OLESAIDIMU
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 19,139
- 9,562
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaani kuna watu utadhani wanaishi mochware....huu uzi umetisha, khah!
in addition LL.B
Ni degree yenye heshima kuliko zote duniani
The Bachelor of Laws, imetoka Latin ikimaanisha : Legum
Baccalaureus or LL.B. ni first professional
degree in law, depending on jurisdiction, hii The "LL." of the abbreviation for
the degree imetoka ktka genitive plural legum (of
lex , law). inayotengeneza abbreviation for a plural,
especially from Latin, mara nyingi inafanyika by
doubling the first letter (e.g. "pp" for "pages"),
thus "LL.B." stands for Legum Baccalaureus in
Latin . It is sometimes erroneously called
"Bachelor of Legal Letters" to account for the
double "L". nna imani umepata picha, keep it up.
Binafsi ni wakili na sababu ya Wanazuoni wa Taaluma ya Sheria kuitwa "Wasomi" ni mfumo tuliorithi kutoka kwa Mwingereza wa kuwaita wanasheria "learned brother/sister". Hili tunafundishwa kwenye somo linaitwa Legal Ethics tunaambiwa moja ya majukumu ya ethical practice ni kuheshimu na kutambua taaluma ya mwanazuoni mwenzako na tunawaita wasomi kama moja wapo ya recognition.
2. Kweli taaluma ya Law kwa sasa imepoteza ile heshima ya miaka ya nyuma ila sababu ni kuwa huko nyuma kwanza generally wasomi walikua wachache (katika fani almost zote), halafu Taasisi pekee iliyofundisha sheria ilikua moja tu (UDSM) baadae wakaja Mzumbe, then kulikua na kasumba kua Law ni fani ngumu, mwisho kabisa pia kuna ile "kasumba" ya Wanasheria kujivunia mno fani yao kua ni most Elite & Intellectual course ingawa mimi siamini hivyo.
Kwa sasa wasomi wa sheria ni wengi sana, vyuo pia vingi.
3. Anayesema sheria ni fani bora kuliko zote hii haijakaa sawa. Dunia ya leo inahitaji mjumuiko wa wataalam mbali mbali kufanikisha mambo. Sisi wanasheria tunawahutaji sana Forensic detectives kwenye kusolve criminal issues, tunawahitaji sana wahasibu na wakaguzi kuendesha biashara zetu (law firms), tunawahitaji sana madaktari kuweka afya zetu sawa tuweze kustand trial, tunawahitaji sana mainjinia atlist tuweke mawasiliano sawa na wateja wetu na kwa wakat.
Katika Kilatini kama neno liko katika wingi linafupishwa kwa kuiandika hiyo herufi mara mbili. mfano LL inamaanisha Laws, pp ni ufupisho wa pages in Latin
Teh teh teh teh hivi ODILI SAMALU unajua hesabu? Unajua integration?
Nakubaliana name jibu lako LA kwanini wanaitana learned brothers... nijekweli kwa mujibu Wa legal ethics
Hawa yuuu???!!!
Ayuu lenedi????!!!
Am faini senkyu ticha
Ai yam eduketedi in pabliki afeazi
Siti dauni!!!!!!
Senkyu fo yua introdaksheni...neksti!!!!!
Vijana wa first year hao mkuu achana nao wamefundishwa kuwa arrogant coz law is a noble profession. Wakija mtaani ndio watajua kuwa law is just like any other profession.
Huyo wa PSPA anaemdiss ndiye atakua boss wake endapo ataajiriwa na akiwa law firm asidhani within a year atakua tayari na gari kali.
...i'm a lawyer na ninakubaliana na wewe kuwa umeongea fact
...I'm a lawyer na ninakubaliana na wewe kuwa umeongea fact
Senkyu ticha
My kidumu endi mfagio izi at homu
Legum Baccalaureus meaning Bachelor (Bacca) of Legal (Legum) Science (Laureus). Ni Kilatini/kirumiLL.B ina L mbili lakini!!
Legum Baccalaureus meaning Bachelor (Bacca) of Legal (Legum) Science (Laureus). Ni Kilatini/kirumi
Damn! This was me 10 years ago? 🤣🤣Ni mkorofi kiasi, siyo sana. Hivyo hujakosea kabisa, umepatia kiasi.
Haya, twende kazi, ,mstari kwa mstari, hoja kwa hoja, na hata viroja kwa viroja.
Hilo ni kweli na ninakiri kuwa nilikosea katika kuuliza. Lengo langu halikuwa kuhoji ukweli wa wingi wa wasomi kati ya zama hizi na zile za zamani.
Kwa hiyo upo sahihi, kwamba zamani wasomi wa fani zote nchini Tanzania walikuwa wachache.
Hapo kwenye perceptions nilinuia kulenga zaidi kwenye taaluma ya sheria kupoteza heshima yake ya miaka ya nyuma (kama ulivyodai wewe) kulinganisha na hivi sasa.
Ndo sababu ya mimi kuuliza kuwa ni kweli hiyo taaluma imepoteza heshima au ni perceptions tu za watu? Hivyo hapo nakubali kosa, ilinipasa niwe mahsusi zaidi katika swali langu.
Mbona hata mimi sijasema kuwa wewe umesema kuwa sheria ni ngumu! Kama ukituliza hisia na kurudi tena kusoma kwa utulivu nilichokiandika nadhani utakubaliana nami kuwa hicho nilichokiandika kilikuwa kinaunga mkono mtazamo wako huo.
Nadhani hapo umepaniki bure tu pasipo hata na sababu yoyote ile ya msingi. Hebu rudi tena upasome hapo nilipoandika mimi na ambapo wewe umepanukuu.
Mimi mimeandika kwa mtindo wa rhetorical question ambapo dhumuni lilikuwa ni kuunga mkono kile ulichokiandika wewe kuhusu kasumba ya ugumu wa masomo ya sheria na sikuuliza kwa dhumuni la kutaka kujibiwa.
Aaah sasa miye mbeba maboksi na kusomea sheria wapi na wapi bana? Sijawahi hata siku moja kudai humu kuwa nimesomea sheria mimi. Sina uwezo wa kiakili wa kuwa kaka msomi kama ulivyo wewe na wengineo. Nimeishia kidato cha nne tu mimi.
Nimeiponda hiyo taaluma kivipi na imeniumbuaje?
Hmm...mbona ghadhabu nyingi kaka? Unajua ghadhabu huwa zina uwezo wa kufunika kabisa umakini wa mtu na hapa naona ndicho kilichotokea.
Mimi nilichokuomba unieleze ni kwa nini kuna hiyo kasumba. Na kama umenisoma kwa umakini basi utakuwa umegundua kwamba hapo uliponinukuu kuna maswali matatu ambayo yanahusiana.
Sawa, hata kama kasumba ni sawa na usasili (myth), lakini kama kuna watu ambao wana kasumba fulani fulani ni lazima hizo kasumba ziwe na chanzo. Haziweki tu kujitokeza kwa watu bila sababu.
Sasa, ni bora hata ungesema hujui chanzo chake ni nini kuliko kuanza kunishambulia kwa kuniita "coward". Ni uungwana unapoulizwa jambo, kama hulijui, unasema sijui. Lakini siyo kuanza kunishambulia kwa kuniita majina. Huo si uungwana hata kidogo.
Kwa hiyo, mimi sikusema kwamba unieleze. Nilikuuliza kama unaweza kueleza kwa nini kuna hiyo kasumba. Kuna tofauti kubwa tu kati ya kusema na kuuliza. Au alama za kuuliza hukuziona?
Baada ya mimi kuona wewe umesema hivyo, ndo nami nikauliza kwa nini kuna hiyo kasumba? Hukuwa na haja ya kunishambulia mimi kwa hasira. Ungesema tu hujui (kama hujui), basi. Lakini badala ya kufanya hivyo umenishambulia mimi. Hewala bwana.
Mbona umekaa mkao wa kujihami hami sana kana kwamba mimi nimekushutumu wewe kusema wasomi wa fani zingine hawajaongezeka? Nilichoandika mimi kilipanua tu kile ulichoandika wewe. Kuna kosa hapo?
Hapana kaka, mimi sijakuita hivyo hata kidogo. Ningeandika wewe ni "muumini wa hiyo dhana potofu kwamba wasomi ni wale walosomea sheria tu" basi ungekuwa na hoja. Lakini kwa kutumia neno 'unless' (sina hakika na tafsiri yake kwa Kiswahili katika huu muktadha) maana nzima ya sentensi ni sivyo ulivyoichukulia wewe.
Lakini sasa huna hoja kwa sababu (1) hujaonyesha umakini wowote ule katika kusoma na kuelewa nilichokiandika na hivyo kupelekea kufikia hitimisho ambalo linamakosa na (2) hakuna ukorofi wala upuuzi wowote ule katika nilichokiandika na kama upo basi ni wa kufikirika tu.
Nadhani ingekuwa ni vyema na busara kwa wewe kuanza kuufanyia kazi kwanza huu ushauri wako kabla hujaanza kuutoa kwa wengine. Unaonaje?
Hata mimi sijasema kuwa umesoma UDSM lakini nakiri kosa kwa kudokeza kuwa ulisoma hapo. Niwie radhi kwa hilo.
Mbona hata mimi sijasema kuwa wewe umesema hivyo. Kwa sababu jinsi unavyojihami unatoa taswira ya kana kwamba mimi nimesema kuwa wewe umesema hivyo. La hasha ndugu.
Wapi nimegeuza maneno yako ili kwa lengo la kuzua tafrani? Hilo la UDSM nimeomba radhi na nimekiri kosa langu. Punguza jazba ndugu. Sawa?
Nimeikashifu fani wapi? Na wewe kuniita mimi mpumba.vu bila kuonyesha wapi nimeikashifu hiyo fani na bila kuonyesha hiyo fani imeniumbua vipi, sijui hata nikuiteje aisee!!
You don't want to meet me anywehere in a court of law with your kind of elementary comprehension level and rudimentary arguing skills.
I'll eat your lunch, brother-man!