Kinga kwa Rais aliyeko madarakani na wastaafu ni kichocheo cha uvunjaji haki, Iangaliwe upya

Teh teh teh sisi tunao wawili tu tena kama waliohusika ni kipindi wapo huko kwenye chama cha majambazi. Sasa sipati picha huko CCM kama kuna mtu atabaki.
 
Nikisema Nduga ni taahira watu watakasirika former PMs so what? Si acha sheria ichukue mkondo wake? Kwa huyu kilaza ndugai yeye kazi yake ni kulinda watu alio karibu nao tu maslahi ya nchi zero! I command Curses against Ndugai!! Hili ni jipu baya kuliko yote!!
 
Tatizo uelewa wako ni mdg,

Issue zote za serikali iwe mikataba iwe nini,inapitia kwanza kwenye kikao cha makatibu wakuu wakishakubaliana huko linakuja kwenye baraza LA mawaziri ambapo raisi ni mwenyekiti na ndio signatory mkubwa,raisi akilikataa lile jambo haliwezi kupita au kutekelezwa na hiyo ni kwa mujibu wa katiba,sasa leo unaposema Sumaye au Lowassa wakamatwe basi ujue wakifika huko watasema walitekeleza malekezo ya raisi kwa mujibu wa katiba,sasa Ndugai lzm apige biti kwamba mkiwataja maraisi wastaafu mjue upande wenu wamo akimaanisha Sumaye & Lowassa ili wapinzani waogope kutaja maraisi wastaafu maana cha kitaumbuka hata kuanguka kabisa....

Sijui umenipata bwana mdg...?tumia akili zako kufikiria acha ushabiki kitoto,binafsi kizalendo nataka hao mawaziri wakuu wastaafu wapelekwe mahakamani uone ngoma itakavyonoga vizuri.
 
Second thought.......sidhani kama Mh.Spika kaongea maneno hayo.kuna clip ya kuthibitisha au HANSARD za bunge zinaonesha hayo maneno.
 
Wote tu waliohusika washtakiwe kama ni wa MACCM au waliohamia Chadema. Kama walihusika kwa namna moja au nyingine basi hakuna jinsi.
Wote wapotezwe, bila kujali itikadi ya sasa au zamani! Wa sasa na wazamani, wote wapotezwe! Wa richmond, dowans escrow; na waliouza nyumba za serikali kwa vei chee, wote wapotezwe tu. Tumechoka sasa tunasema basi, imetosha!
 
Usikwepe hoja.
Mkapa.
Kikwete
Sumaye
Lowasa.
Je upo tayari hiyo team yote ishtakiwe?
Hapo mtoto wa mkulima Pinda hachomoki, Warioba pia hachomoki. Acha washtakiwe hatia au hapana mahakama ndo itaamua..
 
washitakiwe hii katiba yetu haina tofauti na borgus treaty wa mjeruman
 
Swali hili nalielekeza kwenu wenye akili.
Je Lowasa anastahili kushitakiwa na yeye kwenye sakata la mikataba ya madini
Kama viongozi walio husika watafikishwa mahakamani??
Mana huyu alikuwa kiongozi wa ngazi ya Juu tena mtendaji wa serikali na msimamizi wa shughuli zote za serikali bungeni hivyo alibariki hii mikataba na kuipigia debe.
Tena alitetea hizi sera akiwa bungeni kipindi upinzani wakilalamikia hii mikataba ya kifisadi.

Je anastahili kuwajibishwa??

Mana hata magufuli pia analaaniwa kwa hili tena yeye alikuwa waziri tu.
Ila huyu Lowasa yeye ndo alikuwa waziri mkuu.
Je likoje hili???

Na je angekuwa ndio Rais na kutokana na uhusika wake je angethubutu kufukua haya???

Ahsanteni
 
Tuanze na Acacia kwanza....
Je lisu anaweza kutusaidia kuishtakia acacia MIGA?
 
lowassa aliahidi kuyafukua,sijui kama angeweza au asingeweza...
kufukua sio tatizo,tatizo ni umefukuaje,tusubiri mpaka mwisho wa hii picha ndio tutathmini vizuri,lakini tayari nimeshaona ubaguzi kwenye kuwajibishana!!!
 
Mkuu wanaomlani JPM wakati akiwa Waziri wa Kawaida wanajisahaulisha kuwa Lowassa's alikuwa PM kipindi hicho lakini kwa sasa Lowassa wanaye wanamuogopa kama ukoma kumtaja. Lissu Mnafiki sana anamtaja Kikwete halafu anaogopa kumtaja Lowassa sababu anajua akimtaja àtapigwa zengwe la kisiasa na atakuwa hana pa kukimbilia.
 
Huyuu spikaa ni wa hovyooo cjuii nimepatiaaa akitokea team mate wake anachangiaa mashudu na dakikaa anamuongezeaa lakini timu pinzan akizungumzaa hataa dakika 10 hazifiki na maneno ya mipashoo kibao yanii sahivii kaamua kabisa kujionyesha rangi yake halisii
 
Katiba ingemwondolea Rais kinga pengine akina BM na Jay kaka wangekuwa wanapiga selfie na Seya mida hii. Naota tu
 
Nataka kuwasiliana na mwanasheria wangu nione jinsi gani naweza kumfungulia mashtaka BM kwa kutukana. Na Fanya hivyo kwa niaba ya Watanzania tuliotukanwa.
Ila nijue kwanza, jee baada ya kukabidhi ofisi bado ana Kinga dhidi ya makosa ya jinai na madai?
Nataka niiombe mahakama pia izuie asilipwe pension yake kwa kuwaita hao wanaomlipa kwa kodi zao wapumbavu.
 
Kwa niaba ya joseverest
Kila la kheri

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…