Kiongozi Mwandamizi wa CHADEMA akutana na Kikwete, Kinana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa

EU wanakuja na Spana Tani arobani hakuna namna ni kunyoosha mikono juu....
Hivi walidhani wale wazungu wanatania? Yaani walivyo wajinga waliona EBU parliement wanavyoongea kwa utulivu na sio kama Bunge la akina Msukuma na Gambo wanaongea kwa kupayuka na varangati juu wakadhani imeisha.

Hii ngoma haijaisha mpaka kieleweke
 
Huijui serikali vizuri mzee, Mbowe ni takataka tu, Aliuawa MKURUGENZI WA TAIFA MSTAAFU KISA KUMSHABIKIA MREMA, SEMBUSE HUYO CHIZI WENU MAKENGEZA MBOWE?? Hivi nyie mkisikia SERIKALI ina mkono mrefu huwa mnaelewa nini??
una laana si bure
 
Kuna kitu kinaitwa "capital letter". Kuna tofauti kati ya "l" na "r". Mwisho, katika jamii yetu wazee ni watu wa kuheshimiwa na sio kubezwa. Mtu mzima akitaka kuongea na wewe, si rahisi kumkatalia.

Amandla...
 
Amka dogo kumekucha
 
Punguani mkubwa.
Mbowe tangu lini ukasikia akitukana.
Unadhani ni yule kichaa wenu mwendazake?
 
'Wasiohusika' ndio 'Wahusika' na Wahusika ndio wasiohusika
Wana mtandao wamerudi kwa kasi,haya mambo yasingewezekana enzi za mwendazake, yaani badala ya kumuona mhusika wanaonwa wasiohusika!
 
 


Haina ubishi wanufaika wakubwa wa siku 100 za kwanza za Rais SSH ni CDM, Mbowe na Mdude kwa maelekezo, falsafa na haiba ya Samia. Mpaka tukaandika threads nyingi za kusema "Mama anaupiga mwingi

Ningetegemea Mbowe na Lissu watumie busara katika madai yao kwa kuwa wasikivu na wavumilivu pale Samia aliposema suala la Katiba lisubiri ajenge uchumi

On the contrary Mbowe na Lissu wakaanza kumfokea Rais kama vile ni mbunge wa BAWACHA?? Na Mdude akasema " nitamnyoa mama yenu kwa wembe uleule nilio mnyolea mtangulizi wake

Nini kikiwapata hawa watu ambao kwa Mwendazake waliufyata miaka 5. Mwendazake kawapiga risasi, kavunja Bilicanas na kavunja na mashamba yake, kamchukulia na fedha kwenye akaunti. Hajawahi hata kulalamika

Samia kamrudishia akaunti, kesi zao za kubambika zikapigwa chini pamoja na ya MDUDE. Halafu wao ndiyo wa kwanza kusema HATUWEZI KUMBEMBELEZA Samia
 
Mama alitoa hivyo vyote kama hisani au rushwa??! Na Mbowe anaonewa ili kuonesha makucha na mapembe ya mama? Usitutukanie mama yetu! Suala ni moja tu, kama anahusika ni kosa, kama hahusiki ajitabainishe!
 
Wana mtandao wamerudi kwa kasi,haya mambo yasingewezekana enzi za mwendazake, yaani badala ya kumuona mhusika wanaonwa wasiohusika!

hao si ndio wanaongoza nchi kwa remote. mradi imefika huko wakiridhia hata kesho anatoka
 

Ujinga wako uko hapa:

"Haijaweza kufahamika kama jitihada hizo ni za Mnyika binafsi au zina baraka ya chama hicho"

Kwani Mnyika kakutana mwenyewe? Kwa nini jitihada hizo haziwezi Kuwa zimefanywa na:

  • Ccm
  • Kinana
  • Jk
  • Serikal
  • Diwan
 
Chahali ni Team Kikwete , yuko kundi moja na Steve Nyerere , alikuwa ana ugomvi na Magufuli tu kama Mange

ugomvi wa chahali na magufuli ni kama ule ule ugomvi wenu na magufuli.
tofauti yenu na chahali nyinyi mmejificha kwenyw siasa.

wote nyinyi ni watu wa maslahi tu.
 
Wasipo omba msamaha inakuuma nini
 

Mkuu kuna points katika unayosema. Lakini kinachotushangaza baadhi yetu ni harakati zinazoshika kasi za kutaka Mbowe na CHADEMA wamuombe msamaha Rais SSH (hadharani) ili afute kesi hiyo ya ugaidi na Mbowe kuwa huru. Ni kama vile SSH anataka sana kuifuta hiyo kesi (almost desperate)!

Kwanza, kuna dharura yoyote au umuhimu mkubwa kiasi hicho kwa SSH kesi hiyo ikifutiliwa mbali?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…