Kadhi Mkuu 1
JF-Expert Member
- Feb 4, 2015
- 19,687
- 23,689
Kwanini ungoje upewe hiyo gun na Hamza? Nenda nawe kanyang'anye ya kwako uwashughulikie hao police.Wafe tu na midhuluma yao si wanajiona wenyewe miungu.Huyu jamaa angenipa hiyo gun moja tuwashughulikie vizuri
Ni tukio la kushangaza na lenye maswali mengi kwa sasa hivi hakuna ajuae Ukweli ngoja tusubiri taarifa ya jeshi la polisi.
Mpaka muda huu tayari ndugu wa Bwana Hamza wamechukulia wako polisi kwa mahojiano zaidi.
Lakini tujiulize
1. Hamza ni nani ?
2. Ni raia wa Nchi gani ?
3. Anafanya Kazi gani ?
4. Kama tukio hili tutaliweka kwenye kundi la Ugaidi tujiulize kwanini shumbulio lake liliwalenga Askari polisi pekee licha kuwa na nafasi ya kuwadhuru raia waliokuwepo karibu nae mfano kwenye Daladala.
4. Ukitazama vizuri baadhi ya video utaona jamaa alikuwa anashambulia na kukwepa (swali) mafunzo haya aliyapata wapi au tuseme ameiga kwenye Movie??
......................
Huo ni Upande mmoja wa maswali lakini Kuna upande mwingine umejaa tetesi kwamba huyu Bwana Hamza ana mgodi huku Chunya mkoani Mbeya ambao waliachiwa na Marehemu Baba yao. Tetesi hizi zinadai kwamba siku ya tukio Bwana Hamza alikuwa kwenye mipango ya kufanya Biashara ya Madini na suala hili Kuna maafisa wa jeshi la polisi walikuwa wanalijua sasa basi Kuna kitu cha ajabu Sana kikatokea na kukwamisha hiyo biashara. Ni kitu gani hicho ngoja kwanza jeshi la Polisi limalize Kazi yake May be litatueleza ukweli narudia tena May be.
**********
REJEA.
Nenda kwenye Post za Millard Ayo (Instagram) Kuna Dereva tax anaefanya shughuli zake karibu na nyumbani kwa Akina Hamza amekiri ni kweli Hamza na ndugu zake wengine waliachiwa Mgodi huku Chunya mkoani Mbeya na Marehemu Baba yao.
Lakini pia Kuna kipande cha ujumbe amekipost Le Mutuz nitakiweka hapa ili uunganishe matukio.
Swali la Mwisho. Hamza ni kichaa au ana tatizo la Akili ??
Siku chache zilizopita Kuna watu walikamatwa na Madini feki huko Dar es laam. Please hii nayo usiiweke mbali ukianza kuunganisha matukio
View attachment 1908534
Alivopora silaha akawaua hao police aliowapora silaha.? Hao walioporwa walikuwa wangapi na wameuawa wangapi.? Jumla ni Vifo vingapi kujumlisha na wale wanne waliouawa wakati wa kushambuliana.?Inasikitisha sana kwa askari kuporwa silaha ,askari inatakiwa ume active ,kama umeshika mtutu inatakiwa 20m mtu unammonitor anavyokuapproach,ukimuona haeleweki unamuamuru Hands Up akikaidi inapiga moja kwa hewa kisha ukimuona anataka kuchukua kitu mfukoni unawesha ya mguu kisha unamuattach fasta.
Polisi inabidi warudi mafunzoni,yaani jamaa anatamba dakika 30 nzima na askari wapo kibao wanaogopa,check baada ya jamaa kudongoka ndani ya dakika wakajitokeza askari kanzu wenye mitutu na wa mavazi kama 50 hivi,yaani inashangaza walikuwa kibao lakini walikuwa wanamuogopa jamaa mmoja tu.
Unayajua mazingira yaliyopelekea wao kuporwa hizo silaha?Inasikitisha sana kwa askari kuporwa silaha ,askari inatakiwa ume active ,kama umeshika mtutu inatakiwa 20m mtu unammonitor anavyokuapproach,ukimuona haeleweki unamuamuru Hands Up akikaidi inapiga moja kwa hewa kisha ukimuona anataka kuchukua kitu mfukoni unawesha ya mguu kisha unamuattach fasta...
Mkuu ugaid n mpana sana na usijiwekee mpaka katika mambo nyeti kama haya. Gaid ama ugaid haujawah taki kikubwa ila kama lililotokea. Kwa wakati wako jitahid kusoma sheria ya ugaidi pia kujifunza viashiria vya ugaid namna ugaid unavyopenya.pia na malengo ya magaidi.Inawezekana hilo pia
Ila Gaidi kaacha kushambulia Ubalozi na wananchi anawaambia ondokeni pia kuongea na yule mtoto na kuwaambia madereva waondoke na magari yao
Ugaidi upo ila hii sio mbinu za kigaidi labda iwe mbinu mpya...
Ameshuhudia ila mengne yanamaswali. Maana tulichokiona kwenye video na anachokisema kunasehemu vinakinzana na hii n kwa kawaida kwa binadamu kutaka kuonekana wameshuhudia kutoka mwanzo mpaka mwishoNipe majibu yako baada ya kuchunguza
Mjuba ata kufuatilia huwezi..unachosha watuAlivopora silaha akawaua hao police aliowapora silaha.? Hao walioporwa walikuwa wangapi na wameuawa wangapi.? Jumla ni Vifo vingapi kujumlisha na wale wanne waliouawa wakati wa kushambuliana.?
Hata Kama alidhurumiwa kitendo cha kushambulia polisi na kubeba silaha ya kivita alijiweka kwenye nafasi ya kushambuliwa pia
Hata kama madai yako ni kweli, je kuna haja ya kuchukua hatua za kipumbavu kama alivyochukua mwenzako huyu unayejitahidi kumtetea? Jicho kwa jicho wameliteketeza gaidi la kisomaliScenario inayosemwa ni kua zile silaha alinyang'anya maaskari baada ya kutaka kumwonea kimakosa , haya mambo yanafanyika sana hasa wale wanaitwa tigo wanaozunguka na pikipiki ni washenzi sana wale , hapo mtambambika kesi kua alishirikiana na gaidi walioko Zambia kwa sababu mnajua hawezi ongea lakini damu yake ita wa hunt mmoja baada ya mwingine na hamtatoboa !!
Siwachoshaje watu wakati bado cjapewa majibu ya maswali yangu.? Ingekuwa mtu amenijibu lkn bado nikaendelea kuuliza hapo ndo ungesema nachosha watuMjuba ata kufuatilia huwezi..unachosha watu
Jeshi la polisi wasibebane ktk hili inaonekana huyu Bwana kafanyiwa dhuluma na polisi ndio maana hakuwa na shida la Raia Bali polisi ili kulipiza kisasi. Ni polisi akina Nani hao wamemfanyia dhuruma? ...Ni muda Sasa Rais kumwondoa sirro na waandamizi wengine kulisafisha....Kama watu wanadhulumiwa na kuona solution Ni kupambana kwa risasi Basi tunajenga Taifa jipya kabisa.
Bogus kwenye ubora wakoNi jambo la kheri sana hawa Polisi wanaoitumikia CCM badala ya wananchi kuendelea kuuawa.Mungu bariki sana yule gaidi.
View attachment 1908590
View attachment 1908624
Wabongo tunaupiga mwingi kwenye kutoa ushahidiAmeshuhudia ila mengne yanamaswali. Maana tulichokiona kwenye video na anachokisema kunasehemu vinakinzana na hii n kwa kawaida kwa binadamu kutaka kuonekana wameshuhudia kutoka mwanzo mpaka mwisho
Bogus ni hawa Polisi waliokuwa wanataka kumpora bwana Hamza madini yake wakaishia kuuawa na Bwana Hamza pamoja na wewe unaeshabikia mifumo ya utoaji haki ambayo imeoza katika nchi hii.Bogus kwenye ubora wako
Mkuu wacha kutetea mapolisi...! Jamaa yuko kwenye cross fire lakini yanamkosa yanapiga chini, mengine yapo kwenye range kabisa jamaa anatembea wala hajifichi na yanamkosa! Risasi kibao zinapigwa kama hawana mafunzo π€¦π½ββοΈπ€¦π½ββοΈπ€¦π½ββοΈπ€¦π½ββοΈUnawalaumu bure tu!
Wewe ulitaka polisi wangapi ndiyo wapambane naye?
Hao polisi unaowalaumu walikuwa wanajua kila kitu kuhusu hatari iliyokuwepo? Walikuwa wanajua kuna mtu mmoja tu anayehatarisha usalama na hakuna wengine waliojificha sehemu?
This is so ridiculous.