Kinana: Msilaghaike na kikundi cha wasaka madaraka kwa mgongo wa hoja ya serikali tatu.

Kinana: Msilaghaike na kikundi cha wasaka madaraka kwa mgongo wa hoja ya serikali tatu.

Ndugu, Kama CCM ingekuwa inahadaa wananchi basi isingepata fursa kutoka kwa wananchi hao hao kuiongoza nchii tokea uwanja wa siasa za vyama vingi uanzishwe kikatiba.
...kwani imewahi kupata kibali cha kuongoza...?
 
Hiki ni kichekesho ................... kama UKAWA wanasaka madaraka wao CCM wanafanya nini!!?? Tatizo la CCM wamelewa madaraka such that wanafikiri hakuna Mtanzania mwingine nje ya CCM anayeweza kuongoza au mwenye haki ya kuongoza nchi hii!! CCM wamelewa madaraka mpaka wanasahau kuwa hii nchi ni ya kwetu wote na siyo ya wanaCCM peke yao!! CCM wamelewa madaraka mpaka wanadhani kuwa ni wao peke yao wenye uwezo wa kutuongoza na hakuna mwingine!! CCM wamelewa madaraka kiasi kwamba wanafikiri ni wao peke yao wenye nia njema kwa nchi yetu kuliko raia wengine!! CCM wamelewa madaraka mpaka wamesahau Watanzania tunataka nini!!
 
Ni umoja wa wazalendo wa nchi ya tanzania kwa ajili ya kutetea na kuleta katiba mpya na mabadiliko ambayo yatamkwamua mtanzania kwenye lindi la umaskini wa kutisha.. ambao probably huo umaskini haujui ma hauluumizi mtu kama wewe

Umoja huo una uhalali gani kisheria?
 
Ila wanaipenda dhambi ya kuwagawa wananchi kwa imani ya dini zao kama anavyofanya kada wao Lukuvi!

Mkuu umesahau Nassari alipotaka kumzuia Kikwete eti asikanyage Arusha na Lema awe Rais, kisha yeye (Nassari) awe Waziri Mkuu? Mimi naamini yalikuwa ni mawazo yake binafsi ila ningekuwa na akili kama ya kwako ningesema kuwa hayo ni mawazo ya CHADEMA!
 
ccm heshimuni mawazo ya wananchi na msipo yaheshimu wananchi wao wenyewe watawachukulia hatua kali hapo ndo mtakapooona kuwa wananchi wanataka nini.

Unamaanisha mawazo ya wananchi 37,000 yaheshimiwe?
 
Mkuu umesahau Nassari alipotaka kumzuia Kikwete eti asikanyage Arusha na Lema awe Rais, kisha yeye (Nassari) awe Waziri Mkuu? Mimi naamini yalikuwa ni mawazo yake binafsi ila ningekuwa na akili kama ya kwako ningesema kuwa hayo ni mawazo ya CHADEMA!
Lukuvi ni waziri hivyo kauri yake ni kauri ya serikali, kwa kuwa bichwa lako limejaa takataka za CCM badala ya ubongo huwezi kuliona hili.
 
Kinana ataka wananchi wawalinde kundi la wala rushwa, mafisadi, majangili na wauza pembe za ndovu, watoboa watu macho.
 
kwani kinena ooh shit I mean kinana yeye siyo mwanasiasa alafu yy huzunguka kutafuta nn????? meno ya tembo au madaraka????
 
Hii ni sawa na kusema "msihangaike na kikundi cha walinda madaraka kwa mgongo wa hoja ya serikali mbili"
 
Kinana anachoongea ni true kwani serikali tatu ni kutafuta madaraka kwa hao ukawa,kama wanaitakia nchi hii mema si wapigie debe serikali moja? kupigia debe serikali tatu ni ukweli usiopingika ni uroho wa madaraka.
 
kupitia bunge la katiba, wananchi wapenda taifa endelevu wanazidi kubainishiwa ukweli ulioko ndani ya mioyo na fikra za baadhi ya viongozi kupitia kundi la vyama vya siasa wanaojiita kwa sasa ukawa.

Waingereza wanasema, birds of a feather flock together kwa maana kuwa, kwa sasa bunge la katiba limewakutanisha vinara wa ubaguzi na wasaka madaraka kwa njia zozote zile kuanzia viongozi wa vyama ambao baadhi yao wamekuwa katika uongozi wa juu wa vyama vya siasa kuanzia mwaka 1995 huku wengine wakijaribu kuwaomba wananchi wawaamini na kuwapa ofisi kuu nchini kupitia kura za urais (rais wa tanzania) lakini hawakufanikiwa kwa vile kile ambacho wananchi walikuwa wana wasiwasi nacho kuhusiana na fikra na mitazamo yao kama viongozi wakuu imeanza kudhirika katika bunge maalum.

Ubaguzi wao umezaliwa ndani ya vyama vyao, ukamea na kuimarika huku baadhi ya wanachama na waliokuwa viongozi ndani ya vyama wakiishia kuwa ni wahanga wa ubaguzi huo. Wengine walifukuzwa na huku wengine wakinyang'anywa madaraka. Kwa sasa ubaguzi unatafuta njia nyingine ya kujipandikiza kitaifa kupitia mchakato wa katiba baada ya kutamalaki ndani ya vyama vyao ili waendeleze nia yao ya kusaka madaraka kwa gharama zozote.

Pamoja na baadhi ya viongozi wa ukawa kupewa pesa kutoka nje kwa ajiri ya mradi wa kusaka madaraka. Dhambi ya ubaguzi itawatafuna wao wenyewe na katika dhambi hiyo, hawawezi kufanikiwa kupata kile wanachokitaka kwa nguvu zote. Huwezi kutenda dhambi mbaya kama hii halafu usalimike.

Huwezi kufanya ubaguzi na siasa za matukio halafu ufanikiwe. Siyo muda mrefu wataanza kubaguana wao kwa wao.

ccm ccm
 
Kinachowasumbua ccm ni kwamba wameshaingia mikataba na mashetani. Na hili limefanyika baada ya Nyerere kutokuwepo. Sasa unadhani watatekelezaje bila ya kuwa na mazingira yanayowaruhusu. Sasa wanasahau kuwa Mungu ana nguvu zaidi ya shetani. Hawajui kuwa hata kama sio UKAWA, wakatibumefikia na shetani anatakiwa kushindwa.
 
Mtu mwenye akili akikushauri jambo lab kijinga na ukakubali atakudharau. ccm wanavyotukomalia tuikatae UKAWA tukikubali watatudharau sana kuwa tulipata mkombozi tukashindwa kumtumia.
 
Back
Top Bottom