Kipindi Tunamtafakari Dewji, Naomba atujibu Maswali Haya

Kipindi Tunamtafakari Dewji, Naomba atujibu Maswali Haya

Kama moyo wake ni mdogo basi atachukua moyo wa tembo maana hakuna namna, maana nasikia moyo wa tembo ni mkubwa kama ndoo.
 
Simba Sports Club Haiwezi kuuzwa kwa mtu.
SImba sio Kampuni yenye shares .Imesajiliwa kama Club au association . Haikusajiliwa BRELLA.
Ni club ilosajiliwa na wadhamini , iko chini ya trustees kwa niaba ya wanachama na wapenzi wa timu hio nchini na nje ya nchi.

SUALA : Jee unaweza kuithamini Club ya Simba ? na ukapata thamani yake halisi ili uweze kupata bei ya kuipiga bei ? Jawabu ni Hapana huwezi kui value Timu hii . Simba na Yanga zinakaribia zaidi ya Miaka 100 sasa. Hazijawahi kufa , wala hakuna uwezekano wa kufa ,sana zitashuka daraja na kupanda lakini the brand ipo .

Thamani ya Simba ni priceless .You can?t Value it therefore No body can buy it ?imejengwa miaka mingi ni Zaidi ya Vyama vya siasa amabavyo no body can buy vyama vya siasa,
Unapouza Simba sasa kwa akina Aveva , who are they ? wao ni viongozi tu wenye dhamana ya kuiongoza Simba sio Beneficiary wa Club hii, wanaweza kuondoka na hata kuingia yanga?

Nani beneficiary wa hizo 20 billion ? jee kuinunua yenyewe ni kuingiza kwenye programya Maendelo ? au ndio wanunuzi ni kina Aveva waloikuta Simba juzi ? au ni wajukuua wa waswahili wale waloanzisha hii timu Kutoka Sunderland mpaka ilipo fikia ? nani atafaidika na hizo 20b/ akale nwatoto wake kama jasho la kuwa mwanzilishi na mmiliki halali wa Simba ?
Kwa ufupi Simba hai uziki haina shares inamilikiwa na wanachama chini ya wadhamini wao. washabiki wote wana haki ka club hii.

Jiulize unaweza Kuiuza au kuinunua CUF au CCM ? kama hapana basi Simba ni Hapana mara 100 maana ni zaidi ya CUF na CCM.

Unaweza kuinunua Azam , Muundo wake ni Tofauti ni Kampuni inayomilikiwa kwa share.
Vyenginevyo Unaweza Kujenga MO sports club yako , ukafanya MO Academy , Chamanzi kule viwanja vinapatikana. Aige mfano wa Azam au TP Mazembe au Mtibwa .
lakini ukweli na kisheria No body can buy a club belong to more than 30 million fans ndani na nje ya Tanzania . Simba ipo Tanzania , Ipo Zanzibar , Ipo UK ,UAE,OMAN,USA,SCANDINAVIA nk nk . Simba ni Taifa Kubwa its Big enough for any tycoon to buy it ?Brand yake its worth Trillions of Dollar ni kubwa kuliko any company Tanzania?
Wana simab don?t feel or think too Low ?you have build one the greatest club in Africa.
Simba inahitaji Uongozi imara , wanao penda Football, wenye vision wasio mafisadi pia. Simba ikiwa imara na viongozi madhubuti Company nyingi zitakua tayari kui sponsor kwa mikataba minono ya kuiendesha club hio kwa mafanikio makubwa katika soka..

Viongozi waache hayo mawazo kabisa simba ni kubwa kuliko wao hii club haizuki na hawana uwezo wa kisheria kufanya hivyo. huo,
Wenye Simba haswa Tuliwazika zamani nao walituachia hizi club kama urithi wetu ambao sasa kina Aveva wanafikiria kuuza kwa maslahi binafsi

Asante Mkuu.. Naamini wahusika wamekusikia.
 
Tatizo simba Ina wapenzi tu ila sio wanachama hai Kama kila mwaka hao unaosema wanachama 5mil wangekuwa wanapilia tu kadi zao za uwanachama kiasi cha elfu tano tu kwa mwaka embu Fikiri wangekuwa wanapata sh ngapi ila tatizo sisi porojo nja porojo

Nadhani hao wapenzi hawajaelimishwa vya kutosha juu ya umuhimu wa kuwa wanachama.. Wakati muafaka wa kuwaelimisha na kuwahamasisha zaidi wapenzi na wanachama umuhimu wa kuwa na kulipia kadi zao.. ni sasa.
Nasema ni wakati muafaka kwa sababu,
1. Timu inafanya vizuri katika ligi
2. Ile nguvu moja imerudi.. tofauti na msimu uliopita.
Ndg. Aveva.. mda ndiyo huu.
 
Wakati sisi tunajadili Mo kuwekeza sijui kununua % ngapi,TP Mazembe inazidi kuwaadabisha waarabu na kuleta sifa ukanda Wa chini ya jangwa LA sahara shangwe hiyo ikiambatana na kumpata kinara bora Wa ufungaji Wa mabao CAF champions league kijana Mbwana Samatta,nimesikia fahari kuangalia Aljazeera sports news wakitamka jina la kijana wetu Sammatta.
LA msingi Simba na Yanga wakilenga mikakati madhubuti inawezekana kufikia mafanikio ya TP Mazembe,wapiga deal wakiacha ufisadi.
 
Wapiga dili wa Msimbazi hawataki kabisa kusikia habari ya uwekezaji na umiliki wa timu kwa mtindi wa hisa...Bado miaka 50 mbele ndo Timu za Yanga na Simba zitazinduka....MPIRA PESA au hamuelewi maan ya msemo huu?..Leo TP Mazembe inafanikiwa kwa sababu ya umiliki wa mtu binafsi kama Moise Katumbi....
 
Kasema simba hataki faida sababu ana biashara zaidi ya mia zinampa faida,yeye anataka timu ifanikiwe na mashabiki(akiwemo yeye) wapate raha.

Huyu jamaa ashawahi kuidhamini simba miaka ya 2000 nakumbuka na ilifanya vizuri sana kipindi kile.
Kasema? Na wewe ukamuamini...

Anachotaka kuifanyia Simba kwanini hakuifanyia Mbagala Market? Simba iliwahi kufanya vizuri, ila aliyenufaika zaidi ni MO kutokana na kutangaziwa bure bidhaa zake za Safi, MeTL achilia mbali dili za kijanja alizodaiwa kufanya akiwa na simba.
 
Kidigitali kivipi.. mbona unabwabwaja bila fact? Nakuona umechanganyikiwa na bilioni 20 anazotaka kuwekeza.

Simba S.C ikiiuza jezi 2m kwa 10,000/= tu inapata billion 20... hela anavyotaka kuwekeza huyo Mo.. Kumbuka Simba S.C inawanachama zaidi ya 5m.. na hii ni kwa Tanzania pekee.


Narudia tena kama Mo ana uchungu wa kweli.. tunamkaribisha tena katika Bodi ya wadhamini.. na si kumuuzia Timu.

NB: Thamani ya Simba S.C ni mara 10 ya 20 bilioni.

Mkuu hebu punguza hizi porojo zako sidhani kama wanachama wa Simba wanafika hata 100,000 na hapa bongo hao mashabiki wengi wananunua hizo jezi feki.Kuna haja ya kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa hizi klabu otherwise usitegemee maendeleo yeyote
 
Mkuu hebu punguza hizi porojo zako sidhani kama wanachama wa Simba wanafika hata 100,000 na hapa bongo hao mashabiki wengi wananunua hizo jezi feki.Kuna haja ya kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa hizi klabu otherwise usitegemee maendeleo yeyote
Mkuu tatizo la Watanzania hatupo business minded. Bado tupo katika zama za ujima kutegemea misaada, wafadhili, donations I mean term yoyote ile utakayotumia. Mwaka 1994 Mengi aliposhauri Yanga iendeshwe kibiashara wajinga wajinga walimjia juu hawakumwelewa na nina uhakika hawaelewi alichosema hadi sasa. Tunaogopa mabadiliko tunadhani timu ikiendeshwa kibiashara, ikununuliwa eg Dewji anavyotaka ni kwamba haitakuwa Simba tena , vizee visivyoweza hata kununua karanga havitakuwa na cha kuongea, kujivunia, yaani akili zetu zipo porini porini. Tunashindwa kuangalia na kuelewa kwa nini vilabu vikubwa afrika(TP Mazembe, Kaizer Chiefs etc) South America, na ulaya vinavyojiendesha na bado vina wapenzi sugu kuliko hata sisi ushuzi maharage. Nakumbuka hayati Mziray alisema pindi Simba na Yanga zikifa basi kuna watu wengi Dar es salaam pia watakufa kama nzi, sasa nakubali na hili. Mwanzilishi wa mada hii ambaye ni mpenzi wa Simba anathibitisha msemo huo wa hayati Mziray. Bottom line Mfumo wa uendeshwaji ndio kikwazo kikubwa kwa mafanikio ya vilabu vyetu.
 
Simba msimuuzie huyo Mo timu yenu mtaja chekea choloni, shauri yenu!
 
Huyu ni DEWJI aliyekuwa mbunge wa singida mjini?? Au yupi

Km ni huyo muulizeni ana viwanda vingapi kati ya dar na singida

Ana viwanda vingapi kati ya morogoro na singida

Ana viwanda vingapi kati ya singida na mwanza

Jibu ni kwamba amejenga viwanda sehemu ambako hakuwahi kuwa mbunge

Alisaidia timu gani ya singida angalau ikaingia hata nane bora kwenye harakati za kupanda daraja

Huyo mhindi aache utapeli..muhindi wa kuaminiwa Tanzania ni yule anayegombea ubunge pale Ilala peke yake hawa wengine ni ujinga mtupu
Acheni wivu wa kike team mmeshindwa kuiendesha kwa kukosa akili acheni watu wenye akili wawekeze
 
Mkuu tatizo la Watanzania hatupo business minded. Bado tupo katika zama za ujima kutegemea misaada, wafadhili, donations I mean term yoyote ile utakayotumia. Mwaka 1994 Mengi aliposhauri Yanga iendeshwe kibiashara wajinga wajinga walimjia juu hawakumwelewa na nina uhakika hawaelewi alichosema hadi sasa. Tunaogopa mabadiliko tunadhani timu ikiendeshwa kibiashara, ikununuliwa eg Dewji anavyotaka ni kwamba haitakuwa Simba tena , vizee visivyoweza hata kununua karanga havitakuwa na cha kuongea, kujivunia, yaani akili zetu zipo porini porini. Tunashindwa kuangalia na kuelewa kwa nini vilabu vikubwa afrika(TP Mazembe, Kaizer Chiefs etc) South America, na ulaya vinavyojiendesha na bado vina wapenzi sugu kuliko hata sisi ushuzi maharage. Nakumbuka hayati Mziray alisema pindi Simba na Yanga zikifa basi kuna watu wengi Dar es salaam pia watakufa kama nzi, sasa nakubali na hili. Mwanzilishi wa mada hii ambaye ni mpenzi wa Simba anathibitisha msemo huo wa hayati Mziray. Bottom line Mfumo wa uendeshwaji ndio kikwazo kikubwa kwa mafanikio ya vilabu vyetu.
Hamna haja ya kuenda mbali kuangalia mfano wa TP Mazembe. Azam ni mfano tosha. Akiwekeza hizo billion 20 hata kwa Lipuli, itafika mbali
 
Nyie ndo mlikua mnategemea kusomesha watoto zenu na kununua magari na ela za club sasa mnaona mtakufa njaa mor akichukua timu ona leo mmeumbuka Aveva anahamisha ela ya club kwenye account yake binafsi hata aibu hamuoni shame on you
 
Back
Top Bottom