Kipi hutakisahau mwaka 2019?

Kipi hutakisahau mwaka 2019?

Namshukuru Mungu huu mwaka nimeimarika zaidi kiroho kuliko miaka ya nyuma. Kwani nimeijua dini kwa usahihi na Mungu kunionyesha karama yangu. nafurah sana kumtumikia Baba wa mbinguni.

Namshukuru Mungu huu mwaka nimeweza kujinasua ktk kifungo, kifungo ambacho sikuwah kutegemea km nitatoka lkn nimetoka na ninaenjoy sana tu.

Namshkr Mungu huu mwaka umekuwa na mapito ya kila aina kilio, furaha na maumivu lkn mwisho umekuwa ni neema. Hakika umekuwa ni mwaka wenye changamoto sana.

Namuomba Mungu mwaka 2020 uwe wa neema zaidi, furaha, amani na niweze kutimiza malengo yng niliyojipangia.
 
2019 ndio mwaka nilio elimika zaidi kuliko miaka yote
 
Ajali ya ungo anga la chato
Habarini JF members,

Maisha ya mwanadamu yana vipindi vya furaha na huzuni, chochote kati ya hivyo viwili kinaweza kubaki katika kumbukumbu ya maisha kutokana na kilivyomuumiza/kumfurahisha.

Huu uzi naomba tushee visa/mikasa/wonderfull moment happened in 2019.

N.B Kuna mafundisho mengi sana kwenye mapito ya binadamu mwenzako.

WELCOME 2020!

Sent using Jamii Forums mobile app

Jr[emoji769]
 
Pole sana kwa hayo yatupasa tushukuru kwa kila jambo hakika Mungu ni mwema .
Ni mwaka ambao nimepita katika kila Aina ya vipindi.

Kiroho Ni mwaka nilioimarika Sana,MUNGU alinionyesha kipawa(karama yangu) na baada ya hapo nimepita sehemu ngumu Sana.
Ni mwaka niliopitia magumu mengi,Hadi kuna muda unafika nakata tamaa lakini bado MUNGU ananiambia nisimame.

Familia yangu imepita kwenye misukosuko Sana ila sikuchoka kuomba.

Ni mwaka ambao nimepata marafiki,
Wengine niliwaacha waende maana hawakujua umuhimu wa urafiki wangu na kujitoa kwangu,
Wengine bado nashirikiana nao katika kila Khali.
Hawa wote naomba baraka za Mungu ziwe juu yao.

Ni mwaka ambao rafiki yangu wa karibu(yumo humu) ameondokewa na Mama yake mzazi..hii Ni Jana tu.

Yote Yote kwa yote namshukuru Sana MUNGU.
Ametuagiza tushukuru kwa yote mema na mabaya.
Yeye Ni MUNGU na atabaki kuwa Mungu

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
2019 imekuwa rough sana kwangu binafsi na familia yangu kwa ujumla, pengine ni mwaka niliotoa machozi mengi kuliko mwaka mwingine wowote. Tumekutana na mambo makubwa ambaya hatujawahi kuyashuhudia. Lakini naamini Mungu ni mwema yatakwisha

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole Sana Mungu atarejesha palipovunjika 2020

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom