Kiranga anatoa sadaka na anaamini stori za majini lakini haamini uwepo wa Mungu

Kiranga anatoa sadaka na anaamini stori za majini lakini haamini uwepo wa Mungu

Huo ni uhuru wake kuamua ulimwengu uweje.
Sijakataa kwamba huo ni uhuru wake.

Nimekuuliza, kwa nini kaumba ulimwengu ambao unaruhusu mabaya, wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Inaonekana hata wewe hujui jibu.

Unaamini Mungu ambaye humuelewi.

Huwezi kumuelewa.

Kwa sababu, hayupo. Ametungwa tu na watu.

Huwezi kumuelewa Mungu ambaye hayupo na habari za kuwapo kwake zinajipinga.
 
Sijakataa kwamba huo ni uhuru wake.

Nimekuuliza, kwa nini kaumba ulimwengu ambao unaruhusu mabaya, wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

Inaonekana hata wewe hujui jibu.

Unaamini Mungu ambaye humuelewi.

Huwezi kumuelewa.

Kwa sababu, hayupo. Ametungwa tu na watu.

Huwezi kumuelewa Mungu ambaye hayupo na habari za kuwapi kwake zinajipinga.
Nimeshakujibu hili swali lako kwamba tayari ameuumba ulimwengu ujao usiokuwa na mabaya. Uwezo anao na ndio ameamua hivyo kwenye mali yake. Hakuna wa kumpangia.
 
Nimeshakujibu hili swali lako kwamba tayari ameuumba ulimwengu ujao usiokuwa na mabaya. Uwezo anao na ndio ameamua hivyo kwenye mali yake. Hakuna wa kumpangia.
Unaweza kuthibitisha ulimwengu huo usio na mabaya upo na si hadithi za uongo tu?

Mbona kama unataka kuthibitisha uongo mmoja ambao hauthibitishiki kwa kutumia uongo mwingine ambao hauthibitishiki?

Nakuuliza uthibitishe uwepo wa Mungu, unashindwa, unaleta habari za ulimwengu mwingine ambao hauthibitishiki.

Na kwa nini aruhusu mabaya kwenye ukimwengu huu?

Anapenda kuona mabaya yanavyoendelea?
 
Hiyo ina maana anaruhusu ubaya utokee, maana alimuona shetani kabla hajamrubuni mwanadamu, na bado akamuumba na kumpa uwezo mkubwa sana wakumrubuni mwanadamu. Halafu mwisho wa siku akamuadhibu mwanadamu akiyemuumba akijua atarubuniwa na shetani aliyemuumba yeye.

My head is spinning.

Anyway kwa kifupi mimi si kwamba siamini kama Mungi yupo, ila mimi nina imani yangu binafsi juu yake ambayo haifanani na ya dhehebu lolote.
Mkuu me ningependa kujua wewe unaamini katika njia ipi/Mungu yupi maana vile unauliza maswali kuhusu Mungu ni kama vile huamini katika uwepo wake, ila cha ajabu ni kwamba wewe pia unaamini kuwa yupo, Naomba unisaidie kuelewa vile wewe unaamini juu ya uwepo wake
 
Unaweza kuthibitisha ulimwengu huo usio na mabaya upo na si hadithi za uongo tu?

Mbona kama unataka kuthibitisha uongo mmoja ambao hauthibitishiki kwa kutumia uongo mwingine ambao hauthibitishiki?

Nakuuliza uthibitishe uwepo wa Mungu, unashindwa, unaleta habari za ulimwengu mwingine ambao hauthibitishiki.

Na kwa nini aruhusu mabaya kwenye ukimwengu huu?

Anapenda kuona mabaya yanavyoendelea?
Mabaya ni yapi? Unajuaje hili ni baya na hili ni zuri?

Nimeomba unipe metrics zitakazotumika kupima usahihi wa namna ya kuthibitisha uwepo wa Mungu na haujajibu.
 
Ungejuaje mema bila kuyatambua mabaya? au huoni hapo umepewa uhuru wa kuchagua
Wewe unaongelea ulimwengu huu uliopo, ambao una mema na mabaya.

Mimi nakurudisha Mungu alivyokuwa anaumba ulimwengu, hakuna mema, hakuna mabaya, Mungu ndiyo anaamua jinsi ya kuumba.

Alishindwa kuumba ulimwengu ambao hauna mabaya, una mema tu na watu hawawezi kufanya mabaya, wanafanya mema tu.

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu huo?

Ukiniukiza ningejuaje mema bila mabaya, una maana Mungu angetaka nijue mema bila mabaya kuwapo angeshindwa?
 
Hiyo ina maana anaruhusu ubaya utokee, maana alimuona shetani kabla hajamrubuni mwanadamu, na bado akamuumba na kumpa uwezo mkubwa sana wakumrubuni mwanadamu. Halafu mwisho wa siku akamuadhibu mwanadamu akiyemuumba akijua atarubuniwa na shetani aliyemuumba yeye.

My head is spinning.

Anyway kwa kifupi mimi si kwamba siamini kama Mungi yupo, ila mimi nina imani yangu binafsi juu yake ambayo haifanani na ya dhehebu lolote.
Mkuu,

Kwa nini hii contradiction ya "the problem of evil" inayofanya kichwa chako kizunguke ni rahisi sana mimi na wewe kuiona, halafu watu wengine wengi wanakuwa kama hawaioni?

Ni uzembe wa kufikiri tu au nini?
 
Mabaya ni yapi? Unajuaje hili ni baya na hili ni zuri?

Nimeomba unipe metrics zitakazotumika kupima usahihi wa namna ya kuthibitisha uwepo wa Mungu na haujajibu.
Mimi hata siendi kwa vipimo vyangu.

Mimi nafanya "immanent critique".

Tuseme nakubaliana na wewe Mungu yupo (for the sake of argument, tupate sehemu ya kuanzia).

Na katika kukubaliana nawe hivyo, nakubaliana kwamba mambo ambayo kwa mujibu wa maelezo yako ya uwepo wa Mungu yamesemwa, ni kweli.

Kwa mfano, dhambi zipo na ni mbaya, kuua, kuiba, majanga, ni mambo mabaya.

Sasa nakuuliza, ili nipate kumuelewa vizuri huyu Mungu.

Mmesema huyu Mungu ana uwezo wote, ujuzi wote, upendo wote.

Kwa nini hakuumba ulimwengu huu uwe ambao mabaya hayawezekani, watu waishi na mazuri tu?

Ukijibu kuna ulimwengu huo mbinguni, hilo si jibu, mimi siulizi kama kuna ulimwengu usioruhusu mabaya, nauliza kwa nini hakuumba huu usiruhusu mabaya.

Mungu ambaye anaruhusu mabaya yasiyo idadi yaendelee miaka nenda rudi kwa kisingizio kwamba kuna ulimwengu unaokuja hautaruhusu mabaya atakuwa mkatili sana.

Ukisema katupa uchaguzi wa mabaya na mazuri, hilo si jibu, sijakataa kwamba katupa uchaguzi wa mabaya na mazuri, nauliza kwa nini kaachia mabaya yawezekane wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
 
Mkuu,

Kwa nini hii contradiction ya "the problem of evil" inayofanya kichwa chako kizunguke ni rahisi sana mimi na wewe kuiona, halafu watu wengine wengi wanakuwa kama hawaioni?

Ni uzembe wa kufikiri tu au nini?
Nyie atheist mnaamini kwenye kupasuka kwa utupu kwa bahati tu ndio ulimwengu huu ambao uko systematic and uniform ukatokea. Inashangaza mnapowazia evil and good wakati standard yenu ni bahati nasibu.
 
Nyie atheist mnaamini kwenye kupasuka kwa utupu kwa bahati tu ndio ulimwengu huu ambao uko systematic and uniform ukatokea. Inashangaza mnapowazia evil and good wakati standard yenu ni bahati nasibu.
Hujui hata atheism ni nini.
 
Mimi hata siendi kwa vipimo vyangu.

Mimi nafanya "immanent critique".

Tuseme nakubaliana na wewe Mungu yupo (for the sake of argument, tupate sehemu ya kuanzia).

Na katika kukubaliana nawe hivyo, nakubaliana kwamba mambo ambayo kwa mujibu wa maelezo yako ya uwepo wa Mungu yamesemwa, ni kweli.

Kwa mfano, dhambi zipo na ni mbaya, kuua, kuiba, majanga, ni mambo mabaya.

Sasa nakuuliza, ili nipate kumuelewa vizuri huyu Mungu.

Mmesema huyu Mungu ana uwezo wote, ujuzi wote, upendo wote.

Kwa nini hakuumba ulimwengu huu uwe ambao mabaya hayawezekani, watu waishi na mazuri tu?

Ukijibu kuna ulimwengu huo mbinguni, hilo si jibu, mimi siulizi kama kuna ulimwengu usioruhusu mabaya, nauliza kwa nini hakuumba huu usiruhusu mabaya.

Mungu ambaye anaruhusu mabaya yasiyo idadi yaendelee miaka nenda rudi kwa kisingizio kwamba kuna ulimwengu unaokuja hautaruhusu mabaya atakuwa mkatili sana.

Ukisema katupa uchaguzi wa mabaya na mazuri, hilo si jibu, sijakataa kwamba katupa uchaguzi wa mabaya na mazuri, nauliza kwa nini kaachia mabaya yawezekane wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?
Nikupe mfano rahisi sana kuufikiria japo unaweza usiwe sahihi sana kumfananisha na alichofanya Mungu.

Kwa mujibu wa maelezo yako hapa jf ni dhahiri unafanya kazi wallstreet, Marekani. Je Unafikiri ni sahihi mimi kukwambia kwanini unafanya kazi huko na sio Cameroon? Sina haki ya kuuliza hilo kwasababu hayo ni maamuzi yako.

Sasa Mungu ambaye ni mkuu sana ameumba ulimwengu kwa namna anavyotaka. Sio sahihi kumuuliza kwanini umeumba ulimwengu hivi na sio vile. Ni mali yake. Anaamua atakavyo.
 
Wewe unaongelea ulimwengu huu uliopo, ambao una mema na mabaya.

Mimi nakurudisha Mungu alivyokuwa anaumba ulimwengu, hakuna mema, hakuna mabaya, Mungu ndiyo anaamua jinsi ya kuumba.

Alishindwa kuumba ulimwengu ambao hauna mabaya, una mema tu na watu hawawezi kufanya mabaya, wanafanya mema tu.

Mungu alishindwa kuumba ulimwengu huo?

Ukiniukiza ningejuaje mema bila mabaya, una maana Mungu angetaka nijue mema bila mabaya kuwapo angeshindwa?
Bado haujanijibu kwamba hao watu watajuaje wanayofanya ni mema wakati mabaya hawayatambui?
 
Bado haujanijibu kwamba hao watu watajuaje wanayofanya ni mema wakati mabaya hawayatambui?
Kwa nini kutambua hili ni jema kuwe muhimu kuliko kufanya jema?

Unataka kuniambia kwamba, kati ya ulimwengu A ambao, watu hawajui jema ni lipi, kwa sababu hakuna mabaya, wanafanya mema tu, na ulimwengu B ambao watu wanatambua mema na mabaya, na wanafanya mabaya, ulimwengu B ni bora zaidi ya ulimwengu A?
 
Kwa nini kutambua hili ni jema kuwe muhimu kuliko kufanya jema?

Unataka kuniambia kwamba, kati ya ulimwengu A ambao, watu hawajui jema ni lipi, kwa sababu hakuna mabaya, wanafanya mema tu, na ulimwengu B ambao watu wanatambua mema na mabaya, na wanafanya mabaya, ulimwengu B ni bora zaidi ya ulimwengu A?
Utajuaje umepika wali mbichi kama hujawai pika ulioiva?

Kwanza niambie kati ya ulimwengu A na B unaona sehemu gani wako huru zaidi..?
 
Utajuaje umepika wali mbichi kama hujawai pika ulioiva?

Kwanza niambie kati ya ulimwengu A na B unaona sehemu gani wako huru zaidi..?
Kwani Mungu ameshindwa kupika wali ulioiva bila kupika wali mbichi?

Kwa nini uhuru uwe muhimu zaidi ya kuondoa uwezekano wa mabaya?

Nikisema wewe ni baba, una mtoto wako mchanga uwezo wake wa kuchagua ni mdogo, anaweza kushawishika kuchagua kitu kibaya badala ya kizuri.

Situation A.

Una uwezo wa kufanya nyumba yako iwe na maziwa tu, mtoto akinywa chochote apate virutubisho vya maziwa.

Situation B

Na pia, una uwezo wa kuweka maziwa na sumu sehemu nyiingi nyumbani kwako, mtoto wako awe na uhuru wa kuchagua maziwa ama sumu. Akinywa maziwa aishi, akinywa sumu afe.

Hapo unatakiwa kuchagua A au B.

Wewe kama baba mwenye uwezo huo, ujuzi huo na mapenzi kwa mwana wako, utachagua A au B hapo?
 
Back
Top Bottom