Malinyingi naona unaandika vitu vya ajabu. Ukweli ni Ukweli tu na unatabaki kuwa ukweli tu. Lowassa ni Fisadi kabisa lakini bado ni mwanaCCM muaminifu kwa chama chake. CCM ilipaswa kufuata kanuni, taratibu na katiba yake katika kumwondoa Lowassa na sio kufanya uhuni kama ule.
Kuhusu Zitto ni kweli ni Msaliti kwa CHADEMA dhambi mbaya zaidi katika uaminifu lakini bado kanuni, taratibu na Katiba ya CHADEMA ilitumika kumfukuza.
Alichokisema Mzee Kingunge ndio ukweli wenyewe, na utabaki hivyo hivyo siku zote. Kama humpendi Mzee Kingunge hilo ni sawa, lakini jaribu kuupenda hata ukweli wake.