Kipi kinakukera katika elimu ya tanzania?

Kipi kinakukera katika elimu ya tanzania?

Mengi tu, inshort yanatia hasira,

Sijui serikali yenu inategemea nchi itaendeleaje

Wakati wanaineglet secta muhimu kama elimu


Kama huna hela basi hutopata elimu bora, je maskini watasoma kweli???
 
Mimi kinachonikera ni taasisi kama IFM,TIA&IAA kutoa degree mpaka masters wakati sio vyuo vikuu
Zile ni taasisi za Elimu ya juu zenye hadhi ya kutoa hadi Doctor of Philosophy mfano ni "Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (Nelson Mandela African Institute of Science and Technology) ambayo imenza na Masters na Doctor of Philosophy na hawana kabisa mpango wa kuwa bachelor. Sasa wewe nini kinakukera!
 
Kingine kinachonikera ni tutorial assistant kufundisha bachelor
 
hapo wanakosea sana

Kinachonikera mimi ni kokomoana kwamba umefeli form 4 kwa sababu say utoto ulikuwa mwingi ukaamua kujiendeleza kwa mfano ukaanza na certificate then diploma kwa lengo la kusoma elimu ya juu baadae.Kinachoudhi ni kwamba unapoenda kuomba kusoma degree badala waangalie diploma wanakurudisha nyuma na kuangalia cheti cha form 4 na kukwambia huna sifa.Jamani kama wanaangalia vyeti ili kupima uwezo wako wa kumudu kozi husika sasa hiyo diploma nimepataje kama sina uwezo? Hiki ndio kinachonikera na mpaka leo hii sijui motive ya hii kitu.
 
Mi kinachonikera ni mwalimu wa ngazi ya cheti na diploma kuwa aliyefanya vibaya kwenye mtihani wa kidato cha sita na cha nne
 
watoto wengi wanaomaliza 4m 4 na 4m 6 ni wa kizazi cha mulugo
 
Kinachonikera, Mlugo kuwa Naibu wazir wa elimu ambaye ni mtu asiyejua historia ya nchi ya Tanzania na elimu yake ni kuunga unga alafu Rais wa nchi anamkadhi wizara nyeti ya elimu.
 
Back
Top Bottom