Kiongozi Mwandamizi wa CHADEMA akutana na Kikwete, Kinana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa

Kiongozi Mwandamizi wa CHADEMA akutana na Kikwete, Kinana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa

Jitihada za kumaliza kesi ya ugaidi na uhujumu uchumi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mheshimiwa Freeman Mbowe, zinaendelea “nyuma ya pazia,” ambapo taarifa za uhakika zinaeleza kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika, amekutana na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Abdulrahman Kinana, na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Diwani Athumani.

Haijaweza kufahamika kama jitihada hizo ni za Mnyika binafsi au zina baraka ya chama hicho, ambacho kwenye mitandao ya kijamii kimetanabaisha kuwa hakitaki suluhu yoyote kuhusiana na kesi hiyo.

Taarifa hizo zinaeleza kwamba kimsingi Mama Samia Suluhu aliridhia ombi la kuachiwa kwa Mheshimiwa Mbowe na ilitarajiwa aachiwe kwa “nolle prosequi” (tamko la nia ya kutoendelea na mashtaka) ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) lakini “yaliyojiri kabla, wakati na baada ya mkutano wa vyama vya siasa huko Dodoma” yalipelekea mpango huo kukwama.

Licha ya jitihada hizo za Mnyika, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Masoud Othman nae aliwasilisha maombi ya Chadema kwa Mama Samia, na akashauri Mheshimiwa Mbowe aachiwe bila masharti yoyote.

Uamuzi wa Chadema kususia mkutano huo wa vyama vya siasa huko Dodoma ambao ulifunguliwa na Mama Samia, inatajwa kuwa moja ya sababu zilizopelekea kukwama kwa mpango huo wa kumwachia Mheshimiwa Mbowe.

Taarifa hizi zinakinzana na kauli zinazoongewa na viongozi na wafuasi wa chama hicho kuwa “hawako tayari kuomba Mheshimiwa Mbowe aachiwe” kwa sababu wanaamini kuwa hana hatia na mashtaka dhidi yake ni ya kutungwa.

Yawezekana tofauti hizo kati ya “kinachoendelea faraghani” na “kinachoongelewa hadharani” zikawa ni mkakati wa Chadema hasa ikizingatiwa kuwa wafuasi wengi wa chama hicho hawaafiki kabisa wazo la kuomba Mheshimiwa Mbowe aachiwe. Moja ya sababu zinazochangia “msimamo huo mkali” ni shinikizo la “wanaharakati wa mtandaoni” ambao wanapinga vikali siasa za maridhiano kati ya chama tawala CCM na vyama vya upinzani.

Hata hivyo, suala hilo la kesi ya Mbowe “limevamiwa” pia na kundi moja ndani ya CCM linalompinga Mama Samia, na ambalo linaiona kesi hiyo dhidi ya Mheshimiwa Mbowe kuwa yenye manufaa kwa kundi hilo kwa sababu inatoa taswira mbaya kuhusu Mama Samia.

Nihitimishe kwa kutanabaisha kuwa haitokuwa jambo la kushangaza endapo Mheshimiwa Mnyika atakanusha taarifa hizi kwa sababu “zinaweza kumletea tabu” katika chama chake.

Jumanne njema
And then akitoka mtaona kama atabadilika. Atawatukana hadi mkome kadri anavyoelekezwa na mabwana wa nje. Chadema ni mpango wa ubeberu. Mission yao ni kuindoa ccm madarakani ili kuanzisha serikali itakayokidhi mahitaji ya ubeberu wa nchi za magharibi.
Acheni mbowe apambane na kesi yake ya ugaidi mahakamani. Kama ushahidi unatosheleza ahukumiwe. Vinginevyo mahakama itamwachia.
 
Nimefurahi ulivyoripoti kwa mtiririko mzuri,nafikiri Kama uko CHADEMA si sehemu sahihi kwako, nakukaribisha chama tawala.
 
Nyie si ndo mnamtaka Samia afute kesi?

Sasa mmebadilisha mnasema Samia akamshauri DPP afute kesi?

Well, ushauri huo kampeni DPP nyie wenyewe!, maana hata Samia akimshauri DPP bado DPP kwa mujibu wa mamlaka yake bado anaweza kuukataa vilevile
Mtu anaposema case Ifutwe kwa akili zako fupi anakua amemaanisha utaratibu wa kufuta case usifuatwe?? Hiyo ni akili yako na uwezo wako wa kufikiri ulipo kufikisha

Kauli ya rais 'futeni case hiyo' ina initiate process halali za kisheria kufuta case , sio Kwamba basi tu wanaachiwa kiholela , process zenyewe n DPP kuandika hati anawapa mawakili wa Jamhuri wanaiwasilisha kwa judge

Au mahakama inatumia vifungu vya sheria kuachana na case hiyo manake nao mamlaka hayo wanayo pia
 
Hii ndio misimamo yenu "wapinzani" wa siku hizi.

Mnataka busara itoke kwa Lissu lakini hamtaki yule anayemshikilia Mbowe kinyume cha sheria awe na hiyo busara.

Kwa tabia yako huku jf na ulichozoea kukipigania, naijua motive behind inayokufanya umtetee "mwenzenu" hopless.

Siku hizi hupigi zile kelele zako tena kwasababu "mwenzako" ameshika hatamu, unafiki mtupu.
Mbowe hajafungiwa ndani ya vyumba vya Ikulu, yuko rumande chini ya uangalizi wa magereza, Tena kila siku Jaji ndiye anayesema arudishwe rumande mpaka tarehe fulani.
Tuiache mahakama ifanye kazi, Huenda Samia anatamani Mbowe aachiwe, lakini hawezi kuingilia uhuru wa mahakama!
 
kwa kesi kama hii, ma sheikh wa uamsho walikaa lupango kwa miaka ya kutosha ndani, kesii hii iendelee adi mwisho, after all kwenye kesi hii kuna watu wamepotezwa na hata maiti zao hazija patikana sijui na hili litapotezewa??
 
Mtu anaposema case Ifutwe kwa akili zako fupi anakua amemaanisha utaratibu wa kufuta case usifuatwe?? Hiyo ni akili yako na uwezo wako wa kufikiri ulipo kufikisha

Kauli ya rais 'futeni case hiyo' ina initiate process halali za kisheria kufuta case , sio Kwamba basi tu wanaachiwa kiholela , process zenyewe n DPP kuandika hati anawapa mawakili wa Jamhuri wanaiwasilisha kwa judge

Au mahakama inatumia vifungu vya sheria kuachana na case hiyo manake nao mamlaka hayo wanayo pia
Sasa naona unakubaliana na Zitto aliyesema kesi ifutwe kwa kufuata taratibu za kisheria.

Nyie mnaosema Samia afute kesi bila masharti mnakosea, Wacha sheria iamue kesi ifutwe au la
 
Jitihada za kumaliza kesi ya ugaidi na uhujumu uchumi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mheshimiwa Freeman Mbowe, zinaendelea “nyuma ya pazia,” ambapo taarifa za uhakika zinaeleza kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika, amekutana na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Abdulrahman Kinana, na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Diwani Athumani.

Haijaweza kufahamika kama jitihada hizo ni za Mnyika binafsi au zina baraka ya chama hicho, ambacho kwenye mitandao ya kijamii kimetanabaisha kuwa hakitaki suluhu yoyote kuhusiana na kesi hiyo.

Taarifa hizo zinaeleza kwamba kimsingi Mama Samia Suluhu aliridhia ombi la kuachiwa kwa Mheshimiwa Mbowe na ilitarajiwa aachiwe kwa “nolle prosequi” (tamko la nia ya kutoendelea na mashtaka) ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) lakini “yaliyojiri kabla, wakati na baada ya mkutano wa vyama vya siasa huko Dodoma” yalipelekea mpango huo kukwama.

Licha ya jitihada hizo za Mnyika, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Masoud Othman nae aliwasilisha maombi ya Chadema kwa Mama Samia, na akashauri Mheshimiwa Mbowe aachiwe bila masharti yoyote.

Uamuzi wa Chadema kususia mkutano huo wa vyama vya siasa huko Dodoma ambao ulifunguliwa na Mama Samia, inatajwa kuwa moja ya sababu zilizopelekea kukwama kwa mpango huo wa kumwachia Mheshimiwa Mbowe.

Taarifa hizi zinakinzana na kauli zinazoongewa na viongozi na wafuasi wa chama hicho kuwa “hawako tayari kuomba Mheshimiwa Mbowe aachiwe” kwa sababu wanaamini kuwa hana hatia na mashtaka dhidi yake ni ya kutungwa.

Yawezekana tofauti hizo kati ya “kinachoendelea faraghani” na “kinachoongelewa hadharani” zikawa ni mkakati wa Chadema hasa ikizingatiwa kuwa wafuasi wengi wa chama hicho hawaafiki kabisa wazo la kuomba Mheshimiwa Mbowe aachiwe. Moja ya sababu zinazochangia “msimamo huo mkali” ni shinikizo la “wanaharakati wa mtandaoni” ambao wanapinga vikali siasa za maridhiano kati ya chama tawala CCM na vyama vya upinzani.

Hata hivyo, suala hilo la kesi ya Mbowe “limevamiwa” pia na kundi moja ndani ya CCM linalompinga Mama Samia, na ambalo linaiona kesi hiyo dhidi ya Mheshimiwa Mbowe kuwa yenye manufaa kwa kundi hilo kwa sababu inatoa taswira mbaya kuhusu Mama Samia.

Nihitimishe kwa kutanabaisha kuwa haitokuwa jambo la kushangaza endapo Mheshimiwa Mnyika atakanusha taarifa hizi kwa sababu “zinaweza kumletea tabu” katika chama chake.

Jumanne njema
Mleta mada mbona hujiamini? Unaandika taarifa ki woga woga.
 
Sasa naona unakubaliana na Zitto aliyesema kesi ifutwe kwa kufuata taratibu za kisheria.

Nyie mnaosema Samia afute kesi bila masharti mnakosea, Wacha sheria iamue kesi ifutwe au la
Hata kama tusipokubaliana na Zitto, hayo yanabak kua mawazo yetu ila uhalisia n kwamba ukishaingia kwenye mkono wa Sheria iwe kihalali au sio kihalali , utatoka kwa utaratibu wa kisheria hilo liko wazi

Manake kama mahakama ikikuachia ikasema hauna hatia , ni baada ya kutafsiri sheria na kukuta huna kosa.. inatumika Sheria kukuachia , same thing na ukikutwa na cosa

Hata hati ya DPP inafuata utaratibu wa Sheria , lazima kwenye hati aambatanishe vifungu na vitu vingine kukidhi matwaka ya kisheria uweze achiliwa

Hii wote tunafahamu , sema n vile tu ni nature ya binadamu kubisha
 
Huijui serikali vizuri mzee, Mbowe ni takataka tu, Aliuawa MKURUGENZI WA TAIFA MSTAAFU KISA KUMSHABIKIA MREMA, SEMBUSE HUYO CHIZI WENU MAKENGEZA MBOWE?? Hivi nyie mkisikia SERIKALI ina mkono mrefu huwa mnaelewa nini??
Ndio najua leo hii. Kumbe yule Mkurugenzi ilikuwa sababu ni kumshabikia Mrema!!! Hebu weka namba zako za Simu na Jina halisi UTUJUZE ZAIDI HAYO MADINI
 
Back
Top Bottom