Kinana ukiingia Tanga mtafute Bhoke Nyarobi, Afisa Elimu aliyenyanyaswa akaacha kazi

Kinana ukiingia Tanga mtafute Bhoke Nyarobi, Afisa Elimu aliyenyanyaswa akaacha kazi

Standards Person

JF-Expert Member
Joined
Apr 22, 2021
Posts
672
Reaction score
860
Katika mapokezi ya makamu mwenyekiti wa CCM bara ndugu Abrahaman Omari Kinana jana, amesema amepewa maelekezo na mwenyekiti wake aanze kupitia baadhi ya mikoa ikiwemo mkoa wa Tanga.

Kinana utakapo karibia Tanga fanya liwezekanalo hata kwa dakika chache uonane na aliyekua afisa elimu taaluma upande wa sekondari anayeitwa Bhoke ili upate picha ya ukatili uliopo jiji la Tanga

Baada ya mama huyo kuibua wizi wa mamilioni ya fedha za ujenzi zilizoliwa na mkuu wa shule moja jijini hapo na mabosi wake,manyanyaso yalianza ofisini kutoka kwa afisa elimu sekondari na aliyekua mkurugenzi wa jiji ambae kwa sasa hayupo. Kutokana na manyanyaso hayo mama huyo akaamua kuacha kazi. Je nimanyanyaso ya namna gani? Kinana mtafute mama huyo utapata picha kamili ya uozo uliopo Tanga jiji.

Baada ya wizi huo mkuu wa shule alisimamishwa kazi na TAKUKURU wakaingia kazini. Kumbe waliokua wanachunguza nao waliingia bei wakaanza kunyanyasa waliotoa ushahidi na kumuacha akijitamba mtaani mwizi huyo.

Tena kwa kuthibitisha na kuonesha udhaifu mkubwa wa kila aina ya rushwa mkuu huyo wa shule ambae ni mwanamke ati akapewa nafasi akaenda kukalia kiti cha afisa elimu taaluma. Kutoka tuhuma ya wizi hadi kukaa kwenye kiti cha afisa elimu. Hii rushwa iangaliwe vizuri. Ikumbukwe afisa elimu naye ametajwa katika wizi huo mkubwa.

Baadae walikuja watu wa TAMISEMI wakatoa amri mwanamke huyo atoke haraka sana ndani ya ofisi ya afisa elimu sekondari.

Ili kuonesha Tanga imeoza mtu ambaye ana tuhuma ya wizi na anachunguzwa na TAKUKURU eti anapewa uafisa elimu kata.

Tanga ni rushwa na rushwa ni Tanga. Mifumo imekua ya rushwa.

Ofisi ya afisa elimu ichunguzwe vizuri dhidi ya mwanamke huyo. TAKUKURU nao watoe muelekeo wa fedha zilizoibiwa.

Pia TAKUKURU na afisa elimu sekondari wachunguzwe kwamba je wana maslahi gani katika mamilioni yaliyoibiwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Comrade Kinana usifanye makosa
 
Katika mapokezi ya makamu mwenyekiti wa CCM bara ndugu Abrahaman Omari Kinana jana, amesema amepewa maelekezo na mwenyekiti wake aanze kupitia baadhi ya mikoa ikiwemo mkoa wa Tanga.

Kinana utakapo karibia Tanga fanya liwezekanalo hata kwa dakika chache uonane na aliyekua afisa elimu taaluma upande wa sekondari anayeitwa Bhoke ili upate picha ya ukatili uliopo jiji la Tanga
Baada ya mama huyo kuibua wizi wa mamilioni ya fedha za ujenzi zilizoliwa na mkuu wa shule moja jijini hapo na mabosi wake,manyanyaso yalianza ofisini kutoka kwa afisa elimu sekondari na aliyekua mkurugenzi wa jiji ambae kwa sasa hayupo. Kutokana na manyanyaso hayo mama huyo akaamua kuacha kazi. Je nimanyanyaso ya namna gani? Kinana mtafute mama huyo utapata picha kamili ya uozo uliopo Tanga jiji

Baada ya wizi huo mkuu wa shule alisimamishwa kazi na TAKUKURU wakaingia kazini. Kumbe waliokua wanachunguza nao waliingia bei wakaanza kunyanyasa waliotoa ushahidi na kumuacha akijitamba mtaani mwizi huyo.

Tena kwa kuthibitisha na kuonesha udhaifu mkubwa wa kila aina ya rushwa mkuu huyo wa shule ambae ni mwanamke ati akapewa nafasi akaenda kukalia kiti cha afisa elimu taaluma...... Kutoka tuhuma ya wizi hadi kukaa kwenye kiti cha afisa elimu. Hii rushwa iangaliwe vizuri. Ikumbukwe afisa elimu nae ametajwa katika wizi huo mkubwa.

Baadae walikuja watu wa TAMISEMI wakatoa amri mwanamke huyo atoke haraka sana ndani ya ofisi ya afisa elimu sekondari.
Ili kuonesha Tanga imeoza mtu ambaye ana tuhuma ya wizi na anachunguzwa na TAKUKURU eti anapewa uafisa elimu kata.

Tanga ni rushwa na rushwa ni Tanga. Mifumo imekua ya rushwa.

Ofisi ya afisa elimu ichunguzwe vizuri dhidi ya mwanamke huyo.
TAKUKURU nao watoe muelekeo wa fedha zilizoibiwa.

Pia TAKUKURU na afisa elimu sekondari wachunguzwe kwamba je wana maslahi gani katika mamilioni yaliyoibiwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Comrade Kinana usifanye makosa
Tuacheni Unafiki Tanzania nzima aliyenyanyasika sana ni huyu Bhoke wako tu? Kinana apiganie Haki na Usawa kwa Watanzania wote na siyo hawa Wachache.
 
Tuacheni Unafiki Tanzania nzima aliyenyanyasika sana ni huyu Bhoke wako tu? Kinana apiganie Haki na Usawa kwa Watanzania wote na siyo hawa Wachache.
Aliyetajwa ni miongoni mwa hao watanzania wote mkuu
Huyo ni mtanzania na anahaki zake kama binadamu
 
Sasa Kinana nae unamshtakia kuhusu rushwa[emoji23][emoji23], maajabu haya. Kinana nae ana kashfa kibao za kampuni yake ya clearing
Duu, umewaza kama Mimi, CCM hii iliyorudisha mafisadi kazini ili waendelee kulamba asali, Leo wanawezaje kusimamia uozo ambao upo hata kwao?
 
Sasa Kinana nae unamshtakia kuhusu rushwa[emoji23][emoji23], maajabu haya. Kinana nae ana kashfa kibao za kampuni yake ya clearing
Jiwe yeye alikua na kashfa za kuhonga nyumba za serikali kwa mahawala wake lkn alikua anajifanya ndiye jemedari wa kupambana na rushwa.

CCM Ni Ile Ile.
 

Jiwe yeye alikua na kashfa za kuhonga nyumba za serikali kwa mahawala wake lkn alikua anajifanya ndiye jemedari wa kupambana na rushwa.

CCM Ni Ile Ile.
Kinana anauthubutu atalifanyia kazi na wanajukwaa watapata mrejesho
 
Mkuu, kuna Kanuni, Sheria na Taratibu zinazoongoza Utumishi wa Umma, endapo katika kuacha kwake kazi kulizingatia hayo yote, Kinana hana uwezo wa hili, mengine hayo ya Rushwa sidhani kama atafukua makaburi.
Hapo hapo zitaangaliwa sheria na kanuni zilizokiukwa mkuu.
Ninashukuru kwa mawazo
 
Mkuu, kuna Kanuni, Sheria na Taratibu zinazoongoza Utumishi wa Umma, endapo katika kuacha kwake kazi kulizingatia hayo yote, Kinana hana uwezo wa hili, mengine hayo ya Rushwa sidhani kama atafukua makaburi.
Hapo hapo zitaangaliwa sheria na kanuni zilizokiukwa mkuu.
Ninashukuru kwa mawazo
 
Hapo hapo zitaangaliwa sheria na kanuni zilizokiukwa mkuu.
Ninashukuru kwa mawazo
Katika andiko lako umeonesha kuwa aliacha kazi yeye mwenyewe, kama angekuwa ameachishwa kazi bila kufuata Kanuni, Sheria na Taratibu, kuna Mamlaka za rufaa ambapo alitakiwa akate huko.
 
Wewe ndiye huyo bhoke, sijawahi ona mkurya anatishwa hadi kuacha kazi
 
Katika andiko lako umeonesha kuwa aliacha kazi yeye mwenyewe, kama angekuwa ameachishwa kazi bila kufuata Kanuni, Sheria na Taratibu, kuna Mamlaka za rufaa ambapo alitakiwa akate huko.
Ameacha kwasababu ya kunyanyaswa. Neno kunyanyaswa ni pana sana mkuu. Wewe shangaa afisa aliyeamua kuacha kazi kwa kunyanyaswa kisa tu amechokonoa maslahi ya chombo ya wakubwa.
Nadhani hapo umeshanielewa mkuu
 
Back
Top Bottom