Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 122,494
- 96,074
Katiba ip hiyo unayo zungumzia wewe?Humtakii mema JPM. Kwa mustakbari wa Ustawi WA nchi hii lazima kwa sasa awe mwenyekiti ili akibadili katiba ndipo aachie mwingine
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Katiba ip hiyo unayo zungumzia wewe?Humtakii mema JPM. Kwa mustakbari wa Ustawi WA nchi hii lazima kwa sasa awe mwenyekiti ili akibadili katiba ndipo aachie mwingine
Lumumba sasa kunateketea hali si shwari tena kila mtu anaondoka na ubao wakeHuwa wana nichekesha sana ...laiti wangejua...wasingalisema hivyo...
Wee kweli stroke, endelea kusubiri maendeleo yanakuja [emoji1] [emoji1] [emoji1]huyu jamaa hafai kanisani wala msikitini. Anataka kufisha ndoto za watanzania kua na Taifa lenye maendeleo?
Na hivi JPM anashinda humu JF, huyo jamaa aachie madaraka mapema kabla aibu haijamkuta.Nakubaliana na wewe Mkuu. Hawa akina Luhwavi na wenzake ndio wanaotia hofu kwa wanachama wazalendo kuwa Magufuli hafai. Kumbe wana yao mambo
Huyo anatumwa na vigogo tu na sio kwamba yuko peke yake.
Mkuu jamaa kawapiga za uso nini mbona umepanic sana ukweli mbaya sana mwambie mzee wako luhavi ajipange mahakama ya mafisadi inamhusu.Ila unapenda misifa sana, nadhani unatamani upate udc lakini umeshachelewa. Pole
Umempa ushauri mzuri sana alizoiba zinatosha huwezi kuwa unaiba kila siku halafu watu wasijue keshaisha lazima apigwe tu.Namuonea huruma baba wa watu Wamemtoa kafara na kumgombanisha na utawala huu! Ndio basi tena....JPM na mwendo kasi wenzake watamsambaratisha mbali sana!! Mzee Rajabu kila zama na kitabu chake! Pole sana! Ndio si-hasa hizo ulizochagua mwenyewe! Umekula imetosha sasa rudi chini upumzike!.....achia wenzako wasongeshe miaka 10 ijayo!
Ukiwa CCM sio fisadi. Ukitoka fisadikama alifuja pesa mbona mpaka leo hajafikishwa mahakamani? kweli CCM ni ileile mafisadi ni walewale
Gwajima alitAmka kwenye madhabahu wewe unatamka jf,kamanda siro uko wapi? Lizaboni mchochezi au kuna double STD kamanda?Wadau amani iwe kwenu,
Hivi karibuni, tumeshuhudia harakati kadhaa za baadhi ya wanasiasa wa ndani na nje ya CCM wakipaza sauti zao kutaka Rais Magufuli asiwe Mwenyekiti wa Chama hicho ili kumrithi Dr Jakaya Kikwete ambaye anatarajiwa kustaafu rasmi wadhifa huo Julai 23.
Awali kulikuwa na figisu figisu nyingi kuwa chama hakina fedha za kuendeshea Mkutano Mkuu ili tu lengo lao litimie. Thanks kwa jitihada zilizofanywa na Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti Bara Philip Mangula ambao wamehakikisha kuwa fedha zinapatikana na mkutano Mkuu unafanyika Julai 23.
Hata hivyo, tunapoelekea Julai 23, yapo Mambo kadhaa yanaendelea ndani ya CCM ambayo kwa hakika yanaweza kuvuruga utamaduni ambao imejiwekea wa kukabidhiana madaraka ya Uenyekiti pindi Rais anapomaliza muda wake. This time, zipo harakati za chini kwa chini zinazoendeshwa ili Kikwete aendelee kuwa Mwenyekiti na Magufuli abaki kwenye cheo cha Urais tu.
Binafsi baada ya kuona kuwa vuguvugu hilo linazidi, ikabidi niingie chimbo ili kumnasa anayeinjinia mkakati huo. Hakika nilichokibaini kinanishtua sana. Mchawi sasa kajulikana. Ni Rajab Luhwavi, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara ambaye ametwaa madaraka hayo tarehe 9 Julai 2015 mara Baada ya Mwigulu Nchemba kujiuzulu nafasi hiyo wakati wa mchakato wa kumpata Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM. Mtakumbuka kuwa Luhwavi alikuwa Msaidizi wa Rais kwenye Masuala ya Siasa kabla ya nafasi hiyo kumuachia Martin Shigela Julai 2015.
Hoja za Luhwavi kutaka Magufuli asiwe Mwenyekiti wa CCM ni za kitoto sana. kwamba, Magufuli hakijui chama na hivyo yeye pamoja na genge lake wanaamini kuwa atakiharibu badala ya kukiimarisha. Hofu yao imeongezeka hasa kutokana na (kwa mtazamo wao) teuzi alizofanya Rais mpaka sasa kutozingatia kigezo cha Ukada wa CCM.
Hofu nyingine ya Luhwavi ni kupoteza madaraka ndani ya CCM. Luhwavi anaamini kuwa ikiwa Magufuli atakuwa Mwenyekiti wa CCM, hatakuwa na wadhifa wowote ndani ya chama na kwamba hata hiyo nafasi ya Unaibu Katibu Mkuu ataipoteza.
Pia Luhwavi ana hofu kubwa ya kufikishwa Mahakamani kutokana na kufuja fedha nyingi zilizotengwa wakati wa kampeni. Inaelezwa kuwa Luhwavi alikihujumu chama kwa kupeleka fedha kidogo kwenye majimbo ya uchaguzi tofauti na ilivyoidhinishwa na chama. Inadaiwa kuwa kwa baadhi ya mikoa, fedha hizo hazikwenda kabisa na hivyo kufanya baadhi ya wagombea kujigharamia hali iliyochangia kushindwa kwao.
Nani anampendekeza Luhwavi awe Mwenyekiti wa CCM? Hili lipo dhahiri. Luhwavi anataka Jakaya Kikwete aendelee kwenye wadhifa huo. Matarajio ya Luhwavi ni kwamba, ikiwa Kikwete ataendelea kuwa Mwenyekiti wa CCM, atamteua yeye (Luhwavi) kuwa Katibu Mkuu kujaza nafasi ya Katibu Mkuu wa sasa Abdulrahman Kinana ambaye ametangaza kuachia nafasi hiyo baada ya Mkutano Mkuu wa Julai 23.
Mpaka sasa, Luhwavi amezunguka kwenye mikoa kadhaa ya Tanzania Bara kuhamasisha wajumbe wa Mkutano Mkuu wasiridhie hoja ya Magufuli kuwa Mwenyekiti wa CCM. Inasemekana kuwa mpunga wa kutosha umetembea kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu ili wamkwamishe Rais Magufuli.
Hata hivyo, inaonekana dhahiri sasa kuwa mkakati wa Luhwavi na Timu yake umegonga mwamba. Mwenyekiti wa sasa Jakaya Kikwete amesema hataongeza hata sekunde moja na kwamba dhamira yake ya kwenda kulala usingizi baada ya Magufuli kushinda Urais iko pale pale. Hana mashaka hata kidogo na Rais na anawabeza wale wanaodhani kuwa Magufuli hana uzoefu wa kutosha kuongoza chama. Kwamba, kama amechaguliwa kuwa Rais wa nchi, atashindwaje kuongoza chama?
Nani walio nyuma ya harakati hizo? Nitaendelea kuwajuza kwa kadri tunavyokaribia Julai 23. Stay with me. Niwapongeze tu na kuwatia moyo baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa mikoa ya Njombe, Iringa, Dar es Salaam, Tanga, Manyara, Kilimanjaro, Mbeya na Dodoma ambao wamenipa ushirikiano wa kutosha wakati ninafuatilia jambo hili mpaka mchawi amejulikana. Mikoa hii ni miongoni mwa mikoa ambayo Luhwavi alitembelea kufanikisha mkakati wake.
Katika IT neno ip lina maana yake ila nadhani hukumaanisha internet protocol. Kama ulimanisha neno "ipi" jibu lake ni ya nchi ambapo mgombea binafsi ataruhusiwa.Katiba ip hiyo unayo zungumzia wewe?
endelea na zile zako za kusubiri lowasa kua raisWee kweli stroke, endelea kusubiri maendeleo yanakuja [emoji1] [emoji1] [emoji1]