Kingunge: Mchakato wa kumpata Mgombea Urais CCM ulikuwa batili! Lowassa si fisadi kama inavyodhaniwa

Mnao mdharau Mzee Kingunge hamjui kitu na mpo kama bendera fuata upepo! Kingunge ni mzee makini sana na mnaofurahia jambo hili mtakuja jutia siku moja!
mbona hata viongozi wakuu wa ccm hawazungumzii tena ishu ya urais now wanadili na wabunge na madiwani
 
Mtu huhitaji kuwa na darubini kuona kwamba mchakato wa CCM ulikuwa wa kihuni na usio wa kidemokrasia.

Hao 33 waliokatwa walikatwa kwa vigezo gani? Walipigiwa kura?

Au walikatwa kwa uamuzi wa watu flani flani tu kwamba huyu na yule hawafai?

Licha ya kwamba Kingunge anaonyesha ni mnafiki lakini kwenye hoja yake ya msingi ana hoja.
 
Kama wenyewe hawajitendei haki unadhani watatenda haki kwa wengine jiulize! !?
Hapo jibu lake ni kuwa kwa wengine wanawafunga magoli ya mikono kwa kwenda mbele, kama ilivyo nukuu ya Nape kule pande ya Mwanza.
 
Sasa aone utamu wa kuvuruga taratibu na mchakato.

Kingunge ulishiriki kuvuruga mchakato wa katiba pendekezwa... Sasa usilalamike, muosha uoshwa.

Huyu kikongwe anapovuruga wananchi wengine anaona raha, yeye akivurugwa ana anza kulalamika. Atulie aone raha ya kuvurugwa.
 
Kingunge ni mnafiki mkubwa kwanza mwaka 2005 alikuwa kwenye kamati ya maadili lakini aliondolewa baada ya kuonyesha upendeleo wa waziwazi kwa JK lakini mwaka huo huo taratibu za kupiga kura zilibdilishwa kiasicha kumshangaza hata katibu mkuu Mang'ula lakini hakusema chochote kingunge alitaka kuwaaminisha watanzania bila yeye hakuna mtu anayewez kuwa rais ccm matokeo yake ameumbuka kingunge mwenyewe ni fisadi nani hajui kampuni ya mke wake ya parking ilipewa kazi wakati ilikuwa haijasajiliwa hata brela, nani hajui kampuni ya kukusanya ushuru ubungo ilivyokuwa inaiibia serikali na nani hajui motto wake anafanya biashara ya madawa ya kulevya kwa sababuameshaingia kwenye ufisadi ndio maana hawezi kupinga ufisadi,mwaka 1995 mtu aliyekuwa na nguvu alikuwa malecela lowasa hakuwa na nguvu yoyote ndio maana Nerere alitishia kurudish kadi mwissho ajue wakai wake umepita nio maana alishindwa hata kupata ujumbe wa halmashauri kuu kwenye uchaguzi
 
wanasiasa wengi wanchi hii bara na visiwani wapinzani ukiangalia historia yao wanatoka ccm
 
Makubwa haya, sasa ni dhahiri CCM vipande vipande.
It is very true Ntobi.

Ingawa walipotoka Dodoma walijifariji kwa kusema wanatoka Dodoma wakiwa more stronger kuliko walivyoenda.

Purely hayo ni maneno ya kujifariji sawa sawa na mgonjwa mahututi anayeendelea kuishi kwa kusaidiwa na mitambo ya kupumulia ya oxygen, akijipa matumaini ya kuishi miaka kadhaa ya mbele ambapo kiuhasia ni kuwa madaktari wakiamua tu kuzima mitambo hiyo ndiyo inakuwa the end of the story.
 
Huyu Kingunge aache double standard. Kwenye Mchakato wa Katiba alikwa tayari kukubaliana na CCM kuwaburuza Watanzania, leo hii kuburuzwa kunamhusu mtu wake Lowassa anaona CCM inafanya vibaya kuburuza mambo...Mkuki kwa nguruwe sio?

Kwanza kama alikuwa na nia ya kumsafisha Lowassa, kwa nini asubiri hadi wakati wa kugombea Uraisi, si angeanza kufanya hivyo mapema ili Lowassa angalau arudishwe kwenye Baraza la Mawaziri mapema kabla ya haya mambo ya uchaguzi mkuu?
 
Bado naamini wafuasi wa Lowassa hawana nguvuya kumtisha mwenyekiti wao na hawana ubavu wa kupiga kura za maruhani. Kama wangeweza basi wangeanzia kumpitisha mgombea dhaifu. Huo ubavu hawana kabisa.
 
Mzee kingunge,anataka nin sasa!Magufuli anakubalika zaid ya huyo amtakae yeye!
 

Una akili kuliko Shein
 
Last edited by a moderator:
Mwakyembe: (Kwenye Richmond saga bungeni) ... ombeni kanuni zitenguliwe ili tuwasilishe upya taarifa yetu ili tuseme na siri tuliyoificha ili kuikoa serikali isiporomoke yote..."

Kingunge:"Hadithi ya Lowassa kuwa ni fisadi haina mashiko, ilianza kwa kashfa ya Richmond. Kamati Teule ya Bunge iliundwa na kutoa taarifa za ovyo sana, na hatimaye kwa kulinda heshima ya serikali na chama akajiuzulu..."

 
Kingunge is just retiring the amount of money received from EL.

Kama anasema wananchi wamedharauliwa....mbona hakuwa mstari wa mbele kutetea maoni ya wananchi yaliyomo kwenye rasimu ya katiba? (Double standard)

Wanasiasa ni waongo sana....anafanya yote haya kumridhisha EL kuwa wapo pamoja ( moyoni hayupo hivyo)

Naupenda msemo huu " kunya anye kuku akinya bata kahara"......
 
Huyu mzee sije kuwa hii yote ni mwanzo wa kampeni mpya? Lowasa labda anataka kugombea kupitia chama tofauti na CCM na huu ndio wanzo wakumsafisha, haiwezekani kwa mwanasiasa mzoefu kama kigunge kuamua kufa na Lowasa. tumeona kwa kina Sophia walivyorudi mbio, Tusubiri soon tutasikia EL anapeperusha bendera ya ACT!
 


Kwenye hatua ya kwanza huwa hamna kupiga kura majina yote yanachukuliwa na kuangaliwa moja baada ya jingine na wale wote wenye tabia mbovu mbovu na ambao Tume ya maadili inaona hawafai huwa majina yao hayarudi, wale ambao majina yanarudi ndio hupigiwa kura sasa, nilivyoelewa mimi!
 
Sasa aone utamu wa kuvuruga taratibu na mchakato.

Kingunge ulishiriki kuvuruga mchakato wa katiba pendekezwa... Sasa usilalamike, muosha uoshwa.

Kweli kabisa....kula tano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…