Kipande cha SGR Morogoro to Makutupora 61%

Kipande cha SGR Morogoro to Makutupora 61%

Corticopontine

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2019
Posts
666
Reaction score
1,277
PICHA: Kazi za ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro – Makutupora, Dodoma (KM 422) zinaendelea ambapo Ujenzi wa kipande hicho umefikia 61%.

Ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa unatarajiwa kuwekwa mifumo ya kisasa ambayo itamdhibiti mwendeshaji wa Treni kutovuka spidi iliyowekwa.

====

IMEELEZWA kuwa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), unatarajiwa kuwekwa mifumo ya kisasa ambayo itasaidia kuzuia ajali ambazo zinaweza kujitokeza wakati wa uendeshaji wa reli hiyo na ambao hautamruhusu dereva kuzidi ama kupunguza mwendo uliowekwa.

Hayo yamesemwa na Meneja Msaidizi wa mradi wa reli ya Kisasa, kipande cha Morogoro - Makutopora (Km 422) kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC), Mhandisi Christopher Mang’wela, wakati akizungumza na wahandisi kutoka Serikalini na Sekta Binafsi ambao wametembelea mradi huo uliofika asilimia 61, jijini Dodoma, kwa ajili ya kujifunza utekelezaji wa mradi kuanzia hatua mbalimbali zilizotekelezwa.

“Kama mnavyoona, mradi umefika asilimia 61, na uendeshaji wake utakuwa ni wa kisasa kwani utawekwa vifaa maalum vya kumuongoza dereva wa treni ili kuzuia ajali.” amesema Mhandisi Mang'wela.

Awali, akizungumza kwa niaba ya wahandisi hao, Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), Mhandisi Patrick Barozi, ameeleza kuwa anaona nia ipo na uwezo kwa watanzania katika kusimamia miradi mikubwa inayoendelea nchini huku tukiwa na usimamizi mdogo kutoka wenzetu wa nje na hivyo kuwaleta wahandisi wetu katika mradi kutaongeza chachu ya kuchukua zabuni nyingi za miradi mikubwa inayoatarajiwa kuanza na kuendelea hapa nchini.

"Tumetembelea mradi huu katika baadhi ya maeneo ambapo tumeridhishwa na mradi huu na tumeona unaendeshwa vizuri kuanzia mwanzoni hadi hapa ulipofika kwani kupitia mradi huu wahandisi wamejifunza mengi", amefafanua Mhandisi Barozi.

20210525_024043.jpg
 
PICHA: Kazi za ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro – Makutupora, Dodoma (KM 422) zinaendelea ambapo Ujenzi wa kipande hicho umefikia 61%.

Ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa unatarajiwa kuwekwa mifumo ya kisasa ambayo itamdhibiti mwendeshaji wa Treni kutovuka spidi iliyowekwa.
Hii sio legacy ... Hii ni kumbukumbu.. Kuna tofauti kubwa kati ya legacy na memory

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa sisi watanzania tunashangaza sana tunapojaribu kumponda rais mmoja na kumshabikia mwingine. Wote wanaitekeleza ilani ya CCM, wote hao wanatekeleza malengo yale yale.

Rais Samia aliposema yeye na hayati ni kitu kimoja maana yake ni utekelezaji wa sera zile zile, mikakati ile ile. Ni kichekesho sana kumsimanga rais mmoja na kumpongeza mwingine, kufanikiwa kwa mmoja ni kufanikiwa kwa mwingine kushindwa kwa mmoja ni kushindwa kwa mwingine.

Wangekuwa ni marais wanaotoka vyama tofauti hapo hizi hoja za kishabiki zingeweza angalau kuwa na mashiko.
 
Ni kweli kabisa.Mradi shirikishi wa Viongozi wawili wa Awamu ya Nne na Tano.

Hakuna jipya hapo .Uishe tuutumie mana kila siku tunapandisha na kushusha % za mradi kuisha.
 
Navyofahamu wako mnao.

lalamikia hiyo legecy ila hakuna anae ongelea isiwepo kwani huwa yenyewe haipigiwi promo ila inajionesha tu.

Alafu hiyo ni kumbukumbu sio legecy na ni miradi iliyoko kwa hela za wananchi

Ni wajibu wake kutekeleza kwa usahihi kodi zetu kwenye matumizi ila ukisema ni kazi ya mtu mmoja unakosea na ndo maana amefariki ila ujezi unaendelea.

Hivyo kinachofanya kazi ni hela zetu sio mtu mmoja
 
PICHA: Kazi za ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro – Makutupora, Dodoma (KM 422) zinaendelea ambapo Ujenzi wa kipande hicho umefikia 61%.

Ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa unatarajiwa kuwekwa mifumo ya kisasa ambayo itamdhibiti mwendeshaji wa Treni kutovuka spidi iliyowekwa.
Kujenga reli ya njia moja karne hii halafu unaiita supermodern SGR ya mwendo kasi ni udanganyifu na upotevu mkubwa wa fedha za maskini. Reli za njia moja zilijengwa hapa nchini na Wajerumani mwaka 1910!
 
PICHA: Kazi za ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro – Makutupora, Dodoma (KM 422) zinaendelea ambapo Ujenzi wa kipande hicho umefikia 61%.

Ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa unatarajiwa kuwekwa mifumo ya kisasa ambayo itamdhibiti mwendeshaji wa Treni kutovuka spidi iliyowekwa.

Una uhakika na Unachokisema kuwa Ujenzi ni 61% maana mimi naishi sehemu moja wapo ambako hiyo reli itapita bado hawajaanza hata kurundika Maudongo ambayo yataweka Mazingira ya Reli kuwa juu,sasa hapa ni nje ya Dodoma sijui huko mbele zaidi!
 
Huenda hujui wanapongezwa ama kupondwa katika nini.
 
PICHA: Kazi za ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro – Makutupora, Dodoma (KM 422) zinaendelea ambapo Ujenzi wa kipande hicho umefikia 61%.

Ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa unatarajiwa kuwekwa mifumo ya kisasa ambayo itamdhibiti mwendeshaji wa Treni kutovuka spidi iliyowekwa.
Nadhani utekelezaji wa hii miradi ya kimkakati iko kwenye ilani ya chama inawezaje kuwa ni legacy ya mtu?
 
Nadhani utekelezaji wa hii miradi ya kimkakati iko kwenye ilani ya chama inawezaje kuwa ni legacy ya mtu?
Hata kuhamia Dodoma ilikuwa kwenye ilani ya chama tangu mwaka 1978.
 
PICHA: Kazi za ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro – Makutupora, Dodoma (KM 422) zinaendelea ambapo Ujenzi wa kipande hicho umefikia 61%.

Ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa unatarajiwa kuwekwa mifumo ya kisasa ambayo itamdhibiti mwendeshaji wa Treni kutovuka spidi iliyowekwa.
Wakiloni walijenga, bandari (tunayijivunia leo) viwanja vya ndege (tunavyovikarabati leo), Reli (tunayoiboresha leo, barabara (tunazoboresha leo) , viwanda (vilivpuawa na serikali ya ccm). lakini bado tuliwasema vibaya. mwendazake ni nani asisemwe?
 
Ukimponda Kikwete inabidi umponde Mkapa.

Ukimponda Samia inabidi umponde JPM.

Ukimsifu Nyerere msifu pia na Mwinyi.

Wote ni watekelezaji wa ilani ya Chama kimoja.
Ilani ambazo zimeshindwa kuwapatika watanzania maisha bora aka maendeleo ya watu - watanzania hawa bado wapo kwenye lindi la umasikini mkubwa huku wakipambana na wale maadui watatu ambao Rais wa kwanza Nyerere (Umaskini, Maradhi na Ujinga) aliwataja miaka takribani 60 iliiyopita.

Hizi naongelea ni ilani za uchaguzi za CCM katika awamu tofauti tofauti.
 
Huwa sisi watanzania tunashangaza sana tunapojaribu kumponda rais mmoja na kumshabikia mwingine. Wote wanaitekeleza ilani ya CCM, wote hao wanatekeleza malengo yale yale.

Rais Samia aliposema yeye na hayati ni kitu kimoja maana yake ni utekelezaji wa sera zile zile, mikakati ile ile. Ni kichekesho sana kumsimanga rais mmoja na kumpongeza mwingine, kufanikiwa kwa mmoja ni kufanikiwa kwa mwingine kushindwa kwa mmoja ni kushindwa kwa mwingine.

Wangekuwa ni marais wanaotoka vyama tofauti hapo hizi hoja za kishabiki zingeweza angalau kuwa na mashiko.
Mkuu wengi wana matatizo ya kujifunzia siasa mtandaoni.
 
PICHA: Kazi za ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro – Makutupora, Dodoma (KM 422) zinaendelea ambapo Ujenzi wa kipande hicho umefikia 61%.

Ujenzi wa Reli hiyo ya Kisasa unatarajiwa kuwekwa mifumo ya kisasa ambayo itamdhibiti mwendeshaji wa Treni kutovuka spidi iliyowekwa.

Hivi mnataka nini hasa nyie MATAGA? Hii hela ilikua ya mama yake?
 
Back
Top Bottom