwa shakani hasa za umma kwa kuchomwa kisa sitabadhi gharani haina mashiko kwa kuchelewesha pesa za walipa kodi na wapiga kura.kama kweli ccm ingeshinda kwa kishindo haya yasingetokea hata kama kero hizo zingejitokeza suluhu ingepatikana na si kukimbilia mali za makada wa ccm na mali za serikali.kwahiyo nakusihi acha kutoa jumuisho lisilo na mashiko si hivyo ccm inaungwa mkono bali inashinda kwa hila na ghiriba ambazo hata wapiga kura wanazifahamu.

 
ccm heshimuni mawazo ya wananchi na msipo yaheshimu wananchi wao wenyewe watawachukulia hatua kali hapo ndo mtakapooona kuwa wananchi wanataka nini.
 
Hahaaaahaa

Kila ukianzisha uzi wako wa propaganda huwa unaweka picha, vp pemba kamera ziligoma?

Hahaaa mtakufa kwa vihoro mwaka huu, Serikali tatu ni lazima sio ombi wala hisani.

Hata mimi nimejiuliza sana imekuwaje huyu mpiga picha akawa hana picha za huyu muuwa Tembo wetu.??
 
Matumaini makubwa ya watanzania ni kupata Katiba itakayotumika kutuongoza ili kutuletea maendeleo na maridhiano katika taifa. Isiwe Katiba itakayowekwa kabatini na ikatoa mwanya kwa utawala usio kuwa na dira na hatimaye kutuzalishia utawala wa kidikteta. Pengine ni vyema wananchi waendelee kuelezwa umuhimu wa Katiba katika nchi kuliko kukatishwa tamaa.
 
Ndugu, Kama CCM ingekuwa inahadaa wananchi basi isingepata fursa kutoka kwa wananchi hao hao kuiongoza nchii tokea uwanja wa siasa za vyama vingi uanzishwe kikatiba.

Si wanaongoza kwa hadaa vilevile au ni uongo? Uchaguzi wa shinyanga unakumbuka halmashauri ilichomwa moto? Sisi tulio neutral hatupendi ulaghai tunapenda mshindane kwa haki bila ulaghai wa kula nk!!
 
MwanaDiwani Nilikuuliza wagombea madaraka ni wepi waliopo madarakani miaka 50yrs
au wanaotaka kuondoa uozo huu???
Mdude Chadema Nyagali > Sauti ya Tanganyika DENI LA TAIFA KUTOKA TRION 27 MWAKA JANA MPAKA TRION 40.6
KWA NINI DENI LA TAIFA LINAONGEZEKA WAKATI MATUMIZI NI YALE YALE?
1.MISHAHARA KWA WATUMISHI NI ILE ILE
2.BARABARA NI ZILEZILE.
3.HOSPITAL NI ZILEZILE NA BADO HAZINA MADAWA
4 KAMA NI KATIBA TOKA MCHAKATO UANZE KWA JAJI WARIOBA MPAKA BUNGE LA KATIBA NI BILON 82 TU NDO ZILIZOTUMIKA.

HUENDA MATUMIZI MABAYA YA SERIKALI NDIYO YANAYOSABABISHA DENI HILI KUWA KUBWA EBU TUANGALIE MATUMIZI KWENYE OFISI LA RAIS USUSANI SAFARI ZA NJE .

1.Rais kama anasafiri nje ya nchi huongozana na maafisa wasiopungua 22 wakiwamo afisa usalama madoctor n.k.

2.mjumbe ama afisa yoyote anayekuwa kwenye msafara wa rais analipwa 600000/= laki sita kwa siku sasa unapaswa kuzidisha pesa hiyo kwa wajumbe wote 22 ambapo utapata milion 13200000/=milion kumi na tatu laki mbili kwa siku.

3.mjumbe ama afisa anayekuwa kwenye msafara wa rais analala HOTEL yenye thamani ya DOLA 1200 ambayo sawa na 1900000/= milion moja na laki 9 pesa hiyo uizidishe mara wajumbe 22 unapata 41800000/= milion arobaini na moja na laki nane kwa siku moja

4.hivyo basi ukijumlisha posho na malazi ya maafisa ama wajumbe kwenye msafara wa rais unapata shilingi 55000000/=milioni hamsini na tano kwa siku moja.

jumla ya safari za rais nje ya nchi ni 395 ukizidisha 395 mara shilingi milion 55 utapata hesabu kamili ya matumizi ya safari zote za rais nje ya nchi kwa maana calculator yangu imenock kwa kulingana na ukubwa wa hesabu.

5.bado usafiri ndege ya rais iliruka angani kwa muda wa saa moja hutumia milion 16.2
bado matumizi mengine kwenye ofisi ya rais kama vile safari za ndani n.k

6.baraza la mawaziri ;waziri mmoja hutengewa mafuta lita 200 ambazo sawa na laki nne 400000/= kwa siku ata kama anakoenda hakujulikani na hakuna faida kwa serikali na kuna mawaziri 60 ukizidisha idadi ya mawaziri hao mara laki 4 unapata 24000000/=milion ishilini na nne kwa siku moja

SASA NDUGU ZANGU KWA MATUMIZI HAYA KWA NINI TAIFA LISIPATE DENI KUBWA?
KWA NINI WATANZANIA MNAENDELEA KUKUMBATIA CCM KWA MATUMIZI MABAYA KAMA HAYA WAKATI HUO KUNA SHULE HAZINA MADARASA?

TAFAKARI CHUKUA HATUA
Bado tuu unatetea wezi, mafisadi na rushwa Mikataba mibovu ya siri???

Inauma sana kwakweli.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom