Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
sawa""Nyinyi ndio mnauziwaga uchawi na kuroga wenzenu.. sa kipi hako cha kukuvutia hadi uende inbox?
doh basi huyo alikuwa msukule..walimshindw wazee wa angaDunia hii inatisha Sana mkuu, kuna mdogo wangu sasa hivi ni marehemu aliwahi kupotea kijijini kwetu usiku ktk mazingira ya utata Sana, tulimtafuta kila sehemu hatukumwona, alikuwa na miaka 8 tu kipindi kile, tulipokata tamaa na kurudi nyumbani ili tujipange upya mida ya saa 9 alfajiri, marehemu mama alifungua chumba kilichokuwa kimefungwa muda mrefu na tukamkuta amekaa humo akiwa kimya haongei lolote, hadi alipokuja kuwa mtu mzima na kujitambua ,aligoma kabisa kusema alikuwa wapi hadi anafariki.
Mkuu Pole sana. Ni mwaka gani hii na ni wapi??Mi pia babu yang aliwahi toweka kimiujiza akimsindikiza mgeni..tulintafuta sana lakini hatukufanikiwa kumpata wote tulijua amefariki lakini kitu cha ajabu alirudi baada ya siku nne..alipoulizwa alikua wapi alisema alipotoka kumsindikiza mgeni ambaye alikua ni rafiki ake wa siku nyingi alijikuta anatokea sehem ambayo hakuifaham japo kulikua na watu waliokua wakimshangaa na walizungumza lugha ambayo hakuielewa wala hakuwahi kuisikia ila hakukumbuka ilikuaje mpaka akarudi tena...haikuchua muda alifariki..!!
Asante sana mkuu....tushapoa ilikua mwaka 1999 huko GeitaMkuu Pole sana. Ni mwaka gani hii na ni wapi??