Kinachonikera mimi ni kokomoana kwamba umefeli form 4 kwa sababu say utoto ulikuwa mwingi ukaamua kujiendeleza kwa mfano ukaanza na certificate then diploma kwa lengo la kusoma elimu ya juu baadae.Kinachoudhi ni kwamba unapoenda kuomba kusoma degree badala waangalie diploma wanakurudisha nyuma na kuangalia cheti cha form 4 na kukwambia huna sifa.Jamani kama wanaangalia vyeti ili kupima uwezo wako wa kumudu kozi husika sasa hiyo diploma nimepataje kama sina uwezo? Hiki ndio kinachonikera na mpaka leo hii sijui motive ya hii kitu.