Kipi kilisabisha mkachapwa Darasa zima kipindi unasoma?

Kipi kilisabisha mkachapwa Darasa zima kipindi unasoma?

Dah darasa la saba nikikumbuka walikuja walimu ambao walikuw ni wanajeshi baada ya kubadilishwa kwa mkuu wa shule akaja huyo mbibi ndo akaleta sijui hao vijana wake oya sio poa ukisikis WIFA WINYA WIFA WILOLA sio poa walivokuja wakasema mnakubali kushilikiana wauni tukajibu Ndiooooo ndioooooo ndiooiooo darsa zima jumla ya wanafunzi 203 yani hakuna A B wala C wote katik class 1 tulipangwa kama tupo ofisini vile na tukafit na wale wajeshi sasa kumbe bila kujua tulisaini mkataba na mashetani ilikuwa akifeli mmoja katika maksi za chini darasa zima kazi mnayo ndio maana ya ushirikiano kwa hiyo wale vichwa wa class ambao walikiw waoga wa bakora wakawa wakisoma na kuelewa vizuri na mwalimu hayupo class basi wanapigisha class wakati huo monitor na monitress wako serious minuno empire 45 awachekeshi 👺👺 kuangalia noise maker na wasumbufu ulikuw ukikamatwa aiseee umeisha maana wale wajeshi wanahakikisha matizi yote ya JWTZ, FBI na SWAT yanaangukia kwako mpaka inafika miezi 6 ivi darasa letu kwa mara ya pili ikawa bright sana tulifaulu wote ispokuwa wawili tu mmoja alkuw na matatizo ya akili na mwingne alipata mimba ila nae alifaulu ila nikikumbuka wale walimu walikuwa wakipeleka mioto sio poa na nakumbuka kuna hiyo siku kuna mwanafunzi mwenzetu aliropoka serikali za mitaa pale kuwa walimu wamehifadhi zaidi ya bakora 100 nyuma ya mlango wa darasa kesho yake ambao wale wakaguzi wa manispaa sijuibwalivokuja hawakukuta kitu na sisi tukabisha kusema nani aliyesema kikaturamba class nzima tena ila mpk tulivowazoea ilkuw tunapass A za maana tukawa washkaj na wale walim
 
Nakumbuka alikuwa mwalimu wa phyz aliita wanafunzi kama wa4 wakajibu swali pale mbele, asa mm nikawa natafuna zangu karatasi ili nimpige nalo mtu, wakat namtupia mtu hilo karatasi kati ya wale walioko pale mbele si mwalimu likampiga mdomoni mwakee😂 asa mwalimu alivyo mjinga akachagua upande lilipotokea lile karatasi akaacha ule upande wangu nlipokuwa, na alieniona n demu flan na hakusema na alikuwa upande wa mwalimu aliouchagua, aloooh!!! Walikula mbokoooo kama nne nne hv, ila mimi Aaah!😂😂😂🙌
 
Nlikua form 2 afu Ni wiki moja twende likizo ubao wa darasa ulipakwa mafuta kisa hatutaki kusoma nahatumtaji aliefanya hivyo. Basi tukala viboko class nzima. Cha ajabu kesho yake madarasa yote yalifanya Kama sisi
 
Wakati tuko darasa la 7 miaka hiyo watu wanasoma huku tayari wameota ndevu na mavuzi, mjinga mmoja akamuandikia barua ya kumtongoza mwalimu mkuu halafu hakuweka hata jina lake ila alitaja darasa analosoma......kilichofuatia ilikuwa ni kama vile mateka wa ki Israel tumepelekwa kambi ya kijeshi huko Hamas
nyie hakika mlichezea kwa kuzingatia itifaki ya viboko
 
Back
Top Bottom