Kisa cha Malaika JIBRIL. Nimesoma hadi nikapigwa na kibaridi flani

Kisa cha Malaika JIBRIL. Nimesoma hadi nikapigwa na kibaridi flani

Katika Utekelezaji wa Majukumu yake Mwenyezi Mungu muweza wa yote amekasimisha baadhi ya majukumu hayo kwa Malaika wake.

Sasa katika moja ya hao Malaika ndio huyu. Anaitwa ISRAEL A. S... Dah anatisha sana huyu kiumbe. Ndio aliyepewa jukumu la kutoa Uhai /roho na kupaa nazo kuzipeleka kwa Muumba.

Kisa chake hiki nimekikuta mahali nikaona nishare hapa kwa ndugu zangu Waislam na hata wasio waislam wapate Ukumbusho. Karibuni

Aliwahi kuulizwa malakul maut na ALLAH S.W Jee uliwahi kulia au kucheka pindi unapotoa roho za waja wangu?
Akajibu "niliwahi kulia, kucheka na kupatwa na fazaa".
Nilicheka siku moja nilipokwenda kwa mtu mmoja kuchukuwa roho yake nikamkuta anaongea na fundi wa viatu akimuambia nishonee vizuri nivae mwaka mzima, nitanunua vipya mwakani nikacheka na kuichukuwa roho yake kabla hajavivaa.

Na kilichoniliza ni siku Ulinituma kuchukuwa roho ya mwanamke mmoja aliekuwa pangoni peke yake akimnyonyesha mwanawe na hakuna mtu aliekuwa anajua mahali alipo basi nikaitoa roho yake huku mtoto akilia kwa uchungu na mimi nikalia.

Na kilichonipa fazaa ni siku ulionituma nikachukuwe roho ya mcha Mungu sana wakati nilipoingia chumbani mwake nikakuta chumba chake kimegubikwa na nuru nikapata tabu kumfikia nilipokuwa natoa roho yake fazaa kubwa ikanishika.
ALLAH S.W akamuuliza jee unamfahamu mtu huyo?
Akajibu malakul maut: lah simfahamu zaidi ya kuwa ni mwanachuoni.
ALLAH S.W akamuambia huyo ni yule mtoto aliyekuwa akinyonyeshwa na mama yake pangoni na ukaichukuwa roho ya mama yake.

Huyo ndio malakul maut anaewatenganisha wapendanao mama na mtoto wake, mtu na mkewe, mtu na rafiki yake mtu na mzazi wake.
Basi usimsahau malaika huyu hakika yeye hakusahau inapokuja amri kwake kaniitie mja wangu fulani basi hushuka kwa haraka na kutii amri ya ALLAH S.W tukumbuke ipo siku na saa atatutembelea wakati wowote saa yoyote dakika yoyote sekunde yoyote tukae tukilitaffakar hili kwani huenda chochote kile tunachokifanya kikawa ndio tendo letu la mwisho au ikawa ndio kauli ya mwisho
Tumuombe ALLAH S.W atupe khatma njema katika matendo yetu ya mwisho na atujaalie kauli yetu ya mwisho iwe LAAILAHA ILLA LLAH MUHAMMADU RASSULU-LLAH

AMIN.

FADHAKIR FAINNA DHIKRA TANFAUL MUUMININ.
Pongezi kwa atakayeisoma,
akaifahamu na akakimbilia
kuitendea kazi... na Allah
amjaze kheri atakayeituma hii kwa wengine.

ALLAH S.W akamuuliza jee unamfahamu mtu huyo?

Akajibu malakul maut: lah simfahamu zaidi ya kuwa ni mwanachuoni.


Hapa ni watu wawili wanapiga story au soga


Samahani mtoa mada 'Product ya Udsm' nina maswali yafuatayo

1)Malaika wanamuona Mungu ana kwa ana au uso kwa uso?????


2)Haya majina ya malaika Mungu aliwapa lini????Kwamba wewe jina lako ni hili na kazi yako ni hii????


ALLAH S.W
akamuambia huyo ni yule mtoto aliyekuwa akinyonyeshwa na mama yake pangoni na ukaichukuwa roho ya mama yake.


Kwa kutumia ubongo wako unamuona Mungu mwenye huruma hapo?????Au Mungu mwenye roho mbaya???
 
ndugu Jibril na Israel ni malaika wawili tofauti,Jibril kazi yake ni kuleta wahy kwa mtume Muhammad S.A.W huyo Israel yeye kazi ni moya kutoa roho zetu

Hivi hata maana ya neno israel huwa manaelezwa kweli humo madrasa,au mana karirishwa tu kwa sababu ya hate kwa wayahudi?
 
ALLAH S.W akamuuliza jee unamfahamu mtu huyo?

Akajibu malakul maut: lah simfahamu zaidi ya kuwa ni mwanachuoni.


Hapa ni watu wawili wanapiga story au soga


Samahani mtoa mada 'Product ya Udsm' nina maswali yafuatayo

1)Malaika wanamuona Mungu ana kwa ana au uso kwa uso?????


2)Haya majina ya malaika Mungu aliwapa lini????Kwamba wewe jina lako ni hili na kazi yako ni hii????


ALLAH S.W
akamuambia huyo ni yule mtoto aliyekuwa akinyonyeshwa na mama yake pangoni na ukaichukuwa roho ya mama yake.


Kwa kutumia ubongo wako unamuona Mungu mwenye huruma hapo?????Au Mungu mwenye roho mbaya???
1.kwa mujibu wa Qurani malaika wana space yao katika mbingu tofauti na Mwenyezi Mungu sasa katika maongezi yao mpaka malaika atekeleze Agizo manake anapewa Amri na Si lazima aonane Waonane.

2. Malaika walipewa majina kwa ajili ya Utambuzi kama wewe unavyopewa jina ili utambuliwe na wenzako
 
Umesoma andiko la mleta mada ajazungumzia mama wa kosovo wala vita.

Unaweza tupa ushahidi wa maneno, video, sautu au picha kuonesha ukweli wa ilo la kosovo maana umeleta mada nyingine kabisa
Nimeleta mfano tu
Najua haihusiani kabisa na mada hii ila nimekumbukia tu hiki kisa kwa sababu kiliandikwa na ku trend sana Kama hukusoma au kusikia basi tafuta kwa mda wako

Dunia hii kuna mengi ya kujifunza
 
Waislam YANI ISRAEL NYIE MMEMKOPI NA KUMUITA ISRAEL MTOA ROHO [emoji3] MUHAMADI ALAANIWE AISE HII DINI ALIWAINGIZA WATU CHAKA

YANI BABA YETU ISRAEL MNAMUITA ISRAEL MTOA ROHO - KWELI KURANI INAKOPI VITU KUTOKA BIBLIA KITABU CHA MCHONGO HICHO
 
Kuna watu ambao hawatakuwa interested na hili bandiko, sio kosa ila kupita kimya kimya watashindwa na waleta kebehi, matusi na unaweza shangaa kukawa na mjadala mkubwa Wa kuambatana na matusi kana kwamba Uzi umeletwa katika Questionnaire oriented kumbe Uzi umeletwa kama habari watu wasome wajue!
Tujue upumbavu? Ukileta upumbavu kwenye hadhira ya watu wengi jua utapingwa tu. ukitaka usipingwe kaeni nao huko kwenye nyumba zenu za ibada hakuna mtu atawafata huko.nahata akitokea nitaungana nanyi kumpinga sababu amewafata kwenye faragha yenu.
 
Kwa mujibu Qurani, kifo chochote kinachotokea roho hiyo anayeichukua ni huyo Malaika ISRAEL ... Hiyo kukatwa panga sijui ajali na mengineyo yote huwa ni sababu tu
Aisee hiz hadithi ukizisoma kama gazeti la udaku unaweza, kuamini kila kifo ni mpango wa mungu lkn ukisoma na kutafakari utagundua kua sio kila kifo ni mpango wa mungu na hii kuamini kila kifo ni mpango wa mungu imewafanya waafrica kua wajinga sana mm bnafsi siamini kua kila kifo ni mpango wa mungu vingine ni mipango ya binadamu wenyewe

Sent from my PRA-LA1 using JamiiForums mobile app
 
Tujue upumbavu? Ukileta upumbavu kwenye hadhira ya watu wengi jua utapingwa tu. ukitaka usipingwe kaeni nao huko kwenye nyumba zenu za ibada hakuna mtu atawafata huko.nahata akitokea nitaungana nanyi kumpinga sababu amewafata kwenye faragha yenu.
Relax body
 
Aisee hiz hadithi ukizisoma kama gazeti la udaku unaweza, kuamini kila kifo ni mpango wa mungu lkn ukisoma na kutafakari utagundua kua sio kila kifo ni mpango wa mungu na hii kuamini kila kifo ni mpango wa mungu imewafanya waafrica kua wajinga sana mm bnafsi siamini kua kila kifo ni mpango wa mungu vingine ni mipango ya binadamu wenyewe

Sent from my PRA-LA1 using JamiiForums mobile app
Sawa
 
ndugu Jibril na Israel ni malaika wawili tofauti,Jibril kazi yake ni kuleta wahy kwa mtume Muhammad S.A.W huyo Israel yeye kazi ni moya kutoa roho zetu
Ndio maana Mwislam hampendi Israel?
Nimeuliza tu nijue
Ostadhat Carleen waweza kujibu pia
 
Back
Top Bottom