Kipindi cha Mkasi kimefikia tamati!!??

Ngonepi

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2013
Posts
1,872
Reaction score
1,207
Waungwana wa huku naamini mambo mengi sana mjini kwetu Dsm mna ufahamu nayo!

Nilikuwa na shabiki sana wa Salama jabir na kilichokuwa kipindi cha Mkasi pale Eatv, sasa katika hizi siku za karibuni naona matangazo ya kitu ninachodhani ni dada kuja na kipindi kipya kiitwacho Ngazi kwa ngazi palepale Eatv kila alhamis.

Wajuvi mnieleweshe, inamaana MKASI ndio ushavunjika tena! Na vipi hiki kipindi kipya bado kitakuwa cha yuleyule founder AY!?
 
Wamefanya modification... Wanakuja na NgaziKwangazi
 
Naona Salama anakuja na kipindi kipya kila alhamisi saa tatu usiku, amekiita ngazi kwa ngazi, inaweza kuwa mkasi imesambaratika tayari.
 
Ameshawahoji macelebrity wote wa bongo so kipindi kimeisha
 
Mbona unauliza maswali ambayo majibu yake utayapata siku ya alhamis na j3?!
Kama mkas umevunjika automatic j3 hutokiona hicho kipindi
 
Super star Le Mutuz hata mimi sijawahi mtazama akihojiwa Mkasini!!

Sasa hapa kusema washahojiwa mastar wote nakataa!!
 
Bongo kuna star gani? Hebu watajeni. Sema kuna watu maarufu kina kingwendu, wemasepenga, wolper nk
 
salama yupo juu sana kusema ukweli watangazaji wabongo wanaopenda kufanya interview waige kwa huyu mwana dada.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…