Kinana: Serikali iwachukulie hatua waliotajwa Ripoti za CAG

Kinana: Serikali iwachukulie hatua waliotajwa Ripoti za CAG

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
KINANA ARUSHA 10.jpg

Makamu Mwenyekiti wa CCM, Abdulrahman Kinana amesema ni wakati wa Serikali kuchukua hatua dhidi ya watu waliokutwa wameenda kinyume na maadili katika Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali

Amesema, "CAG hazushi, anafanya kazi zake kitaaluma. Katika Ripoti zake anaeleza kasoro nyingi na mambo yasiyofaa ambayo yamefanyika ikiwemo upotevu wa Fedha za Umma na matumizi mabaya"

Amesema Vyombo husika vya Serikali vina wajibu wa kuchukua hatua ili Fedha za Wananchi zisichezewe
 
Na Mwandishi Wetu,
Arusha.


Makamu mwenyekiti Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara komredi Abdulrahman Omar Kinana ameishauri na ameiomba serikali kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya wale wote waliotajwa kwenye ripoti ya mkaguzi na mdhibiti Mkuu wa hesabu za serikali (CAG).

Akizungumza kwenye mkutano wa ndani wa chama hicho mjini Arusha, Kinana amesema ni muhimu wote waliotajwa kwenye ripoti ya CAG wakachukuliwa hatua.

“Wakati umefika kwa serikali kuchukua hatua kwa wahusika wote waliylotajwa kwa kuisababishia serikali hasara, upotevu au ubadhirifu wa fedha za umma kupitia ripoti ya CAG” amesema Kinana na kuongeza

“ Ripoti ile inaonesha mambo ya hovyo yamefanyika, Si uzushi kazi ile ya ukaguzi imefanywa kisayansi na kitaalamu, wabunge wameijadili kwa ukali sana, hata wasomi na wananchi wengine wameijadili kwa ukali vile vile, Mimi nadhani ingekuwa vyema hatua ziwe zinachukuliwa papo kwa papo ili watu wajenge nidhamu na heshima kwa fedha za wananchi.” alisititiza Kinana

Kinana ambaye alikuwa anahitimisha ziara yake ya mikoa minne kukagua uhai wa chama, alisema pamoja na kwamba hana mamlaka ya kutoa amri kwa serikali lakini atamwambia Rais juu ya ushauri huo.

“Kwa nafasi yangu nazungumza kwa niaba ya mwenyekiti wetu ambaye ni Rais kwamba wahusika wachukuliwe hatua. Si kila jambo lazima Rais aagize, tujenge utamaduni wa kuwajibika sisi wenyewe.'

Amesema lazima kuwe na utaratibu wa kuwajibika mtu anapofanya kosa na akishindwa kufanya hivyo vyombo na taasisi zenye wajibu wa kusimamia uadilifu kwa viongozi na watendaji nchini hususani kwenye kujenga nidhamu na fedha za umma zichukue dhidi yake.

“Tujenge utamaduni wa kuwahi kuchukua hatua kwa wakati, mtu akae pembeni apishe uchunguzi na akithitika apishe wengine kwani kuna watu wengi wana uwezo hawana kazi!" alisema na kuongeza

“ Kila ripoti ya CAG inapotolewa tukianzia na hii wale wanaotajwa wawajibishwe kujibu na kuchukuliwa hatua. Ikiendelea kubaki hivi, ripoti inatolewa na kuwekwa kabatini fedha za wananchi zitaendelea kuchezewa.”

Kinana akiambata na katibu wa NEC itikikadi na uenezi Shaka Hamdu Shaka alihitimisha ziara yake ya mikoa minne ya Pwani, Tanga, Kilimanjaro na Arusha kukagua uhai wa chama leo mkoani Arusha.

IMG-20220427-WA0049.jpg
IMG-20220427-WA0063.jpg
IMG-20220427-WA0057.jpg
IMG-20220427-WA0039.jpg
IMG-20220427-WA0045.jpg
IMG-20220427-WA0055.jpg
IMG-20220427-WA0050.jpg
 
Na ile issue ya meno ya tembo kwenye meli yake ifufuliwe ili kulinda tembo wetu mbugani.
 
Hivi huyu hajawahi kutajwa kwenye tuhuma zozote ? Alichukuliwa Hatua ?

Naomba tufuate ushauri wake ipasavyo... ila sio CAG tu bale tuhuma zozote zichunguzwe na mwisho wa siku haki itendeke
Subiri siku ajikwae kwa Chadema ndio honeymoon yake itaisha ila akitaka aendelee kupigiwa makofi amponde JPM tu na kutembelea matawi ya chama [emoji38]
 
Na Mwandishi Wetu,
Arusha.

Makamu mwenyekiti Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara komredi Abdulrahman Omar Kinana ameishauri na ameiomba serikali kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya wale wote waliotajwa kwenye ripoti ya mkaguzi na mdhibiti Mkuu wa hesabu za serikali (CAG)...
Inamaana Kinana hamjasikia nguli wa siasa za Tanzania Mtukufu sana Dr Slaa akipinga ripoti ya CAG ?
 
Nimemuangalia usoni kwenye hii picha yake ni kajikuta na sema kwa sauti ya Mwl Nyerere hata wewe unamoral autority ya kuyasema haya?!!! Meli inayobeba mzigo isiyo jua ni kitu gani ilichobeba as long as umelipiwa nauli ya kuusafirisha.
 
Kata ya mbagala manispaa ya Temeke,mradi wa dmdp 2.16 bil pesa za fidia, C.A.G amebaini wakazi 94 ambao wamelipwa pesa hizo ili hali hawatambuliki hata na viongozi wa ngazi za mitaa,na kibaya zaidi kuna vipande vya barabara vimeshindika na kumalizia ujenzi sababu ya fidia.
 
Back
Top Bottom